Mtoa post hajui UGUMU wa multiple choice yeye anawaza huko s/msingi wanakooneshwa majibu na kuhisi wamebahatisha,na ukitaka kuuliza ugumu wake uliza wana UDSM ambao walikuwa hawakutani na Mc qns watakupa mrejesho wa mtihani,Acha bwana muuliple choice unaweza kuomba maji kwenye mtihani.
Leo mnasifia MCQs za vyuo vikuu wakat huo huo mnaponda utaratibu wa mitihan ya darasa la saba kuwa kwenye muundo wa MCQs na kusisitiza watoto inabid wakokotoe...! Watanzania bhana kwa unafiki hatujambo
Ni vyuo vya Tanzania tu wanaendekeza huu upuuzi mimi nimesoma UDSM (Bachelor Degree), Univ. of Cape Town (Master Degree) na South Hampton (Master ya 2) na Short courses vyuo vya Netherlands na USA sijawahi kuona huu upuuzi wa MULTIPLE CHOICE. Nimefanya utafiti vyuo vya Kenya & Uganda hawana huo utaratibu. Nyie wa-TZ endeleeni kujifariji tu na uj.Inga wenu
Bora ukutane na essay kuliko mcq...udsm ni chuo kigumu sana ikifuatia na mzumbe,tia pamoja dit.
Wadau, salaam!
Nimekutana na karatasi ya Maswali ya Mtihani uliopita mwaka wa 3 (Final Year) pale UDSM una maswali ya multiple choice kama 20 hivi na kila swali lina marks 1, hivyo mtu akipata maswali yote hata kwa ku-guess tu ana marks 20 tayari kati ya 60 anazotakiwa kupata katika University Exam (UE). Swali langu ni kwamba, wa level ya Chuo Kikuu (University) tena Mwaka wa 3 anayepewa multiple choice kweli tunaanda wataalamu wa aina gani?
Rai Yangu:
Ningeshauri vyuo vikuu vibadili mtindo huu wa kutunga maswali (Multiple Choice) maana unavutia (encourage) kubahatisha (guessing) bila kufikirisha akili ya mwanafunzi.
Najua hapa watakuja watu kuutetea, ooh idadi ya wanafunzi wamekuwa wengi ndo maana lecturers wanatunga multiple choice questions ili iwe rahisi kusahihisha lakini sababu hiyo tu haitoshi kuharibu wanachuo hawa ambao baada ya kumaliza hapo, wanaenda kupambana na wasomi wa Kenya, Uganda, Afrika Kusini & dunia nzima
secondar na chuo ni vitu viwili tofauti mcqs za chuo zinahtaji mtu uelewe vizuri consept ndo unaweza kupata,maana majibu yote ni kweli lakini pale kuna kweli zaidi, ukitaka kujua hilo kutana na dr Ananda pale udomwatu ni vigeugeu sana.Juzijuzi nyie wenyewe mlikua mnamlaumu na kumponda mama Ndalichako na NECTA kwamba kwa nini anawapa wanafunzi maswali ya MULTIPLE CHOICE leo kwa kua pepa ya aina hiyo wamepewa UDSM mnatetea! Tena sababu za kutetea ni zilezile walizokuwa wakitoa Necta. Ha huu unafki huu!
Ajabu sana inawezekana hujui lolote nini maana ya mtihani cha mno ni level of understanding.Nilikuwa Muce lakini kuna test Fulani darasa la watu 900 wa kwanza alikuwa na 12 out of 20 wengi sana zero mpaka tano.GPA udsm huwezi pata ya tano hebu uliza st Joseph na sauti kwenye essay kama za darasa la awali hadi aibu.Gpa hadi za tano.Udsm tunaoondoka na GPA chini ya 3.5 ndo kibao lakini wenzetu wengi wanatoka na zaidi ya 3.5