Kwa hii aina ya demokrasia tunayolazimishwa kuifuata, itachukua miaka mingi sana kupata maendeleo

Kwa hii aina ya demokrasia tunayolazimishwa kuifuata, itachukua miaka mingi sana kupata maendeleo

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Nimetafakari sana nimeona hii demokrasia tunayolazimishwa kuifuata inazidi kutudidimiza. Iko kinyume kabisa na shughuli za maendeleo. Mabeberu waliona mbali sana kwa kutuaminisha kuwa WENGI WAPE. Na kuna wengine wana msemo wao wenye utata usemao "Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu"... binafsi sioni lazima ya WENGI WAPE ikiwa hao wengi hawana hoja nzito za kisayansi mezani.

Kwa mfano wafuasi wa Mwamposa, Kiboko ya wachawi, Kuhani Musa, Mkandamizaji, na manabii feki wengine ni wengi sana kiasi kwamba wana madhara kwenye sanduku la kura. Sasa kwa uwingi wao si wanaweza wakasababisha tukapata kiongozi mbovu kisa tu wengi wape?

USA waliona mbali sana ndo maana kwenye uchaguzi wao kuna kikundi cha watu wasiozidi 600 huamua nani awe Rais kwa kupiga kura baada ya wananchi wote kupiga kura. Yaani wananchi hata kama mlimchagua kiongozi wenu ni kuwa hicho kikundi ndo kina kauli ya mwisho nani awe Rais. UK na mfalme wao hawana muda na demokrasia za kipuuzi. Waarabu na wachina nao hawana huu ujinga tulio nao.

Pia kwenye hii demokrasia yetu tunatumia muda mwingi sana kwenye mijadala na kubishana badala ya kufanya maendeleo.

Kimsingi maendeleo hayahitaji kumbelezana wala mijadala mingi. Ninashauri Afrika tuamue jinsi gani ya kufanya mambo yetu bila kufuata hii demokrasia uchwara.
 
Wanaofanya hiyo mijadala ni kina nani? Usitupie lawama wengine ikiwa wewe mwenyewe upo hapa kushiriki kila mjadala + propaganda

Pia hata tukiacha kufuata hiyo demokrasia bado tunawez tusiendelee. Kuna nchi hazifuati demokrasia na hazijaendelea
 
Hakuna kikundi cha watu 600 kinachopiga kura kuamua nani awe Rais USA
 
Nimetafakari sana nimeona hii demokrasia tunayolazimishwa kuifuata inazidi kutudidimiza. Iko kinyume kabisa na shughuli za maendeleo. Mabeberu waliona mbali sana kwa kutuaminisha kuwa WENGI WAPE. Na kuna wengine wana msemo wao wenye utata usemao "Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu"... binafsi sioni lazima ya WENGI WAPE ikiwa hao wengi hawana hoja nzito za kisayansi mezani.

Kwa mfano wafuasi wa Mwamposa, Kiboko ya wachawi, Kuhani Musa, Mkandamizaji, na manabii feki wengine ni wengi sana kiasi kwamba wana madhara kwenye sanduku la kura. Sasa kwa uwingi wao si wanaweza wakasababisha tukapata kiongozi mbovu kisa tu wengi wape?

USA waliona mbali sana ndo maana kwenye uchaguzi wao kuna kikundi cha watu wasiozidi 600 huamua nani awe Rais kwa kupiga kura baada ya wananchi wote kupiga kura. Yaani wananchi hata kama mlimchagua kiongozi wenu ni kuwa hicho kikundi ndo kina kauli ya mwisho nani awe Rais. UK na mfalme wao hawana muda na demokrasia za kipuuzi. Waarabu na wachina nao hawana huu ujinga tulio nao.

Pia kwenye hii demokrasia yetu tunatumia muda mwingi sana kwenye mijadala na kubishana badala ya kufanya maendeleo.

Kimsingi maendeleo hayahitaji kumbelezana wala mijadala mingi. Ninashauri Afrika tuamue jinsi gani ya kufanya mambo yetu bila kufuata hii demokrasia uchwara.
Kama usemacho ni kweli, Africa ilitakiwa kuwa na maendeleo makubwa sana, maana huku kila kita anasifiwa kiongozi ndio kafanya.
 
Aisee mara nyingi mi nasema mabeberu kipnd wao wanaendelea hawakua na democrasia kama hii ya kwetu….ila baaada ya kufika kilelen mwa maendeleo yao ndo wakaone walete hii democrasia uchwara ili kutudhibiti sie wajinga…
 
Hoja Yako Ina mashiko sana ndio maana Huwa Nasema kupata kiongozi anae faa Kwa kupanga foreni na kutumbukiza makaratasikwenye sanduku ni kupoteza muda tu Kwa aina ya demokrasia na viongozi tulio nao mkuu.

