Kuwa makini na aina hii ya Utapeli

GuyFromArusha

Member
Joined
May 10, 2016
Posts
71
Reaction score
84
Juzi juzi nilikua napitia pitia ajira online nikakutana na hii moja toka website ya Zoom Tanzania. Kampuni inaitwa DELIP ni NGO japo nlipojaribu kuifanyia utafiti sikuweza pata chochote online nikawa nahisi ni ya kiutapeli tapeli. Lakini kwakuwa ni kutuma tu cv ikabidi nitume sasa jana nkatumiwa message hii.


Hello, am Mr. KAUGA from DELIP NGO Dar, tupo kwenye kikao tunapitia cv za kuinterview for PROJECT OFFICER post, CV yako ni nzuri nitakusaidia upate hii kazi kwa masharti yafuatayo, salary ni 1,300,000/=(take home) ukilipwa mshahara wa kwanza utanipa laki 4 kwa kukusaidia, na kabla ya saa 11 na nusu jioni leo uwe umetuma Tsh. elfu 35 by tigopesa kwenda namba hiihii ili nimpe mtu wa interview atanipa maswali nitakutumia leoleo kwenye email, ntakupigia simu nikitoka kikaoni.

Hii inaonesha wazi kwamba hawa jamaa ni matapeli. Wanatafuta desperate, ill informed job seekers na kuahidi watawataftia kazi lakini utume kwanza hela. Naweza fikiria watu wengi tu ambao wangedakwa kwenye mtego huu.. Kuweni makini!!!
 
Bado wanatapeli watu kwa style hii? Nadhani watafute mbinu Mpya.
 
if you are competent enough, then what is the use of paying for a job....wanaoliwa ni vilaza ambao wanapenda vya dezo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…