kwa hili alilofanyiwa malcom ni ubaguzi mkubwa na haufai kwenye soka!

kwa hili alilofanyiwa malcom ni ubaguzi mkubwa na haufai kwenye soka!

Its Pancho

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
15,966
Reaction score
26,404
Naandika hapa nikiwa na hasira na uchungu mwingi.
Baada ya Malcolm kuuzwa juzi hapa kwenda zenit St Petersburg ya huko Russia..
Sasa kimeibuka kioja kingine!
Mechi yao juzi waliotoka droo.
Mashabiki walikuwa na mabango yanayomtaka Malcolm auzwe haraka na hawamtaki kwani club yao haina utamaduni wa kusajili weusi!

Iliskika taarifa.
"sisi club yetu ipo pembezoni mwa mji na pia hatuna utamaduni wa kusajili watu weusi. ili kulinda utamaduni wetu
hatuchangamani na watu weusi kiakili wala vyovyote vile
Watu kutoka Pacific America kusini, Africa sisi hatupatani nao "

Sasa zenit nao wamepanga kumuuza Malcom ili kuwaridhisha mashabiki wao!

Mimi kama shabiki wa barca nilishasemaga rais wetu bartomeu na yule mkurugenzi wake wa ufundi (rafiki yake) na huyu kocha valvede hawatufai barca na hawafai kwa ustawi wa wachezaji! Ntakuja na kuelezea madudu yao wanayofanya shenzy!

Nawe Malcolm ni bora ungeendaga as Roma walipokutaka mwanzo. Yasingekupata haya 😢 😢
Uongozi wa sasa hivi barca haufai kwa kukuza wachezaji wao siku hizi wanataka mchezaji aliyetengenezwa huko tayari..

I stand with Malcolm 💪💪
 
Inawezekana mkuu sababu aliwafanyia roma uhuni ila Malcolm wa Bordeaux alikuwa ni balaa jengine aseeh 🔥 🔥
 
Malcom aliyataka kukimbilia barca, ila hawa wangese zenit si walikuwa na Hulk, kwani hulk ni mchina au!!?
 
Sasa mbona tetesi ninazosikia ni kwamba wanawake wa Kirusi wanawazimia sana watu weusi! Nasikia ukikanyaga tu, na ndoa anatangaza hapo hapo!
 
Hivi Barcelona imekuaje asee??? mbona inapoteza uwezo wa wachezaji wengi nowadays, kuna ulazima gani wa kutaka kumsajili kila mchezaji wakati timu inawachezaji wengi na wazuri
 
Hivi Barcelona imekuaje asee??? mbona inapoteza uwezo wa wachezaji wengi nowadays, kuna ulazima gani wa kutaka kumsajili kila mchezaji wakati timu inawachezaji wengi na wazuri
kweli kama nilivyosema mkuu uongozi wa sasa haufai!
wameshindwa kwenda na falsafa ya miaka yote ya kutengeneza wachezaji na sasa wamekuwa kituo cha kuharibu viwango vya wachezaji!
kuna dogo wa la masia xavi simon kiungo fundi uyo wamekauza jumla psg kisa hela ilikuwa nzuri!
hii barca ya bartomeu haitufai!
 
Putin na vibaka wenzie na team yao ya serikali ni wabaguzi sana
 
Halafu kuna Waafrika wenzangu (weusi) utashangaa likitokea timbwili la Russia vs USA, wengi wao wanakuwa upande wa Russia.Hawa Warusi ni wabaguzi kinoma!

Pamoja na kwamba Marekani ubaguzi bado ungalipo,lakini Urusi wamezidi.Kwa ufupi,nchi za Mashariki (za Kijamaa) zina ubaguzi mkali zaidi kuliko nchi za Magharibi (za Kibepali).Mfano,Angalia tofauti ya maisha ya Mwislamu anayeishi China na yule anayeishi US.
 
Back
Top Bottom