Pengine hamjui Maestro Ibrahim Masoud ni moja ya vichwa pale mawingu na kuchomoka kwake si jambo dogo.Maestro alikuwa mzuri zaidi kama director na mbunifu wa vipindi vingi.
Lakini pamoja na mapungufu yake yoooooote! Ruge ndio Ingine ya Clouds na ndio kila kitu hasa upande wa ubunifu na kuvumbua vipaji na namna ya kuvitumia.Hakuna mtangazaji ambaye kuondoka kwake kutaitikisa Clouds.
Ile dream team ya akina ML Criss,Bonny Love,Bobby,Fina,Amina Chifupa,Masoud Kipanya,Seven,Jimmy Kabwe,DJ Charles,DJ Boogie Master,Gadner Habash,Othman Njaidi etc woooooote hawa hawapo tena na walikuwa vichwa kupitiliza lakini bado radio haifanyi vibaya kama tulivyofikiri ingeweza kufa kabisa.
Kuna aliyetarajia kipindi kama cha Aspen kile cha Taji Liundi kuna mtu angeweza kufanya kiendelee kuwa juu? Lakini Sebastian Ndege akaja na njia panda na kinafanya vizuri ingawa si kama zamani kutokana na pia mabadiliko ya mambo mengi kama kuongezeka kwa matumizi ya vitu vingine kama TV programmes, watu kushinda wakichat kwenye mitandao n.k
Nadhani Ruge akitoka pale ndio Mawingu inaweza kwenda chini lakini si hawa watangazaji.