Pre GE2025 CHADEMA yadai kuzuiwa kufanya Mkutano katika kumbi za Hoteli ya Sea Cliff, uliopangwa kufanyika leo, Februari 27, 2025 Dar

Pre GE2025 CHADEMA yadai kuzuiwa kufanya Mkutano katika kumbi za Hoteli ya Sea Cliff, uliopangwa kufanyika leo, Februari 27, 2025 Dar

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema, amedai kuwa chama hicho kimezuiwa kufanya mkutano wake uliopangwa kufanyika leo, Februari 27, 2025, katika hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam.

Kupitia ujumbe wake kwenye mtandao wa X, Lema amesema walipata taarifa kuwa ukumbi waliokuwa wameukodi hauwezi kutumika kwa sababu ya hitilafu ya umeme na AC. Baada ya kuelekezwa kwenye hoteli ya Coral Beach kama mbadala, nao walizuiwa baadaye na menejimenti ya hoteli hiyo.

1740658470263.png
Lema ameitaja hali hiyo kuwa ni aina ya ubaguzi, lakini ameahidi kuwa CHADEMA haitakata tamaa. Mkutano huo sasa utafanyika katika Makao Makuu ya chama kuanzia saa 12:00 jioni leo.

Soma, Pia: Godbless Lema watangaza kufanya tukio kubwa Tarehe 27 Februari, 2025 ikiwemo kuzindua kampeni ya kidigitiali

Andiko la Lema kutoka X (zamani twitter);

"Tulikuwa Tumefanya Booking ya Ukumbi kwa ajili ya shughuli yetu leo 27/2/2025 ktk hotel ya Sea Clif Hotel. Asubuhi nilipigiwa simu nikaambiwa kuna dharura kuwa AC zimeharibika na umeme umekoroga hapa ukumbini na kwa hiyo hatuwezi kufanya mkutano wetu, Sea Cliff wakatutafutia ukumbi mbadala ktk hotel ya Coral beach."

"Tulienda Coral beach hotel na kukubaliana tutafanyia hapo na maandalizi yalianza. Baada ya masaa mawili nikipapigiwa simu kutoka kCoral beach kwamba wamepokea meseji kutoka menejimenti ya juu kuwa CHADEMA hawaruhusiwi kufanya mkutano hapo.

"Hii mbegu ya ubaguzi waliyopanda wataijutia sana. Hata hivyo hatuwezi kukata tamaa hivyo basi tumeamua kuwa tutaendelea na tukio letu kama lilivyopangwa ktk ukumbi wetu Makao Makuu ya Chama kuanzia saa 12:00 Jioni. Wanachama wote na waalikwa karibuni.
Defeat is not an option."

GkyqmrzWgAARZx1.jpg
 
Huu ni uonevu wa wazi kabisa unaofanywa na watu wanaojitapa na kuwadanganya Watanzania kuwa mwaka jana wamerekebisha Sheria za Uchaguzi na Demokrasia.

Huu ni uthibitisho kuwa Tanzania hakuna demokrasia na siasa zinafanywa kuwapendelea CCM tu.

Huu ni uthibitisho kuwa CCM wanafanya uonevu wa wazi hivyo mwaka huu vyovyote vile tuwaombe wenye akili na wanaoguswa na haya kwenye vyombo vya ulinzi wa Usalama watusaidie kweli kuwaambia CCM kuwa There Should be No Election this Year Without Reforms.
Screenshot_20250227_145815_Gallery.jpg
 
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema, amedai kuwa chama hicho kimezuiwa kufanya mkutano wake uliopangwa kufanyika leo, Februari 27, 2025, katika hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam.

Kupitia ujumbe wake kwenye mtandao wa X, Lema amesema walipata taarifa kuwa ukumbi waliokuwa wameukodi hauwezi kutumika kwa sababu ya hitilafu ya umeme na AC. Baada ya kuelekezwa kwenye hoteli ya Coral Beach kama mbadala, nao walizuiwa baadaye na menejimenti ya hoteli hiyo.

Lema ameitaja hali hiyo kuwa ni aina ya ubaguzi, lakini ameahidi kuwa CHADEMA haitakata tamaa. Mkutano huo sasa utafanyika katika Makao Makuu ya chama kuanzia saa 12:00 jioni leo.

ikiwa kulikua na dhamira ovu, hilo ni jambo sahihi la kheri 🐒
 
Naunga mkono mia kwa mia hiyo Hotel kukataa wasifanye mkutano

Haiwezekani Lisu anasema Chama hakina fedha watu wachangie halafu wanaenda kufanya mikutano hoteli za kitalii za mamilioni

Wafanyie ofisini kwao makao makuu ya Chadema

Mahoteli mengine igeni huo mfano mtasaidia pesa za Chadema na wafadhili kununusurika

Hii mifisadi team Lisu wanasafisha pesa zote akaunti za Chadema

Lisu nakuuliza tena Chadema ina hela su haina hela? Asiye na hela aweza kwenda kufanya mkutano hotel kubwa ya kitalii ya sea Cliff

Wanachadema amkeni
 
Huu ni uonevu wa wazi kabisa unaofanywa na watu wanaojitapa na kuwadanganya Watanzania kuwa mwaka jana wamerekebisha Sheria za Uchaguzi na Demokrasia.

Huu ni uthibitisho kuwa Tanzania hakuna demokrasia na siasa zinafanywa kuwapendelea CCM tu.

Huu ni uthibitisho kuwa CCM wanafanya uonevu wa wazi hivyo mwaka huu vyovyote vile tuwaombe wenye akili na wanaoguswa na haya kwenye vyombo vya ulinzi wa Usalama watusaidie kweli kuwaambia CCM kuwa There Should be No Election this Year Without Reforms.
View attachment 3251842

View: https://x.com/Getrude_mollel/status/1895078638900416936?t=idyz5cRv5PnetLfymqfuqg&s=19
 
Naunga mkono mia kwa mia hiyo Hotel kukataa wasifanye mkutano

Haiwezekani Lisu anasema Chama hakina fedha watu wachangie halafu wanaenda kufanya mikutano hoteli za kitalii za mamilioni

Wafanyie ofisini kwao makao makuu ya Chadema

Mahoteli mengine igeni huo mfano mtasaidia pesa za Chadema na wafadhili kununusurika

Hii mifisadi team Lisu wanasafisha pesa zote akaunti za Chadema

Lisu nakuuliza tena Chadema ina hela su haina hela? Asiye na hela aweza kwenda kufanya mkutano hotel kubwa ya kitalii ya sea Cliff

Wanachadema amkeni
Unateseka ukiwa upande upi?
 
Back
Top Bottom