Kwa haya ya Makamba na Bashe, hakika serikali imebadilika

Kwa haya ya Makamba na Bashe, hakika serikali imebadilika

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
"TUJIKUMBUSHE KIDOGO"

Mwanzoni mwa mwaka huu, mwezi Januari, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe aliagiza mtuhumiwa aliyekuwa amekamatwa kwa kosa la kuendesha kiwanda bubu cha kutengeneza mafuta ya Mawese katika Kijiji cha Kongowe-Kibaha, Halifa Said atafutwe na asaidiwe na Shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO). Awali Halifa alikamatwa na Polisi kwa tuhuma za kuendesha kiwanda Bubu lakini Waziri Bashe alisema Serikali ya Rais Samia inapaswa kuwezesha wananchi na sio kuwa Serikali ya kamatakamata na fungiafungia

Siku chache zilizopita akiwa Kijiji cha Ugaka, Waziri wa Nishati, January Makamba akizungumza katika mkutano wa hadhara alizungumza na mwananchi Shaban Ali ambaye kwa sasa anafanya biashara ya mafuta kwa njia ya chupa na madumu kwenye Kijiji hicho ambapo alisema Serikali itamkopesha Shilingi Milioni 50 kutoka katika Shilingi Bilioni 2 ambazo zimetengwa na Wizara kama sehemu ya majaribio kwa mwaka huu wa fedha kuwawezesha Wajasiriamali kufungua vituo vidogo vya mafuta vijijini ili kuuza mafuta safi, kwa njia salama na kwa bei elekezi.

Kwa mara nyingine tena, ingekuwa ni Serikali ile iliyopita huyu kijana angekuwa anapumulia nyuma ya nondo kwani badala ya kumuwezesha angeanza kuulizwa leseni ya biashara, cheti cha TBS, NEMC wangekuja kudai EIA na mambo mengine kibao ya kukwamisha biashara.

Bashe na January ni mfano tu wa yale anayoyahubiri Rais Samia Suluhu Hassan lakini hii haipaswi kuishia kwa mtu mmojammoja bali mifumo imara na thabiti inapaswa kuwekwa ili haya wanayoyafanya yawe endelevu hata pale watakapoondoka katika nafasi walizopo hivi sasa.

Ila yote kwa yote nyakati zimebadilika sana.

Screenshot 2022-07-27 at 20.29.25.png
Screenshot 2022-07-27 at 20.29.35.png
 
Cheap politics. Watu wanataka umeme wa uhakika na kwa bei nafuu, Propaganda za kusema vijana wamekopeshwa ili wafunguwe vituo vya mafuta vjijini ni kudharau Watanzania maana hao vijana ni wanatumika kuficha upigaji. Hizo bilioni 2 zitaliwa kama njugu na hakuna la maana mtakaloona. Makamba kaachiwa vijiji 2000 ambavyo bado havijapata umeme, leo anaweza kusema amefikisha vijijini vingapi?
 
Unataka kujua namna wamachinga walisaidiwa awamu ya Tano?

Au unazani hao unao waongelea sio wamachinga.
 
Cheap politics. Watu wanataka umeme wa uhakika na kwa bei nafuu, Propaganda za kusema vijana wamekopeshwa ili wafunguwe vituo vya mafuta vjijini ni kudharau Watanzania maana hao vijana ni wanatumika kuficha upigaji. Hizo bilioni 2 zitaliwa kama njugu na hakuna la maana mtakaloona. Makamba kaachiwa vijiji 2000 ambavyo bado havijapata umeme, leo anaweza kusema amefikisha vijijini vingapi?
Sasa kama fungu lilitengwa na bajeti na limeanza kutumiwa kwa kazi husika, hapo cheap politics inatoka wapi, kama wataka mjadala wa vijiji viliyobaki ni mjadala unaojitosheleza kabisa lakini kujibu hoja X kwa majibu ya hoja Y nadhani sio sahihi
 
Stori yako kidogo (hapana, kikubwa), inatatiza.

Kwanza ni kama unapiga kampeni. Uchaguzi bado, ni kule 2025.

Lakini la muhimu zaidi, stori yako ni kama inashangilian watu kufanya shughuli zao nje ya taratibu?

Huyo mwenyekiwanda cha mafuta ya kula, mafuta hayo ni salama na ni ya kiwango?
Hapana, sijasema kumtia hatihati na kumweka ndani ilikuwa njiia sahihi. Kitu ninachokubali ni njia walizotumia hao mawaziri kusaidia hao watu warasimishe kazi zao. Lakini hata hapa; je huu ndio utakaokuwa utaratibu wa kuwaibua wajasiriamali na kuwapa misaada? Hawa mawaziri ndio watakaokuwa wakipita sehemu zote na kuamua nani apewe msaada, na kiasi kinachostahili kutolewa?
 
Stori yako kidogo (hapana, kikubwa), inatatiza.

Kwanza ni kama unapiga kampeni. Uchaguzi bado, ni kule 2025.

Lakini la muhimu zaidi, stori yako ni kama inashangilian watu kufanya shughuli zao nje ya taratibu?

Huyo mwenyekiwanda cha mafuta ya kula, mafuta hayo ni salama na ni ya kiwango?
Hapana, sijasema kumtia hatihati na kumweka ndani ilikuwa njiia sahihi. Kitu ninachokubali ni njia walizotumia hao mawaziri kusaidia hao watu warasimishe kazi zao. Lakini hata hapa; je huu ndio utakaokuwa utaratibu wa kuwaibua wajasiriamali na kuwapa misaada? Hawa mawaziri ndio watakaokuwa wakipita sehemu zote na kuamua nani apewe msaada, na kiasi kinachostahili kutolewa?
Dodoki hilo liache tu ndugu yangu.
 
Back
Top Bottom