Kuwarudisha Ndani Washitakiwa Kwa Madai Mahakama Haina Uwezo Wa Kusikiliza Kesi Hiyo, Ikoje?

Kuwarudisha Ndani Washitakiwa Kwa Madai Mahakama Haina Uwezo Wa Kusikiliza Kesi Hiyo, Ikoje?

G4rpolitics

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2015
Posts
4,369
Reaction score
5,248
Ndg Wanajamvi.
Siyo mara ya kwanza kusikia hii hoja pale ambapo mtu anakabiliwa na kesi fulani na kuambiwa kuwa mahakama haina uwezo kusikiliza hilo shitaka, kinachonikera zaidi ni kwa nini mtu asipelekwe moja kwa moja hadi sehemu husika hadi azungushwe, wengine wanapigwa kalenda hadi miezi minne ndo wanapelekwa panapohusika utafikiri hizo mahakama za kusikiliza hiyo kesi ziko nje ya nchi. Wanasheria tunaomba msaada wenu..
 
Hata mimi nashangaa huu upuuzi, kwani DPP aliyesema mtu ashitakiwe hajui kesi inaenda mahakama ipi?! Wanasheria tusaidieni.
 
Hata mimi nashangaa huu upuuzi, kwani DPP aliyesema mtu ashitakiwe hajui kesi inaenda mahakama ipi?! Wanasheria tusaidieni.
Inakera sana na mtu anaweza akasota huko miezi na miezi na anapelekwa huko huko, kufata nini kama haina uwezo huo?
 
Huwa ni kuwakomoa tu wahusika especially kama walishawahi kuwa quoted somewhere kwamba wao hawawezekani. Visasi na kuonyeshana umwamba ndo mpango mzima

Si alituaminisha kwamba kwake yeye ukiiba huchukui round na mahakama zikawa urged kuhukumu fasta bila kupoteza muda?
 
Kuna vitu watu wanashindwa kuelewa. Siyo kwamba DPP hajui kesi hiyo inaenda wapi ni anafahamu. Kuna baadhi ya makosa yanasikilizwa mahakama kuu. Ili ifike mahakama kuu lazima wafuate procedures kwanza kesi hizo zinafunguliwa mahakama ya chini yake. Mpaka pale upelelezi utakapo kamilika na mtu huyo amefanyiwa kitu kinaitwa "Commital", kesi hiyo ndipo itakapo hamishiwa mahakama kuu na kuanza kusikilizwa. Na ndio maana mtu atosemewa shtaka katika mahakama hiyo ya chini lakini ataambiwa asijibu chochote kwasababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza. Na kama kosa hilo halidhaminiki mtu huyo atarudishwa rumande. Ikumbukwe kuwa office ya DDP haifanyi upelelezi siyo kazi yake hiyo ni kazi ya Office ya DCI.
 
Kuna vitu watu wanashindwa kuelewa. Siyo kwamba DPP hajui kesi hiyo inaenda wapi ni anafahamu. Kuna baadhi ya makosa yanasikilizwa mahakama kuu. Ili ifike mahakama kuu lazima wafuate procedures kwanza kesi hizo zinafunguliwa mahakama ya chini yake. Mpaka pale upelelezi utakapo kamilika na mtu huyo amefanyiwa kitu kinaitwa "Commital", kesi hiyo ndipo itakapo hamishiwa mahakama kuu na kuanza kusikilizwa. Na ndio maana mtu atosemewa shtaka katika mahakama hiyo ya chini lakini ataambiwa asijibu chochote kwasababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza. Na kama kosa hilo halidhaminiki mtu huyo atarudishwa rumande. Ikumbukwe kuwa office ya DDP haifanyi upelelezi siyo kazi yake hiyo ni kazi ya Office ya DCI.
Pamoja sana
 
Kuna vitu watu wanashindwa kuelewa. Siyo kwamba DPP hajui kesi hiyo inaenda wapi ni anafahamu. Kuna baadhi ya makosa yanasikilizwa mahakama kuu. Ili ifike mahakama kuu lazima wafuate procedures kwanza kesi hizo zinafunguliwa mahakama ya chini yake. Mpaka pale upelelezi utakapo kamilika na mtu huyo amefanyiwa kitu kinaitwa "Commital", kesi hiyo ndipo itakapo hamishiwa mahakama kuu na kuanza kusikilizwa. Na ndio maana mtu atosemewa shtaka katika mahakama hiyo ya chini lakini ataambiwa asijibu chochote kwasababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza. Na kama kosa hilo halidhaminiki mtu huyo atarudishwa rumande. Ikumbukwe kuwa office ya DDP haifanyi upelelezi siyo kazi yake hiyo ni kazi ya Office ya DCI.
DCI alitakiwa chini ya WOO.Inakuwaje unaendesha mashitaka alhali haupelelezi??
 
