muthe_x
Member
- Sep 25, 2013
- 10
- 56
Nini chanzo cha kuyeyuka kwa barafu katika maeneo ya arctict na antarcticta? Nadhani jibu litakua rahisi sana kama ku muuliza motto wa darasa la tano. Nalo ni kuongezeka kwa joto duniani linalosababishwa na shughuli mbalili mbali za binadamu. Hili ndilo wengi wetu tumekua tukisikia katika vyombo mbali mbali na hata kufundishwa darasani. Lakini nimekuna na taarifa iliyo nipa changamoto sana na kuona kabisa ya kwamba niliyoyajua mwanzo wenda nilivyojua mwanzo siku sahihi. Tujiulize, ukiangalia ripoti nyingi na taarifa zinaonesha kuongezeka kwa joto dunianiani ndio chanzo cha hiyo barafu kuyeyuka lakini tuungalie joto la maeneo haya Arctic ni kwa wastani wa karibu -17 [17 below freezing]na Antarctica ambalo hili ni bara lenye barafu yenye kina cha karibu 1mile, ni karibu -30 [30 below freezing].sasa inakua vipi ongezeko la joto na hapa tunazungua air temperature iweze kusababisha barafu ya huko kuweza kuyeyuka? We unadhani chanzo ni nini? au ukweli ni upi?