Kwa hali ilivyotokea kwa Tundu Lissu Mbeya kweli kulikuwa na mpango kuhamia CCM hivi karibuni kama Msigwa alivyokuwa anatuambia?

Kwa hali ilivyotokea kwa Tundu Lissu Mbeya kweli kulikuwa na mpango kuhamia CCM hivi karibuni kama Msigwa alivyokuwa anatuambia?

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288
Siasa tofauti na dini. Dini hata uteswe vipi, uhadiwe mabilioni ya shilingi hutakiwi ubadilike

Nitaoa mifano yaliowakuta watu enzi za tawala za nyuma kabisa
kwa mfano

1.Bilal ibn Rabah (RA): Alikuwa mtumwa wa kipagani wa Kikuraishi, Umayya ibn Khalaf. Alipokea mateso makubwa, ikiwemo kuwekwa kwenye mchanga moto huku akiwa amefungwa mawe makubwa juu yake. Aliteswa ili aachane na Uislamu, lakini aliendelea kusema "Ahad, Ahad" (Mmoja, Mmoja), akimaanisha Mungu ni mmoja.

2.Ammar ibn Yasir (RA), mama yake Sumayyah (RA), na baba yake Yasir (RA): Familia hii iliteswa vibaya sana. Sumayyah, mama wa Ammar, alikuwa mwanamke wa kwanza kuuawa kwa ajili ya Uislamu baada ya kuteswa hadi kufa. Yasir, baba yake Ammar, pia aliuawa kutokana na mateso. Ammar alilazimishwa kusema maneno ya ukafiri kwa ajili ya mateso makubwa aliyokuwa akipata, lakini Mtume (SAW) alimfariji na kumwambia kuwa imani yake ilikuwa bado thabiti moyoni mwake.

3. Khabbab ibn al-Aratt (RA): Aliteswa na Wakuraishi kwa kuchomwa moto mgongoni mwake, lakini alibaki thabiti katika imani yake.

4.Suhaib ibn Sinan al-Rumi (RA): Suhaib alikuwa Mroma ambaye alihamia Makka na kuingia Uislamu. Wakuraishi walimtesa na kumzuilia mali zake kwa sababu ya Uislamu wake. Alikimbia kwenda Madina kuungana na Mtume Muhammad (SAW) na Waislamu wengine, lakini aliwapa Wakuraishi mali zake zote ili wamruhusu kuondoka. Mtume (SAW) alimpongeza kwa kusema kuwa alikuwa amefanya biashara yenye faida kwa kuuza mali yake kwa ajili ya imani yake.

Soma Pia: Lissu, Mnyika na Sugu wakamatwa na Polisi usiku huu. Baadhi ya Waandishi wa habari pia wakamatwa

5. Zunairah al-Rumiya (RA)
: Alikuwa mtumwa ambaye alisilimu na kufuatia kuingia kwake katika Uislamu, aliteswa sana na bwana wake. Watu walimtesa hadi akapoteza uwezo wake wa kuona. Wakati huo, Wakuraishi walimdhihaki na kumwambia kuwa miungu yao ndio iliyomfanya kipofu, lakini alisisitiza kuwa Allah ndiye atakayerudisha uwezo wake wa kuona. Kwa neema ya Mwenyezi Mungu, macho yake yalipona, jambo lililowashangaza watesaji wake.

6.Abu Fukayha (RA): Alikuwa mtumwa wa Kipagani wa Kikuraishi na aliteswa vikali kwa sababu ya kuingia kwake Uislamu. Aliburutwa kwa kamba kwenye barabara zenye joto kali, na mateso mengine mengi. Hata hivyo, alikataa kurudi kwenye ukafiri na alibaki thabiti katika imani yake.

7.Lubaynah (RA): Lubaynah alikuwa mtumwa aliyeingia Uislamu na kufuatia hilo, bwana wake aliamua kumtesa vikali kwa matumaini kwamba atakataa Uislamu, lakini alibaki imara. Hata alipoteswa, Lubaynah hakujihusisha na ukafiri.

