Kuwafanyia watoto DNA test

Ooooh!! I realy like this comment. Mapenzi ni 'imani' tu, ikikosekana hata DNA haina maana
 
how did you take this Sir?

Mh, nimeichukulia kawaida maana mimi ni wale ambao wanaamini binadamu na hulka ni momentarily na marriage is an institution which was generated by selfish philosophers wishing to retain all teh qualities of beauties around
 

MJ, mimi naamini kwamba kama mwanamke ni muaminifu, basi atamshika mkono mumewe na kuelekea kupima... kitendo cha nyie wenzetu kupima ndio kinachekesha

Mbona mkituuliza tulikuwa na nani huwa tunasema? au ukisikia mie nina bibi nje huwa natoa ruhusa ya counter-checking?
 
ahahahha...ati hutaki comments lazima alikuwa kwenye ligi pia....si unaju tu mambo ya kwaya 😉

Nilikuambia sitaki comments. Ntake radhi. Am counting 8...7....6....
 
i understand how u feel baby but if unajiamini uoga wa nini??? na kwa nini ujihisi vibaya? ningekuwa mimi tena ningesikia raha kwa vile kuanzia siku hiyo ndio atakuwa ananiamini zaidi na zaidi.

Ndio maana ninasema ningekwenda kupima ndio but ningeumia sana moyoni mwangu ingawa ndio ni njia nzuri ya kumfanya akuamini zaidi but lol it pain kwa kweli. Hebu imagine umekuwa masomoni kwa mwaka mzima au miezi sita, then unaporudi home kitu cha kwanza wifi anakwambia mwende mkapime UKIMWI kwanza au magonjwa ya Zinaa wakati mlishacheck kabla ya ndoa.
 
Ndio maana kwangu mimi naona mapenzi kuwa ni imani zaidi ya DNA, ukiwa na imani na mpenzio huhitaji DNA. Kuhitaji DNA ni dalili za mashaka kwa mwenzi
 

........ Ni kweli kuwa haieleweki lakini nikifikiria hiyo linalokuja moja kwa moja ni kuwa huyu ananishuku natoka nje ya ndoa na kuomba dna kwa wattoto ni mbinu tu ya kutaka kunikamata. So hata kama ni mwaminifu kivije nitahuzunika. Kama alivyosema mdau hapo juu mapenzi ni imani na ndio maana mie naishi na wewe kwa kuwa nakuamini otherwise niwe nakucheck spermcount kila unapotoka safari
 
Ndio maana kwangu mimi naona mapenzi kuwa ni imani zaidi ya DNA, ukiwa na imani na mpenzio huhitaji DNA. Kuhitaji DNA ni dalili za mashaka kwa mwenzi

Aksante Sipo. Hiki ndicho ninachopata shida kukielezea kieleweke hapa!
 
Hahaha! Leo mzee wa malangueji amazikong'oli Senksi za malijendi wa mambo ya malavidavi. Hii inahitaji thread yake.

Legend huyu anachangiaga kila thread kuna wale wenye msimamo mkali na presha presha/SIHASA hao mh!..........
 

MJ1

kama ulivyosema, mapenzi ni imani, sasa jiulize kama ni imani.... mbona mnataka kukataza ushuhuda?

Ushuhuda wa mapenzi ni pamoja na DNA, na si blind beliefs/trust
 
Bro mambo vipi? leo umetumia luga ambayo naweza kucomment.

Mtiriko wa point mzuri ila hapo kwenye red kuna utata.

Kama kuna mtu mwenye utata for sure ni wewe unayeusema utata bila kuuelezea, na hivyo kuongeza utata badala ya kupunguza.

Utata uko wapi?

Mimi nimeuliza swali, sijatoa statement.

Kuna utata kuuliza? Narudia, nioe ili iweje? Kuna kitu gani cha msingi ambacho kinanilazimisha mimi kuoa?
 
Ha ha ha Hopo kwenye Red umenifurahisha ila Majibu ya hili mbona mengi...Atakwambia Niliota usiku teh teh teh
 
Aksante Sipo. Hiki ndicho ninachopata shida kukielezea kieleweke hapa!