Nchi kama hii kuendelea ni ndoto ya mchana.mfano ulitoa ni sahihi kabisa unao wahusu wakina mwamposa.

Leo hii mwamposa akichuana Joel nauka ama hata na malisa g hakika atawashinda mbali sana kwenye kura!

Maana wajinga wengi wata amini atafanya miujiza hata kuomba maji yatoke bila mabomba na watamwamini. Lakini wataachwa vijana wenye akili na maono kama joel ama malisa nk.

Kwa sasa tusubiri kizazi kingine mkuu.
 
Wanaofanya hiyo mijadala ni kina nani? Usitupie lawama wengine ikiwa wewe mwenyewe upo hapa kushiriki kila mjadala + propaganda

Pia hata tukiacha kufuata hiyo demokrasia bado tunawez tusiendelee. Kuna nchi hazifuati demokrasia na hazijaendelea
Jikite kwenye lengo la uzi.
 
Maendeleo sio pumzi kwamba kila mmoja awe nayo. Dunia hii wote tukiwa na maendeleo kipi kitakuwa kipimo cha kutoendelea. Mi nadhani demokrasia yetu inatufaa wenyewe kwa namna tulivyo kwenye nchi yetu binafsi
 
Siwezi kusoma huu uzi ila nacoment.mleta mada jaribu kutumia akili kidogo japo ulifeli fomu 4.rejea definition ya demokrasia ndo utaelewa na definition ni moja sio kwa matakwa ya mafisadi ya afrika.ukiendesha jamii yoyote ile kinyume na demokrasia madhara yake ni makubwa saana.mfano Tanzania tunapoteza wananchii zaidi ya 300,000 kwa mwaka kwa sababu ya umasikini na maradhi sababu ya ukosefu wa demokrasia na utawala wa sheria.
 
Kama usemacho ni kweli, Africa ilitakiwa kuwa na maendeleo makubwa sana, maana huku kila kita anasifiwa kiongozi ndio kafanya.
na wakati anaingia madarakani hakuwa na kila kitu zaidi ya maneno tu
 
Tanzania tuna demokrasia sifuri 0%kwa sababu kuna mhimili mmoja ambao unaongoza nchii.ukitaka kujua demokrasia nenda kenya wapo kwenye 70% at least mihimili ya kenya inafanya kazi japo bado wanapaswa kupush zaidi wawe bora hii nchii miaka 10 ijayo utaona matokeo.
 
Demokrasia ni michosho, inazuia maendeleo na inarudisha nyuma maendeleo yanayopatikana. Ndiyo maana nchi za magharibi zipo kwenye decline. Na demokrasia uchwara kama hizi zetu ni mbaya hata zaidi.
 
Nimetafakari sana nimeona hii demokrasia tunayolazimishwa kuifuata inazidi kutudidimiza. Iko kinyume kabisa na shughuli za maendeleo. Mabeberu waliona mbali sana kwa kutuaminisha kuwa WENGI WAPE. Na kuna wengine wana msemo wao wenye utata usemao "Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu"... binafsi sioni lazima ya WENGI WAPE ikiwa hao wengi hawana hoja nzito za kisayansi mezani.

Kwa mfano wafuasi wa Mwamposa, Kiboko ya wachawi, Kuhani Musa, Mkandamizaji, na manabii feki wengine ni wengi sana kiasi kwamba wana madhara kwenye sanduku la kura. Sasa kwa uwingi wao si wanaweza wakasababisha tukapata kiongozi mbovu kisa tu wengi wape?

USA waliona mbali sana ndo maana kwenye uchaguzi wao kuna kikundi cha watu wasiozidi 600 huamua nani awe Rais kwa kupiga kura baada ya wananchi wote kupiga kura. Yaani wananchi hata kama mlimchagua kiongozi wenu ni kuwa hicho kikundi ndo kina kauli ya mwisho nani awe Rais. UK na mfalme wao hawana muda na demokrasia za kipuuzi. Waarabu na wachina nao hawana huu ujinga tulio nao.

Pia kwenye hii demokrasia yetu tunatumia muda mwingi sana kwenye mijadala na kubishana badala ya kufanya maendeleo.

Kimsingi maendeleo hayahitaji kumbelezana wala mijadala mingi. Ninashauri Afrika tuamue jinsi gani ya kufanya mambo yetu bila kufuata hii demokrasia uchwara.
Inategemeana na jinsi mnavompata viongozi na huyo kiongozi mkuu. Hata ikiwa system ya chama kimoja anatakiwa akizi vigezo vyote na awe na uwezo. System iwe inafuata meritocracy.

Nchi kama Tanzania kimsingi ni kama nchi ya chama kimoja lakini bado inapata viongozi wabovu wakati China inawapa viongozi shupavu.
 
Back
Top Bottom