Hizo ni mamlaka zilizowekwa kisheria. Sasa ukiniuliza ni kwanini unaendesha mashtaka ili hali haupelellezi kesi siwezi kukujibu labda uwaulize watunga sheria. Lakini kwa upeo wangu naweza kukujibu kwamba mamlaka hizi japo zinafanya kazi kwa ushirikiano zimetenganishwa ili kuwepo na haki dhidi ya mtuhumiwa na mlalamikaji. Ikumbukwe anayeendesha mashtaka ni mwanasheria(Wakili wa serikali) na anae peleleza ni polisi (mpelelezi). Na wakali anaweza kuondoa kesi mahakamani akiona swala zima la upelelezi na ushahidi haujakaa vizuri. Na ikiwezekana mtuhumiwa huyo anaweza asirudishwe tena mahakamani. Kwahiyo Wakili wa Serikali kupitia mamlaka aliyopewa na DPP anaweza kutoa haki kwa mtindo huo.
 
Jamani Petro E. Mselewa tunaomba msaada tutani tafadhali

Mkuu CHIKIRA MTABARI jambo hilo la kumfikisha Mshtakiwa kwenye mahakama isiyo na uwezo wa kusikiliza mashtaka yake linaruhusiwa kisheria na kimahakama. Utaratibu huo, katika lugha ya kisheria, huitwa committal proceedings au preliminary inquiry. Hapo, Mshtakiwa hufikishwa kwenye mahakama isiyo na uwezo wa kumsikiliza kwa lengo la kuiandaa kesi kwa kuipeleka mahakama mahususi na yenye uwezo wa kusikiliza kwa ajili ya kusikilizwa na kuamuliwa.

Mfano, makosa ya mauwaji, uhujumu uchumi, ugaidi na utakatishaji fedha ni makosa ambayo husikilizwa na Mahakama Kuu tu kwa mara ya kwanza (kabla ya rufaa kwenda Mahakama ya Rufani). Hatahivyo, washtakiwa waweza kupelekwa na kusomewa makosa yao Mahakama ya Hakimu Mkazi-kama Kinondoni, Ilala na Kisutu kwa ajili ya committal proceedings. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 246 cha Sheria ya Mwenendo wa makosa ya Jinai, Sura Na.20 ya Sheria za Tanzania.

Lengo la committal proceedings ni kukamilisha upelelezi wa kesi husika; kuandaa ushahidi wa nyaraka na watu pamoja na mambo mengineyo ya kisheria. Yote yanapokamilika, jalada la kesi husika hupelekwa Mahakama yenye uwezo wa kusikiliza kesi husika kwa ajili ya kusikilizwa na kuamuliwa. Kimsingi, pamoja na kuruhusiwa kisheria, committal proceedings ina changamoto zake. Mojawapo ni kutumika muda mrefu katika kupeleleza na kufanya mengineyo niliyoyataja.

Inasemwa kuwa, wakati mwingine, committal proceedings hufanywa kuwa njia ya kuwatesa washtakiwa kwa kuwaleta mahakamani na kuwarejesha rumande. Ingawa mahabusu hafanyi kazi kama alivyo mfungwa, ni vyema kukawa na uharaka wa kukamilisha committal proceedings ili kutenda haki kwa pande zote za shauri. Sheria inapaswa kutazama hasa upande dhaifu-upande wa Mshtakiwa.
 