8.Ummi Ubays (RA): Alikuwa miongoni mwa wanawake walioteswa kwa sababu ya imani yao. Alijitolea kwa Uislamu na hakuwahi kurudi nyuma licha ya vitisho na mateso.
Licha ya mateso haya na majaribu ya kuahidiwa vyeo, mali, au heshima, Maswahaba hawa na wengine wengi walibaki waaminifu kwa Uislamu na hawakurudi kwenye ukafiri. Imani yao iliwafanya waepuke majaribu yote ya dunia na kuendelea kushikilia imani yao kwa Mungu mmoja.

Swali la msingi

Je, kwa msimamo alionesha lissu mbeya ni kweli kulikuwa na mpango wa kuhamia ccm hivi karibuni?
 
Siasa tofauti na dini. Dini hata uteswe vipi, uhadiwe mabilioni ya shilingi hutakiwi ubadilike

Nitaoa mifano yaliowakuta watu enzi za tawala za nyuma kabisa
kwa mfano

  1. Bilal ibn Rabah (RA): Alikuwa mtumwa wa kipagani wa Kikuraishi, Umayya ibn Khalaf. Alipokea mateso makubwa, ikiwemo kuwekwa kwenye mchanga moto huku akiwa amefungwa mawe makubwa juu yake. Aliteswa ili aachane na Uislamu, lakini aliendelea kusema "Ahad, Ahad" (Mmoja, Mmoja), akimaanisha Mungu ni mmoja.
  2. Ammar ibn Yasir (RA), mama yake Sumayyah (RA), na baba yake Yasir (RA): Familia hii iliteswa vibaya sana. Sumayyah, mama wa Ammar, alikuwa mwanamke wa kwanza kuuawa kwa ajili ya Uislamu baada ya kuteswa hadi kufa. Yasir, baba yake Ammar, pia aliuawa kutokana na mateso. Ammar alilazimishwa kusema maneno ya ukafiri kwa ajili ya mateso makubwa aliyokuwa akipata, lakini Mtume (SAW) alimfariji na kumwambia kuwa imani yake ilikuwa bado thabiti moyoni mwake.
  3. Khabbab ibn al-Aratt (RA): Aliteswa na Wakuraishi kwa kuchomwa moto mgongoni mwake, lakini alibaki thabiti katika imani yake.

  • Suhaib ibn Sinan al-Rumi (RA): Suhaib alikuwa Mroma ambaye alihamia Makka na kuingia Uislamu. Wakuraishi walimtesa na kumzuilia mali zake kwa sababu ya Uislamu wake. Alikimbia kwenda Madina kuungana na Mtume Muhammad (SAW) na Waislamu wengine, lakini aliwapa Wakuraishi mali zake zote ili wamruhusu kuondoka. Mtume (SAW) alimpongeza kwa kusema kuwa alikuwa amefanya biashara yenye faida kwa kuuza mali yake kwa ajili ya imani yake.
  • Zunairah al-Rumiya (RA): Alikuwa mtumwa ambaye alisilimu na kufuatia kuingia kwake katika Uislamu, aliteswa sana na bwana wake. Watu walimtesa hadi akapoteza uwezo wake wa kuona. Wakati huo, Wakuraishi walimdhihaki na kumwambia kuwa miungu yao ndio iliyomfanya kipofu, lakini alisisitiza kuwa Allah ndiye atakayerudisha uwezo wake wa kuona. Kwa neema ya Mwenyezi Mungu, macho yake yalipona, jambo lililowashangaza watesaji wake.
  • Abu Fukayha (RA): Alikuwa mtumwa wa Kipagani wa Kikuraishi na aliteswa vikali kwa sababu ya kuingia kwake Uislamu. Aliburutwa kwa kamba kwenye barabara zenye joto kali, na mateso mengine mengi. Hata hivyo, alikataa kurudi kwenye ukafiri na alibaki thabiti katika imani yake.
  • Lubaynah (RA): Lubaynah alikuwa mtumwa aliyeingia Uislamu na kufuatia hilo, bwana wake aliamua kumtesa vikali kwa matumaini kwamba atakataa Uislamu, lakini alibaki imara. Hata alipoteswa, Lubaynah hakujihusisha na ukafiri.
  • Ummi Ubays (RA): Alikuwa miongoni mwa wanawake walioteswa kwa sababu ya imani yao. Alijitolea kwa Uislamu na hakuwahi kurudi nyuma licha ya vitisho na mateso.
Licha ya mateso haya na majaribu ya kuahidiwa vyeo, mali, au heshima, maswahaba hawa na wengine wengi walibaki waaminifu kwa Uislamu na hawakurudi kwenye ukafiri. Imani yao iliwafanya waepuke majaribu yote ya dunia na kuendelea kushikilia imani yao kwa Mungu mmoja.