Kwa sisi wenye kaufahamu ka falsafa kidogo ngoja tutoe definition za IMANI NA MATUMAINI kwa luga nyepesi kabisa.

IMANI-Ni kutaka mambo/jambo unalotaka liwe excactly kama unavyotaka. Hata kama sivyo.

MATUMAINI-Ni kutarajia jambo flani litoke kama unavyotaka hata kama halitatokea.

Kama kuna njia ya kisayansi haya yanabakia kwenye dini tu.
 
Aksante Sipo. Hiki ndicho ninachopata shida kukielezea kieleweke hapa!
MJ1, in the long run kitaeleweka tu, wanandoa hawatakiwi kuishi kama nungu-nungu otherwise there was force behind your marriage
 
MJ1

kama ulivyosema, mapenzi ni imani, sasa jiulize kama ni imani.... mbona mnataka kukataza ushuhuda?

Ushuhuda wa mapenzi ni pamoja na DNA, na si blind beliefs/trust
KUsema ukweli MTM sijui ninaelewa kuwa DNA ina umuhimu but nadhani kile kinachopimwa au maudhui ya upimaji wake ndo unaonifanya niwe mzto kuuruhusu ushukuda huo. Ingekuwa DNA inapimwa kama inavyopimwa damu kujua blood group ambapo audhui yake ni kuwa kama mtoto atapata tatizo linalomfanya aongezewe damu iwe rahisi maudhui ya DNA ni kujua kama ni kweli mtoto ni wako au lah- yaani kwa kifupi ni kujua kama mkeo amekuwa akicheat au la!! nafikiri ndo mana huwa ninakuwa na moyo mzito kidogo. Mimi mwenzangu alikwenda kumcheck mwanetu peke yake hakunihusisha but alivyokujaniambia niliumia sana pamoja na kuwa ninajiamini katika suala la uaminifu but inanihaunt hadi leo- yaani huwa najiuliza aliwaza nini hasa hadi akaamua kwenda kucheck?--- sipati jibu hadi leo pamoja na majibu lukuki alonipa
 
Ndio maana kwangu mimi naona mapenzi kuwa ni imani zaidi ya DNA, ukiwa na imani na mpenzio huhitaji DNA. Kuhitaji DNA ni dalili za mashaka kwa mwenzi

hii imani samtaimu ndio inaleta balaa ndani ya nyumba. kuna vile viruka njia vijike kwa vidume huwa vinafanya mambo yao na ukiviuliza vinajifanya kuja juu aaargh sasa hatuaminiani? muulizaji ukirudi matawi ya chini neksti day anaendeleza libeneke. hapo njomba utakuwa umekwisha!!!!! , zaifu yako imejulikana!!. kama jana alirudi nyumbani sunseti kesho anarudi sunraiz. lakini uskonde tupo washauri wa kujitolea hapa jf. likikutokezea hili balaa usisite kuliripoti hapa jukwaa la mahusiano.
 
Ha ha ha Hopo kwenye Red umenifurahisha ila Majibu ya hili mbona mengi...Atakwambia Niliota usiku teh teh teh
Na ndio maana nikasema inakuwa vigumu kueleweka. Assume hakuna kuota wala kufanya sef service-
 

Nafikiri ndio maana kukaletwa ule msemo wa kitanda hakizai haramu au?
 

Nashukuru mkuu tuko pamoja


 
MJ1

kama ulivyosema, mapenzi ni imani, sasa jiulize kama ni imani.... mbona mnataka kukataza ushuhuda?

Ushuhuda wa mapenzi ni pamoja na DNA, na si blind beliefs/trust
Lakini Mkuu, ushuhuda wa nini? Wewe umelea mimba mpaka mtoto amezaliwa, ina maana siku zote ulikuwa na wasiwasi na mimba ya mtoto husika. Au unataka u-create fear situation kwa mkeo hasitoke nje ya ndoa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…