Kuvimba kwa tezi za Thyroid (Goita)

Kuvimba kwa tezi za Thyroid (Goita)

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Goita (Goiter) ni uvimbe unaotokea kwenye tezi ya thyroid inayopatikana sehemu ya mbele ya shingo.

49C76763-BC3C-451A-870B-D1CD3E97B1C4.jpeg


Tezi hii yenye umbo linalofanana na kipepeo huzalisha homoni za T4 na T3 ambazo huhusika kwenye kuratibu mifumo mbalimbali ya mwili ikiwemo joto, mihemko ya mwili, mapigo ya moyo na mmeng’enyo wa chakula.

Upungufu wa madini joto (Iodine) ndiyo chanzo kikubwa cha kutokea kwa ugonjwa huu. Wakati huu, tezi za thyroid huongezeka ukubwa ili kufidia upungufu uliopo, jambo ambalo huifanya ivimbe.

Sababu zingine kama uwepo wa kiasi kingi au kichache sana cha homoni za thyroid, maambukizi kwenye tezi za thyroid, saratani na ujauzito zinaweza kusababisha kutokea kwa Goita.

Dalili zake-
  • Uvimbe shingoni
  • Maumivu na Kukaza kwa shingo
  • Ugumu kwenye kupumua na kumeza chakula
  • Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
  • Uchovu usio na sababu
  • Kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi
  • Sauti kuwa ya mikwaruzo
  • Wakati mwingine, mishipa ya damu ya shingoni inaweza kuvimba pia na kusababisha mtu kujihisi kizunguzungu pindi anapoinua mikono yake juu
Kuna aina nyingi za Goita, lakini ile inayosababishwa na upungufu wa madini joto (Iodine) ndiyo huonekana kwa watu wengi. Hii ndiyo Goita unayoweza kuizuia.

Samaki wa baharini, maziwa pamoja na bidhaa zake, mayai pamoja na maini ya wanyama ni vyakula vyenye utajiri mkubwa wa madini joto (Iodine)

Aidha, hakikisha kila siku unapika chakula chako kwa kutumia chumvi iliyo ongezewa madini joto (Iodine) ili ujiweke salama. Unaweza kuitambua chumvi yenye madini haya kwa kusoma kifungashio chake kwanza kabla haujainunua.

Tiba ya tatizo hii ipo, mgonjwa anapaswa kufika hospitalini kwa uchunguzi na matibabu.

Chanzo: Cleveland Clinic
 
Goita (Goiter) ni uvimbe unaotokea kwenye tezi ya thyroid inayopatikana sehemu ya mbele ya shingo.

View attachment 2378580

Tezi hii yenye umbo linalofanana na kipepeo huzalisha homoni za T4 na T3 ambazo huhusika kwenye kuratibu mifumo mbalimbali ya mwili ikiwemo joto, mihemko ya mwili, mapigo ya moyo na mmeng’enyo wa chakula.

Upungufu wa madini joto (Iodine) ndiyo chanzo kikubwa cha kutokea kwa ugonjwa huu. Wakati huu, tezi za thyroid huongezeka ukubwa ili kufidia upungufu uliopo, jambo ambalo huifanya ivimbe.

Sababu zingine kama uwepo wa kiasi kingi au kichache sana cha homoni za thyroid, maambukizi kwenye tezi za thyroid, saratani na ujauzito zinaweza kusababisha kutokea kwa Goita.

Dalili zake-
  • Uvimbe shingoni
  • Maumivu na Kukaza kwa shingo
  • Ugumu kwenye kupumua na kumeza chakula
  • Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
  • Uchovu usio na sababu
  • Kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi
  • Sauti kuwa ya mikwaruzo
  • Wakati mwingine, mishipa ya damu ya shingoni inaweza kuvimba pia na kusababisha mtu kujihisi kizunguzungu pindi anapoinua mikono yake juu
Kuna aina nyingi za Goita, lakini ile inayosababishwa na upungufu wa madini joto (Iodine) ndiyo huonekana kwa watu wengi. Hii ndiyo Goita unayoweza kuizuia.

Samaki wa baharini, maziwa pamoja na bidhaa zake, mayai pamoja na maini ya wanyama ni vyakula vyenye utajiri mkubwa wa madini joto (Iodine)

Aidha, hakikisha kila siku unapika chakula chako kwa kutumia chumvi iliyo ongezewa madini joto (Iodine) ili ujiweke salama. Unaweza kuitambua chumvi yenye madini haya kwa kusoma kifungashio chake kwanza kabla haujainunua.

Tiba ya tatizo hii ipo, mgonjwa anapaswa kufika hospitalini kwa uchunguzi na matibabu.

Chanzo: Cleveland Clinic
Vipi ukiachana na matumizi ya chumvi kabisa, badala yake ukatumia hivyo vingine tu kama samaki maziwa nk.
 
Vipi ukiachana na matumizi ya chumvi kabisa, badala yake ukatumia hivyo vingine tu kama samaki maziwa nk.
Chumvi hutoa uhakika mkuwa zaidi wa kupata madini joto kwa kuwa wazalishaji wote hupaswa kuyaongeza kabla haijaingizwa sokoni.

Nafikiri ni muhimu zaidi kutumia chumvi as uhakika kwa kupata madini joto (kuliko sehemu zingine) upo guaranteed
 
Chumvi hutoa uhakika mkuwa zaidi wa kupata madini joto kwa kuwa wazalishaji wote hupaswa kuyaongeza kabla haijaingizwa sokoni.

Nafikiri ni muhimu zaidi kutumia chumvi as uhakika kwa kupata madini joto (kuliko sehemu zingine) upo guaranteed
Nimekuelewa mkuuu.

Sasa huwa inakuwaje kwa wale wagonjwa wa hypertension waliokatazwa kutumia chumvi, maana pamoja na kukatazwa kutumia chumvi sijawahi kuona wanaugua goita
 
Mzizi mkavu tuelezee mbona mwalimu wako Dr sebi hajawahi zungumzia hii
 
Back
Top Bottom