SWALI LA MSINGI

JEE KWA MSIMAMO ALIONESHA LISSU MBEYA NI KWELI KULIKUWA NA MPANGO WA KUHAMIA CCM HIVI KARIBUNI?
Inahitaji akili ya mwendawazimu kumuamini Msigwa mtu ambaye miezi miwili iliyopita alikuwa anaitukana CCM kuwa ni chama cha wahuni kinachoongozwa na watu wenye akili ndogo leo hii anatokwa na povu kuisifia CCM. Huyu ni mchumia tumbo tu . APUUZWE TU.
 
Mleta.mada umenifanya nijihisi Niko makaburini yaani umejaza taarifa za ndani za marehemu kibao unatoka kuelezea marehemu huyu unakuja kuelezea marehemu mwingine

Wewe mwanga Nini?
Umesoma shule za kata au internationa school?
 
Mleta.mada umenifanya nijihisi Niko makaburini yaani umejaza taarifa za ndani za marehemu kibao unatoka kuelezea marehemu huyu unakuja kuelezea marehemu mwingine
Umebobea kwenye habari za marehemu

Wewe mwanga Nini?
Historia
 
Inahitaji akili ya mwendawazimu kumuamini Msigwa mtu ambaye miezi miwili iliyopita alikuwa anaitukana CCM kuwa ni chama cha wahuni kinachoongozwa na watu wenye akili ndogo leo hii anatokwa na povu kuisifia CCM. Huyu ni mchumia tumbo tu . APUUZWE TU.
Ningekuwa kwenye nafasi ya Msigwa hata ingetokea nimevuta hela ya watu, basi ningechagua kwamba hayo malipo yawe kwa ajili ya kuachana kabisa na siasa badala ya kuhama Chama.
Kipindi cha mwendazake kuna jamaa wa CHADEMA alikuwa maarufu sana Iringa na alikuwa yupo vizuri kwa kujenga hoja. Wakamtaka ahamie CCM akagoma, wakajaribu kumpa hela akagoma, walichofa walimvamia akiwa barabarani anaendesha gari wakamteka na kumpawiti na kumlazimisha ahamie CCM, yule jamaa aligoma akaamua kuklachana na siasa lakini si kuhamia CCM, akawaambia kama ni picha moazisambaze tu.
Hayo yanayomtokea Msigwa hamuwezi kujua anapambana na anakubali kuropika kila anachoandikiwa huenda kuna aibu anaificha
 
Inahitaji akili ya mwendawazimu kumuamini Msigwa mtu ambaye miezi miwili iliyopita alikuwa anaitukana CCM kuwa ni chama cha wahuni kinachoongozwa na watu wenye akili ndogo leo hii anatokwa na povu kuisifia CCM. Huyu ni mchumia tumbo tu . APUUZWE TU.
Na hili ni angalizo sio kwa Msigwa tu, bali kwa wanasiasa wooote. Haijalishi ni nani na yuko chama gani? Ni waongo sana ,you shouldnt rely on them or believe any single word out their mouths
 
Ningekuwa kwenye nafasi ya Msigwa hata ingetokea nimevuta hela ya watu, basi ningechagua kwamba hayo malipo yawe kwa ajili ya kuachana kabisa na siasa badala ya kuhama Chama.
Kipindi cha mwendazake kuna jamaa wa CHADEMA alikuwa maarufu sana Iringa na alikuwa yupo vizuri kwa kujenga hoja. Wakamtaka ahamie CCM akagoma, wakajaribu kumpa hela akagoma, walichofa walimvamia akiwa barabarani anaendesha gari wakamteka na kumpawiti na kumlazimisha ahamie CCM, yule jamaa aligoma akaamua kuklachana na siasa lakini si kuhamia CCM, akawaambia kama ni picha moazisambaze tu.
Hayo yanayomtokea Msigwa hamuwezi kujua anapambana na anakubali kuropika kila anachoandikiwa huenda kuna aibu anaificha
Ila kweli siri ya mtungi aijuae kata
 