Kuna vitu watu wanashindwa kuelewa. Siyo kwamba DPP hajui kesi hiyo inaenda wapi ni anafahamu. Kuna baadhi ya makosa yanasikilizwa mahakama kuu. Ili ifike mahakama kuu lazima wafuate procedures kwanza kesi hizo zinafunguliwa mahakama ya chini yake. Mpaka pale upelelezi utakapo kamilika na mtu huyo amefanyiwa kitu kinaitwa "Commital", kesi hiyo ndipo itakapo hamishiwa mahakama kuu na kuanza kusikilizwa. Na ndio maana mtu atosemewa shtaka katika mahakama hiyo ya chini lakini ataambiwa asijibu chochote kwasababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza. Na kama kosa hilo halidhaminiki mtu huyo atarudishwa rumande. Ikumbukwe kuwa office ya DDP haifanyi upelelezi siyo kazi yake hiyo ni kazi ya Office ya DCI.
Asante kwa shule nzuri
 
Mkuu CHIKIRA MTABARI jambo hilo la kumfikisha Mshtakiwa kwenye mahakama isiyo na uwezo wa kusikiliza mashtaka yake linaruhusiwa kisheria na kimahakama. Utaratibu huo, katika lugha ya kisheria, huitwa committal proceedings au preliminary inquiry. Hapo, Mshtakiwa hufikishwa kwenye mahakama isiyo na uwezo wa kumsikiliza kwa lengo la kuiandaa kesi kwa kuipeleka mahakama mahususi na yenye uwezo wa kusikiliza kwa ajili ya kusikilizwa na kuamuliwa.

Mfano, makosa ya mauwaji, uhujumu uchumi, ugaidi na utakatishaji fedha ni makosa ambayo husikilizwa na Mahakama Kuu tu kwa mara ya kwanza (kabla ya rufaa kwenda Mahakama ya Rufani). Hatahivyo, washtakiwa waweza kupelekwa na kusomewa makosa yao Mahakama ya Hakimu Mkazi-kama Kinondoni, Ilala na Kisutu kwa ajili ya committal proceedings. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 246 cha Sheria ya Mwenendo wa makosa ya Jinai, Sura Na.20 ya Sheria za Tanzania.

Lengo la committal proceedings ni kukamilisha upelelezi wa kesi husika; kuandaa ushahidi wa nyaraka na watu pamoja na mambo mengineyo ya kisheria. Yote yanapokamilika, jalada la kesi husika hupelekwa Mahakama yenye uwezo wa kusikiliza kesi husika kwa ajili ya kusikilizwa na kuamuliwa. Kimsingi, pamoja na kuruhusiwa kisheria, committal proceedings ina changamoto zake. Mojawapo ni kutumika muda mrefu katika kupeleleza na kufanya mengineyo niliyoyataja.

Inasemwa kuwa, wakati mwingine, committal proceedings hufanywa kuwa njia ya kuwatesa washtakiwa kwa kuwaleta mahakamani na kuwarejesha rumande. Ingawa mahabusu hafanyi kazi kama alivyo mfungwa, ni vyema kukawa na uharaka wa kukamilisha committal proceedings ili kutenda haki kwa pande zote za shauri. Sheria inapaswa kutazama hasa upande dhaifu-upande wa Mshtakiwa.
Ahsante sana usinichoke kukutagi mara kwa mara
 
Mimi binafsi ni mbumbumbu mzungu wa reli kwenye sheria. Napenda kujua, committal proceedings au preliminary proceedings zina umuhimu gani? Kwanini zifanyike mahakama ya chini? Ina maana yale yanayofanyika kwa Hakimu Mkazi hayawezi kufanyika Mahakama Kuu? Kama lengo ni kupata ushahidi, ina maana kesi ikifika mahakama kuu haiwezekani kuleta ushahidi 'mpya'?
 
  • Thanks
Reactions: cdc
...

Sent from my GT-I9300 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu CHIKIRA MTABARI jambo hilo la kumfikisha Mshtakiwa kwenye mahakama isiyo na uwezo wa kusikiliza mashtaka yake linaruhusiwa kisheria na kimahakama. Utaratibu huo, katika lugha ya kisheria, huitwa committal proceedings au preliminary inquiry. Hapo, Mshtakiwa hufikishwa kwenye mahakama isiyo na uwezo wa kumsikiliza kwa lengo la kuiandaa kesi kwa kuipeleka mahakama mahususi na yenye uwezo wa kusikiliza kwa ajili ya kusikilizwa na kuamuliwa.

