Kuwashwa sana kwenye nyayo za miguu au viganja vya mikono husababishwa na nini?

Kuwashwa sana kwenye nyayo za miguu au viganja vya mikono husababishwa na nini?

Mabobish

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2018
Posts
367
Reaction score
282
Mwenzenu kwa muda mrefu sasa nimekuwa na tatizo la kuwashwa sana kwenye unyayo wa miguu tena kwa kubadilika badilika miguu.

Aidha wakati mwingine nimekuwa na tatizo la kuwashwa sana kwenye kiganja cha mkononi hususani kwenye dole gumba au vidole vingine kimojawapo.

Tendo hili limekuwa likinitokea mara kwa mara katika wiki wakati mwingine huweza kunitokea mara tatu au nne kwa wiki, kibaya zaidi hutokea muda wowote si usiku si mchana, kwa wakati wa usiku naweza kuwa katikati ya usingizi mzito lakini mara tu hali ya kuwashwa inapotokea basi lazima niamke kwa kustuka usingizini.

Kinachofuata ni kujikuna kwa muda mrefu takribani dk 20 mpaka 30 tena kwa ama kutumia brush ngumu au jiwe la kuogea ndipo muwasho unaisha. Katika kujikuna sometimes mpaka eneo ninalojikuna linachubuka ndo inakuwa kupata ahueni kwangu.

Wadau naomba mwenye kufahamu hali hii inasabishwa na nini na tiba yake ni nini mnisaidie maana kibaya zaidi muwasho mkali hutokea wakati wowote hata kama nilikuwa naendesha gari basi hulazimika kupark gari, kuvua Kiatu in case imetokea unyayoni kisha kujikuna mpaka hali itulie.
 
Utapata safari ya mbali na pia tarajia kupata pesa nyingi hivi karibuni
 
unyayo ukiwasha ni safari au mwendo mkono ukiwasha dalili ya kupata pesa
 
Nenda hospital mkuu utajua tatizo zaidi. Huu ni ushauri muhimu

Au nenda duka la madawa nunua dawa za fangazi hasa moja ipo box la kijani(jina nimesahau) pakiwasha tu pakaa eneo husika
 
Inafurahisha hahahaa,

Inawezekanaje eti kiganja kiwashe kua ni dalili ya kupata pesa au utajiri wakati huna chanzo chochote Cha kuweza kua sababu ya kua tajiri.

Utajiri wala pesa hauji kwa kuwashwa kiganja. Juhudi binafsi inahitajika ndio kufikia hayo.

Weee endelea kuwaskiliza hao uendelee kukuna kiganja chako ukiusubiri utajiri.

Mitano tena!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nenda hospital mkuu utajua tatizo zaidi. Huu ni ushauri muhimu

Au nenda duka la madawa nunua dawa za fangazi hasa moja ipo box la kijani(jina nimesahau) pakiwasha tu pakaa eneo huika
Angalau wewe umeweza kunipatia ushauri wa kujengana kuliko wengine hawako serious wanashauri famba tu
 
Hao hawajui mateso unayoyapata mkuu. Pitia na hapa unaweza pata mwanga zaidi

Angalau wewe umeweza kunipatia ushauri wa kujengana kuliko wengine hawako serious wanashauri famba tu
 
Inafurahisha hahahaa,

Inawezekanaje eti kiganja kiwashe kua ni dalili ya kupata pesa au utajiri wakati huna chanzo chochote Cha kuweza kua sababu ya kua tajiri.

Utajiri wala pesa hauji kwa kuwashwa kiganja. Juhudi binafsi inahitajika ndio kufikia hayo.

Weee endelea kuwaskiliza hao uendelee kukuna kiganja chako ukiusubiri utajiri.

Mitano tena!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Ww umejuaje hana chanzo Cha kumuingizia pesa
 
Kapime mapema hiyo ni dalili ya ugonjwa,ikiwa ni bahati basi huwezi kuwashwa mpaka ukaamka kutoka usingizini,
 
Back
Top Bottom