Ningekuwa kwenye nafasi ya Msigwa hata ingetokea nimevuta hela ya watu, basi ningechagua kwamba hayo malipo yawe kwa ajili ya kuachana kabisa na siasa badala ya kuhama Chama.
Kipindi cha mwendazake kuna jamaa wa CHADEMA alikuwa maarufu sana Iringa na alikuwa yupo vizuri kwa kujenga hoja. Wakamtaka ahamie CCM akagoma, wakajaribu kumpa hela akagoma, walichofa walimvamia akiwa barabarani anaendesha gari wakamteka na kumpawiti na kumlazimisha ahamie CCM, yule jamaa aligoma akaamua kuklachana na siasa lakini si kuhamia CCM, akawaambia kama ni picha moazisambaze tu.
Hayo yanayomtokea Msigwa hamuwezi kujua anapambana na anakubali kuropika kila anachoandikiwa huenda kuna aibu anaificha
Naanza kupata picha kwa nini Msigwa amekuwa na mambo ya kike kike siku hizi kumbe tayari ameshamwagiwa kile kiwatilifu cha kibailojia ndiyo maana amekuwa hivyo duu, hawa watu wabaya sana ukute wengine anakutana nao wote wamevalia mboga mboga lakini ni waume zake. Hatari sana.
 
Ila kweli siri ya mtungi aijuae kata
Kumbe tusimlaumu sana tumpe pole, mtu ametunza rinda lake toka utotoni linakuja fumuliwa uzeeni tena na watu unaolazimishwa wawe rafiki zako huu ni unyama sana, kila nikiangalia ile picha amebebeshwa sanamu la mwenyekiti ukiangalia sura yake imeficha majuto mengi sana. Pole zake sana.
 
Siasa tofauti na dini. Dini hata uteswe vipi, uhadiwe mabilioni ya shilingi hutakiwi ubadilike

Nitaoa mifano yaliowakuta watu enzi za tawala za nyuma kabisa
kwa mfano

1.Bilal ibn Rabah (RA): Alikuwa mtumwa wa kipagani wa Kikuraishi, Umayya ibn Khalaf. Alipokea mateso makubwa, ikiwemo kuwekwa kwenye mchanga moto huku akiwa amefungwa mawe makubwa juu yake. Aliteswa ili aachane na Uislamu, lakini aliendelea kusema "Ahad, Ahad" (Mmoja, Mmoja), akimaanisha Mungu ni mmoja.

2.Ammar ibn Yasir (RA), mama yake Sumayyah (RA), na baba yake Yasir (RA): Familia hii iliteswa vibaya sana. Sumayyah, mama wa Ammar, alikuwa mwanamke wa kwanza kuuawa kwa ajili ya Uislamu baada ya kuteswa hadi kufa. Yasir, baba yake Ammar, pia aliuawa kutokana na mateso. Ammar alilazimishwa kusema maneno ya ukafiri kwa ajili ya mateso makubwa aliyokuwa akipata, lakini Mtume (SAW) alimfariji na kumwambia kuwa imani yake ilikuwa bado thabiti moyoni mwake.

3. Khabbab ibn al-Aratt (RA): Aliteswa na Wakuraishi kwa kuchomwa moto mgongoni mwake, lakini alibaki thabiti katika imani yake.

4.Suhaib ibn Sinan al-Rumi (RA): Suhaib alikuwa Mroma ambaye alihamia Makka na kuingia Uislamu. Wakuraishi walimtesa na kumzuilia mali zake kwa sababu ya Uislamu wake. Alikimbia kwenda Madina kuungana na Mtume Muhammad (SAW) na Waislamu wengine, lakini aliwapa Wakuraishi mali zake zote ili wamruhusu kuondoka. Mtume (SAW) alimpongeza kwa kusema kuwa alikuwa amefanya biashara yenye faida kwa kuuza mali yake kwa ajili ya imani yake.

Soma Pia: Lissu, Mnyika na Sugu wakamatwa na Polisi usiku huu. Baadhi ya Waandishi wa habari pia wakamatwa

5. Zunairah al-Rumiya (RA)
: Alikuwa mtumwa ambaye alisilimu na kufuatia kuingia kwake katika Uislamu, aliteswa sana na bwana wake. Watu walimtesa hadi akapoteza uwezo wake wa kuona. Wakati huo, Wakuraishi walimdhihaki na kumwambia kuwa miungu yao ndio iliyomfanya kipofu, lakini alisisitiza kuwa Allah ndiye atakayerudisha uwezo wake wa kuona. Kwa neema ya Mwenyezi Mungu, macho yake yalipona, jambo lililowashangaza watesaji wake.

6.Abu Fukayha (RA): Alikuwa mtumwa wa Kipagani wa Kikuraishi na aliteswa vikali kwa sababu ya kuingia kwake Uislamu. Aliburutwa kwa kamba kwenye barabara zenye joto kali, na mateso mengine mengi. Hata hivyo, alikataa kurudi kwenye ukafiri na alibaki thabiti katika imani yake.

7.Lubaynah (RA): Lubaynah alikuwa mtumwa aliyeingia Uislamu na kufuatia hilo, bwana wake aliamua kumtesa vikali kwa matumaini kwamba atakataa Uislamu, lakini alibaki imara. Hata alipoteswa, Lubaynah hakujihusisha na ukafiri.

8.Ummi Ubays (RA): Alikuwa miongoni mwa wanawake walioteswa kwa sababu ya imani yao. Alijitolea kwa Uislamu na hakuwahi kurudi nyuma licha ya vitisho na mateso.
Licha ya mateso haya na majaribu ya kuahidiwa vyeo, mali, au heshima, Maswahaba hawa na wengine wengi walibaki waaminifu kwa Uislamu na hawakurudi kwenye ukafiri. Imani yao iliwafanya waepuke majaribu yote ya dunia na kuendelea kushikilia imani yao kwa Mungu mmoja.

Swali la msingi

Je, kwa msimamo alionesha lissu mbeya ni kweli kulikuwa na mpango wa kuhamia ccm hivi karibuni?
Huyo mkuu, nadhani ilikuwa kabla au baada ya uchaguzi aliposhindwa, kulikuwa na clip X na kwenye hiyo clip alisikika akisema, akihama Chadema wananchi wachome moto nyumba yake na mali yake. Haujapita muda, akawa amehama. Sasa ni lini alikuwa anasema ukweli, wakati anasema hayo maneno au sasa baada ya kuhama?
 
Kumuamini msigwa ni sawa na unamuona mwendawazimu mtaani halafu anakuambia kuna mtaa mabomba yanatoa maziwa na wewe ukaamini
 
..Nadhani malezi ya kisiasa kwa Watanzania yana matatizo.

..Uelewa wetu kuhusu siasa na demokrasia uko tofauti sana na wenzetu.

..Hali hiyo inatokana urithi na utamaduni wa siasa za KUCHARURANA toka mfumo wa chama kimoja na CCM.

..Kwa miaka mingi sana tangu CCM wakiwa peke yao Watanzania hatukujengewa utamaduni wa kufanya siasa za HOJA.

..Mambo mengi yalikuwa yanaamuliwa kwa kufuata mkumbo wa kumuunga mkono Mwenyekiti wa CCM, na yeyote mwenye mtizamo tofauti aliitwa majina mabaya, alizomewa, alicharurwa.

..Masuala mazito ya kisiasa, kijamii, na kiuchumi, yanajadiliwa utadhani ni mjadala wa Simba dhidi ya Yanga. Watanzania hatuna muda na utulivu wa kusikiliza hoja na kuzichambua. Tunapenda kusikia VIJEMBE.

..Mch.Peter Msigwa, ni zao la mazingira na mfumo huo wa kisiasa na kidemokrasia.
 
Back
Top Bottom