Mfano, makosa ya mauwaji, uhujumu uchumi, ugaidi na utakatishaji fedha ni makosa ambayo husikilizwa na Mahakama Kuu tu kwa mara ya kwanza (kabla ya rufaa kwenda Mahakama ya Rufani). Hatahivyo, washtakiwa waweza kupelekwa na kusomewa makosa yao Mahakama ya Hakimu Mkazi-kama Kinondoni, Ilala na Kisutu kwa ajili ya committal proceedings. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 246 cha Sheria ya Mwenendo wa makosa ya Jinai, Sura Na.20 ya Sheria za Tanzania.

Lengo la committal proceedings ni kukamilisha upelelezi wa kesi husika; kuandaa ushahidi wa nyaraka na watu pamoja na mambo mengineyo ya kisheria. Yote yanapokamilika, jalada la kesi husika hupelekwa Mahakama yenye uwezo wa kusikiliza kesi husika kwa ajili ya kusikilizwa na kuamuliwa. Kimsingi, pamoja na kuruhusiwa kisheria, committal proceedings ina changamoto zake. Mojawapo ni kutumika muda mrefu katika kupeleleza na kufanya mengineyo niliyoyataja.

Inasemwa kuwa, wakati mwingine, committal proceedings hufanywa kuwa njia ya kuwatesa washtakiwa kwa kuwaleta mahakamani na kuwarejesha rumande. Ingawa mahabusu hafanyi kazi kama alivyo mfungwa, ni vyema kukawa na uharaka wa kukamilisha committal proceedings ili kutenda haki kwa pande zote za shauri. Sheria inapaswa kutazama hasa upande dhaifu-upande wa Mshtakiwa.
Pamoja sana Jembe, Ahsante kwa majibu yako..

Sent from my GT-I9300 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu CHIKIRA MTABARI jambo hilo la kumfikisha Mshtakiwa kwenye mahakama isiyo na uwezo wa kusikiliza mashtaka yake linaruhusiwa kisheria na kimahakama. Utaratibu huo, katika lugha ya kisheria, huitwa committal proceedings au preliminary inquiry. Hapo, Mshtakiwa hufikishwa kwenye mahakama isiyo na uwezo wa kumsikiliza kwa lengo la kuiandaa kesi kwa kuipeleka mahakama mahususi na yenye uwezo wa kusikiliza kwa ajili ya kusikilizwa na kuamuliwa.

Mfano, makosa ya mauwaji, uhujumu uchumi, ugaidi na utakatishaji fedha ni makosa ambayo husikilizwa na Mahakama Kuu tu kwa mara ya kwanza (kabla ya rufaa kwenda Mahakama ya Rufani). Hatahivyo, washtakiwa waweza kupelekwa na kusomewa makosa yao Mahakama ya Hakimu Mkazi-kama Kinondoni, Ilala na Kisutu kwa ajili ya committal proceedings. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 246 cha Sheria ya Mwenendo wa makosa ya Jinai, Sura Na.20 ya Sheria za Tanzania.

Lengo la committal proceedings ni kukamilisha upelelezi wa kesi husika; kuandaa ushahidi wa nyaraka na watu pamoja na mambo mengineyo ya kisheria. Yote yanapokamilika, jalada la kesi husika hupelekwa Mahakama yenye uwezo wa kusikiliza kesi husika kwa ajili ya kusikilizwa na kuamuliwa. Kimsingi, pamoja na kuruhusiwa kisheria, committal proceedings ina changamoto zake. Mojawapo ni kutumika muda mrefu katika kupeleleza na kufanya mengineyo niliyoyataja.

Inasemwa kuwa, wakati mwingine, committal proceedings hufanywa kuwa njia ya kuwatesa washtakiwa kwa kuwaleta mahakamani na kuwarejesha rumande. Ingawa mahabusu hafanyi kazi kama alivyo mfungwa, ni vyema kukawa na uharaka wa kukamilisha committal proceedings ili kutenda haki kwa pande zote za shauri. Sheria inapaswa kutazama hasa upande dhaifu-upande wa Mshtakiwa.
pmja na hayo tisaidie na swali la huyu dafa sooth pia.... Napenda kujua, committal proceedings au preliminary proceedings zina umuhimu gani? Kwanini zifanyike mahakama ya chini? Ina maana yale yanayofanyika kwa Hakimu Mkazi hayawezi kufanyika Mahakama Kuu? Kama lengo ni kupata ushahidi, ina maana kesi ikifika mahakama kuu haiwezekani kuleta ushahidi 'mpya'?

Sent from my GT-I9300 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom