Kuwait dinars yaongoza (Rates exchanges)

Kuwait dinars yaongoza (Rates exchanges)

tamimusalim

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2014
Posts
1,822
Reaction score
498
ImageUploadedByJamiiForums1428292342.892920.jpg
Ingawa si maarufu sana hapa nchini kwetu, rakini kwa mataifa ya ghuba hata asia, ni pesa yenye nguvu , kulinganisha hata euro, pound, dutch mark , hata dollar, hii ni pesa ya nchini kuwait inajulikana kama dinar, kuwait ni taifa la kiarabu na kiislam ambalo 90% ya uchumi wake utegemea uchimbaji wa mafuta ,
ImageUploadedByJamiiForums1428292641.725893.jpg
leo hii dinar 1 ni sawa na tsh 5660/= katika benk kuu hapa tanzania, fursa yetu kuchangamkia biashara kati yetu na taifa hili lisilojulikana sana hapa nchini ila lenye uchumi mkubwa sana,
 
Hizo noti zina thamani ndani ya nchi zao na nchi zinazopeleka wafanyakazi kwa wingi kwao kama Pakistan, Bangladesh, India na Ufilipino.

Mara nyingi huwezi kubadili fedha zao nje kirahisi kama pesa za Japan na Uswisi.

Hata Oman, Rial yao ina nguvu sana
(1 Omani Rial = 2.6 USD). Lakini sijaweza kubadilisha noti zao nilivyofika Bangkok, Thailand. Nilijaribu exchanger wengi airport na mjini bila ya mafanikio.

Hata Manila, Ufilipino, siyo money exchanger wote wanazikubali sarafu za Kuwait na Oman.
 
View attachment 240786 Ingawa si maarufu sana hapa nchini kwetu, rakini kwa mataifa ya ghuba hata asia, ni pesa yenye nguvu , kulinganisha hata euro, pound, dutch mark , hata dollar, hii ni pesa ya nchini kuwait inajulikana kama dinar, kuwait ni taifa la kiarabu na kiislam ambalo 90% ya uchumi wake utegemea uchimbaji wa mafuta , View attachment 240788 leo hii dinar 1 ni sawa na tsh 5660/= katika benk kuu hapa tanzania, fursa yetu kuchangamkia biashara kati yetu na taifa hili lisilojulikana sana hapa nchini ila lenye uchumi mkubwa sana,

wachumi waje hapa wanisaidie. uchumi wa Japan uko juu sana lakin hela Yao haina nguvu sana. ukinisaidia mimi utakuwa umemsaidia na huyu ndugu yangu.
 
wachumi waje hapa wanisaidie. uchumi wa Japan uko juu sana lakin hela Yao haina nguvu sana. ukinisaidia mimi utakuwa umemsaidia na huyu ndugu yangu.

Kweli kwani hili hata mi nalishangaa sana
 
Kuna vitu vingi vinahusika na thamani ya fedha ya nchi. Nitajaribu kukupa baadhi yake.

Kwa kifupi, uchumi wa Japan ni wa tatu mkubwa duniani baada ya Marekani na China.

Ndio maana noti ya Japan ya ¥5000 ni sawa na $42 na noti yetu ya Tshs. 5000 ni sawa na $2.75. Sasa utasema Yen haina nguvu hapa?

Thamani ya fedha ya nchi inategemea na ukubwa wa nafasi ya nchi katika biashara za kimataifa (uzalishaji na mauzo yake ndani na nje ya nchi).

Dunia ya leo imeungana sana kibiashara. Matokeo ya uchumi wa nchi moja inaathiri nchi nyingine zinazofanya naye biashara. Kwa mfano, Marekani akipunguza riba ili watu wakope kirahisi katika soko baadhi ya wawekezaji wanahamisha fedha nchi nyingine iliyo na riba zaidi katika benki kwa manufaa ya faida ya haraka.

Kwenye fujo za vita, pesa inaweza kukimbia nchi na kwenda kwenye nchi zilizotulia.

Miaka 10-15 iliyopita, wafanyabiashara wengi walihamisha pesa zao Japan kwa kununua YEN kwa sababu kama hizo na kuifanya fedha yake ipande thamani sana mpaka kufikia Yen 70 kwa dola kutokana na hali ya kivita Mashariki ya Kati na machafuko wa kiuchumi wa bara la Ulaya.

Serikali ya Japan ikaingilia kwenye soko na kununua dola na kumwaga yen kwenye soko ili ijizungushe na ishushe thamani ya Yen.

Nchi kama inazalisha sana na kuuza nje kama Japan, bidhaa zake zinakuwa ghali nje kama pesa yao ikipanda thamani sana. Wafanyabiashara wanapenda Yen iwe Kati ya ¥100-125 kwa dola.

Fedha ikishuka thamani vitu vya nje vinapanda bei na kusababisha mfumuko wa bei katika soko. Hapo serikali inaweza kuamua kupunguza matumuzi kama ya kujenga barabara au kupandisha riba ili watu wasizungushe pesa kwenye uchumi na kuweka pesa benki au kupandisha kodi. Pia, wanaweza kupunguza kuchapisha pesa mpaka ipande thamani au kununua pesa za kigeni katika soko kwa wingi.

Pesa ikiwa na nguvu sana, inadhuru mauzo ya nje na kuleta deflation. Vitu havipandi bei ndani ya nchi na wafanyabiashara kulazimika kwenda nje kupanua masoko kwa kukosa faida kubwa nyumbani na kuacha uchumi wa nyumbani kuning'inia kama ilivyokuwa Japan miaka mingi kabla ya Waziri Mkuu wao Abe kujaribu kuongeza mfumuko wa bei kwa kumwaga YEN kwa matrilioni kwenye soko kwa njia ijulikanayo sasa kama "Abenomics".

Nitaishia hapo kwa sasa. Nina imani watakuja wengine kukusaidia uelewe zaidi kuhusu "monetary and fiscal policies" za uchumi wa nchi.
 
View attachment 240786 Ingawa si maarufu sana hapa nchini kwetu, rakini kwa mataifa ya ghuba hata asia, ni pesa yenye nguvu , kulinganisha hata euro, pound, dutch mark , hata dollar, hii ni pesa ya nchini kuwait inajulikana kama dinar, kuwait ni taifa la kiarabu na kiislam ambalo 90% ya uchumi wake utegemea uchimbaji wa mafuta , View attachment 240788 leo hii dinar 1 ni sawa na tsh 5660/= katika benk kuu hapa tanzania, fursa yetu kuchangamkia biashara kati yetu na taifa hili lisilojulikana sana hapa nchini ila lenye uchumi mkubwa sana,

Hata sisi tukianza kuchimba mafuta tunaweza kurudi enzi zile za pauni
 

Attachments

  • IMG_13020830796799.jpeg
    IMG_13020830796799.jpeg
    33.6 KB · Views: 467
Yen 5000 ni sawa sawa na US$42.

Shilingi 5000 za Tanzania ni sawa na US $ 2.75.

Nilitaka kumwonyesha Mkuu juu hapo kuwa pesa ya Japan ina nguvu sana duniani na kuheshimika sana.

Nadhani alifikiri iwe yen 2 au 3 kwa dola moja kuonyesha nguvu ya uchumi wa Japan kama vile dola moja inaponunua Yuan 6 ya China.

Yen 2 ni kama senti mbili kwao . Haimaanishi pesa ya Japan haina thamani.

Ukisoma pengine Dola moja kama Yen SENTI Mia na ushirini itasaidia kuona picha vizuri badala ya ¥120 kwa dola MOJA japokuwa rate yote ni sawasawa.
 
Hata sisi tukianza kuchimba mafuta tunaweza kurudi enzi zile za pauni

Siyo rahisi kabisa.

Jitahidi kuelewa maswala ya uchumi.

Kwanza, hatuna mafuta ya kuchimba.

Tanzania kuna gesi (LNG) nyingi na hata hivyo, serikali imetangaza mapato ya baadae ya kama $3 Bilioni kwa mwaka watapomaliza ujenzi baina ya 2017 na 2022.

Pia, bei huenda ikipanda au kushuka katika miaka 25- 30 ya Uzalishaji mpaka kisima kukauka.

Kupanda kwa thamani ya fedha ya nchi inahitaji uwe mzalishaji wa vitu mbalimbali vinavyotumiwa duniani, siyo tu gesi.

Kufika katika Maendeleo ya nchi kama Malaysia au Afrika Kusini, tunahitaji uzalishaji wa $300 bilioni. Sasa tunazalisha kama $40 bilioni. Tutafika tukijipanga vizuri, lakini safari ni ndefu.

Kumbuka, Japan hana gesi wala mafuta. Ni uzalishaji tu wa vitu kila kona ya dunia wanavitumia.
 
Japan wanakomaa kushusha thamani ya Yen we we unasifu hao wasiojua uchumi?
 
Japan wanakomaa kushusha thamani ya Yen we we unasifu hao wasiojua uchumi?

Inakomaa kushusha thamani ya yen ili bidhaa zake zinunuliwe kirahisi!maana strong yen will hurt the jananese economy!..yen ikipanda dhidi ya us$..gari lililokuwa linauzwa us$7000..litauzwa us$9000..wanunuzi wataenda kwingine kutafuta unafuu wa bei..hiyo ni kwa industrial goods zote!
 
wachumi waje hapa wanisaidie. uchumi wa Japan uko juu sana lakin hela Yao haina nguvu sana. ukinisaidia mimi utakuwa umemsaidia na huyu ndugu yangu.

japan huwa wanatumia mfumo wa kushusha thamani pesa yao ili kuinua uchumi wao. Wana magari, spare parts, n.k nchi nyingi sana duniani. Sasa kama upo Tanzania kwa mfano na una bajeti ya kununua gari. Una nafasi ya kununua gari ya mwingereza, mkorea, mjapani, mhindi, mjerumani n.k. Lakini utagundua kwanba pesa yako hiyo ya Tanzania inaweza kununua gari zuri ya kijapan kuliko gari ya mwingereza. Kwanini? Sababu ukiibadili pesa yako kwenda Japanese yen utapata yen za kutosha kuliko kiasi cha dola au pound. Kwa ufupi wajapani hushusha thamani ya pesa yao ili waweze uza zaidi bidhaa zao dunia nzima
 
Siyo rahisi kabisa.

Jitahidi kuelewa maswala ya uchumi.

Kwanza, hatuna mafuta ya kuchimba.

Tanzania kuna gesi (LNG) nyingi na hata hivyo, serikali imetangaza mapato ya baadae ya kama $3 Bilioni kwa mwaka watapomaliza ujenzi baina ya 2017 na 2022.

Pia, bei huenda ikipanda au kushuka katika miaka 25- 30 ya Uzalishaji mpaka kisima kukauka.

Kupanda kwa thamani ya fedha ya nchi inahitaji uwe mzalishaji wa vitu mbalimbali vinavyotumiwa duniani, siyo tu gesi.

Kufika katika Maendeleo ya nchi kama Malaysia au Afrika Kusini, tunahitaji uzalishaji wa $300 bilioni. Sasa tunazalisha kama $40 bilioni. Tutafika tukijipanga vizuri, lakini safari ni ndefu.

Kumbuka, Japan hana gesi wala mafuta. Ni uzalishaji tu wa vitu kila kona ya dunia wanavitumia.

mkuu sijasoma post yako hata kidogo ila nahisi kama umeongea pumba flani ila sina uhakika sana... mtazamo
 
Japan wanakomaa kushusha thamani ya Yen we we unasifu hao wasiojua uchumi?

Nadhani umepata jibu tayari juu.

Kwa kuongezea, uchumi wa Japan ni mkubwa sana. Kuna factors nyingi za kuangalia uchumi unasaidiwa vipi na serikali ya Japan.

Kwa mfano, kodi ya mauzo ni ndogo kusaidia jamii na biashara. Marekani kutegemea na mkoa, unalipa kama 15%. Japan ni 8% tena wamepandisha juzi tu. Ilikuwa 5% tangu 1997, na kabla yake ilikuwa 3%.

Kama una watoto, hulipi hata senti tano ukipata mshahara chini ya $100,000 kwa mwaka au una mkopo wa nyumba benki.

Mkopo benki ina riba siyo zaidi ya 2.5% kwa mwaka na wanakupa miaka 25 kulipa. Unaweza kununua nyumba kwa malipo ya $600 kwa mwezi.

Shule ni bure za serikali. Unalipa chakula na uniform tu.

Mama wa nyumbani akifanya kazi part-time, halipi kodi kama ni chini ya $1000 kwa mwezi.

Ni lazima uangalia picha kwa ukubwa wa factors zote kujua jinsi gani uchumi unasaidiwa na serikali yao.
 
mkuu sijasoma post yako hata kidogo ila nahisi kama umeongea pumba flani ila sina uhakika sana... mtazamo

Wakati wewe mwenyewe huna uhakika "pumba" gani nimeandika wala kushindwa kunisoma, ila "unahisi" tu, huoni kwamba wewe ndio unaleta upumba hapa?

Katika mada, lazima utoe sababu za msingi unazozipinga, siyo hisia. Hisia hazina nafasi katika hoja, labda kwenye vijiwe vya kahawa.

Jipange upya ili unielimishe.
 
Kweli kwani hili hata mi nalishangaa sana
Japan wanakomaa kushusha thamani ya Yen we we unasifu hao wasiojua uchumi?
wachumi waje hapa wanisaidie. uchumi wa Japan uko juu sana lakin hela Yao haina nguvu sana. ukinisaidia mimi utakuwa umemsaidia na huyu ndugu yangu.

Kuwait wao uchumi wao unategemea mafuta wana export Oil, wanajua demand ya Oil mara zote iko bei ipande au ishuke kutokana na uhitajikaji wake duniani, Japan wao wanategemea sana magari, vifaa vya umeme na vitu vingine, kwa ujumla inabidi waweke bei kiushindani na nchi nyingine wanaozalisha product hizo hizo.

Kumbuka kupanda kwa thamani ya hela kunafanya export inakuwa ya gharama sana na import inakuwa cheap, Kuwait sababu wanajua soko la mafuta lipo hawajali sana kuhusu bei kuwa juu na wanafaidika na mapato wanayopata kwa kuuza katika bei ya juu na pia wanapata cheap imports maana thamani hela yao iko juu sana. Ndio maana mara zote Kuwait malipo ya imports ni madogo kuliko mapato ya exports (wana balance of payment and balance of trade surplus).

Kusema Kuwait hawajui uchumi Nyakageni ni kukosea, Kuwait ina asilimia kumi ya mafuta duniani, nusu ya pato (GDP) la taifa la Kuwait linatokana na mafuta, asilimia 95 ya mapato yao yanatoka kwenye mafuta. Wameshikipilia mpini so wanaweza vuta wanavyotaka, mpaka pale nchi nyingine zitapoanza kuzalisha mafuta.

Issue ya kuwa unachaguaje thamani ya hela yako inatokana na unazalisha nini, sio ukubwa wa pato bali ushindani katika soko la dunia. Hicho ndio kinatoafutisha Yen (Japan) na Dinar (Kuwait).
 
Last edited by a moderator:
Nadhani umepata jibu tayari juu.

Kwa kuongezea, uchumi wa Japan ni mkubwa sana. Kuna factors nyingi za kuangalia uchumi unasaidiwa vipi na serikali ya Japan.

Kwa mfano, kodi ya mauzo ni ndogo kusaidia jamii na biashara. Marekani kutegemea na mkoa, unalipa kama 15%. Japan ni 8% tena wamepandisha juzi tu. Ilikuwa 5% tangu 1997, na kabla yake ilikuwa 3%.

Kama una watoto, hulipi hata senti tano ukipata mshahara chini ya $100,000 kwa mwaka au una mkopo wa nyumba benki.

Mkopo benki ina riba siyo zaidi ya 2.5% kwa mwaka na wanakupa miaka 25 kulipa. Unaweza kununua nyumba kwa malipo ya $600 kwa mwezi.

Shule ni bure za serikali. Unalipa chakula na uniform tu.

Mama wa nyumbani akifanya kazi part-time, halipi kodi kama ni chini ya $1000 kwa mwezi.

Ni lazima uangalia picha kwa ukubwa wa factors zote kujua jinsi gani uchumi unasaidiwa na serikali yao.

Mkuu Nitakutafuta nina mpango wa kuja kutafuta hela Japan , kama kazi za ndani unakula USD 1,000 kwa mwezi huko kuna unafuu,kama unapata chini ya 100,000 usd kwa mwaka haukatwi kodi wakati huku ukianzia usd 350 kwa mwaka unakatwa kodi,vipi ninaweza nika-make fedha huko Tokyo kwa kupiga BOX?
 
Inakomaa kushusha thamani ya yen ili bidhaa zake zinunuliwe kirahisi!maana strong yen will hurt the jananese economy!..yen ikipanda dhidi ya us$..gari lililokuwa linauzwa us$7000..litauzwa us$9000..wanunuzi wataenda kwingine kutafuta unafuu wa bei..hiyo ni kwa industrial goods zote!

Well said, well elaborated. Nimependa jinsi ambavyo umetumia nafasi ndogo maelezo mazuri!
 
Mkuu Nitakutafuta nina mpango wa kuja kutafuta hela Japan , kama kazi za ndani unakula USD 1,000 kwa mwezi huko kuna unafuu,kama unapata chini ya 100,000 usd kwa mwaka haukatwi kodi wakati huku ukianzia usd 350 kwa mwaka unakatwa kodi,vipi ninaweza nika-make fedha huko Tokyo kwa kupiga BOX?

1. Kuna scholarship za kumwaga. Omba ubalozi wa Japan. Ukifaulu, unaweza kuishi Japan baada ya masomo yako. Wanahitaji watu, raia hawazai.

2. Funga ndoa na Mjapani. Viza ya ndoa inakuruhusu kufanya kazi yoyote. Baada ya miaka 5, unapata "green card" ya Kijapani. Ukifaulu mtihani wa Uraia ( kwa kijapani) unapata pasipoti yao ukipenda.

3. Kazi za BOX zipo nyingi. Inahitaji elimu ya Kijapani. Wananchi wengi hawajui Kiingereza.

Wageni wachache sana, ila lugha ndiyo matatizo. Kuandika Kijapani ni balaa tupu lakini kuongea siyo tabu sana. Unaweza kujifunza mwenyewe katika mtandao.

4. Kodi hukatwi ndani ya kiasi hicho kama una watoto tu au umekopa kununua nyumba.

Kila la heri.
 
Back
Top Bottom