Kwa hili hongera Ommy Dimpoz

Kwa hili hongera Ommy Dimpoz

Innocizy

JF-Expert Member
Joined
Dec 5, 2011
Posts
1,736
Reaction score
1,056
Naomba niweke wazi kwanza kwamba mm si shabiki wake hata nusu. Lakini ni miongoni wa watu wanaotumia muda mwingi ktk social media ambako siku hizi hata TV na redios hazioni ndani kwa social media.

Mapema mwezi huu(sina hakika sana) zilisambaa picha za kijana Ommy Dimpoz akiwa kavaa "kishamba" ktk treni kana kwamba ni "m-bara" anaingia pale stesheni(kwa wale wa zamani mwakumbuka kelele za walete walete wa bara haooo,pale stesheni)

Picha hizo zilizua sana mjadala ktk hizi social networks za hapa kwetu na mijadala mingi ikiwa ni kumponda huyu kijana kwamba alikuja na furushi akiwa mshamba hajui kitu, na kwamba sahivi "anaringa" na anajisikia kwa kuwa kapata "vihela" lakini ajue yeye bado "wakuja" tu.

Sasa kijana akaamua kutoa picha akiwa na Vanessa Mdee na wamebeba lile lile furushi ikiwa ni project yao mpya inayokuja hivi karibuni. Kijana akaenda mbali akitusihi watanzania tuache "kukurupukia" mambo na kupashana habari ambazo sio za kweli.

Hapo ndio kanigusa.
Sisi watanzania tumekuwa watu wa "kunata" na beat iwe reggae hip hop mduara au blues sisi tumo tuu.

Nampongeza sana kijana kwa kuliona hilo na kututega tena na kiukweli ametuteka wengi sana maana ni wengi sana waliamini zile picha ni za kipindi anakuja kweli Dar.

Pia katukumbusha kwamba sisi ni wepesi pia wa kusahau na kuunganisha matukio,kwani hata clouds radio kuna kipindi mwaka huu ilidaiwa watangazaji wamepigana studio(hapo ndo walitutambua watanzania maana tulisema tukamaliza maneno yote) lakini ikaja bainika baadae kwamba lile lilikua tangazo la kampeni fulani(wachache sana walioshituka kabla,ila wengi tulijua ni kweli wametwangana ndo tukaponda haswaa).

Wakati haujapita hata mwaka kijana amerudia kitu kile kile na kweli ametukamata,kwa hili nikaona niandike tuu huu Uzi ingawa utawachosha wengi.

Kwa kweli kuanzia leo mm najitoa ktk chama cha kukurupuka na shukrani zimuendee huyu kijana.

Nilikua mmoja wa mashabiki waliotaka kijana apigwe pale dodoma kwa kauli yake ya "dharau" juu ya legendary wa hip hop bongo HAYATI ALBERT MANGWEIR aka Ngwair.

Lakini naamini hata wakati ule pia nilikurupuka maana kwa hustle za HAYATI alizozifanya,jasho lake lilitakiwa lionekane hata sasa kwa familia yake...lakini mafisadi wachache ndio waliofaidika na jasho la hayati.

Kutokana na surprise hii ya huyu kijana nimejitoa rasmi timu kukurupuka.

NISAMEHENI KWA LI UZI REFU JAMANI.

NIMEWAWEKEA NA PICHA HIZI HAPA.

Asanteni.
 

Attachments

  • 1413927400078.jpg
    1413927400078.jpg
    46.6 KB · Views: 1,080
  • 1413927416551.jpg
    1413927416551.jpg
    60.1 KB · Views: 1,058
mhh unafki unakusumbua. wakat omy dimpoz mwenyewe kakiri ni kweli alipigwa hyo picha kitambo na uncle wake akiwa anatoka msiban kigoma...... na huoni hiyo picha nyingne na vee money ni mpya kuliko iyo ya peke ake?

Lahaula Lakwata.......... Ommy Dimpozi alikiri lini na wapi??????????????

watu kwa kutunga habari hamjambo... ukipewa picha maelezo watemgemeza mwenyewe
 
mhh unafki unakusumbua. wakat omy dimpoz mwenyewe kakiri ni kweli alipigwa hyo picha kitambo na uncle wake akiwa anatoka msiban kigoma...... na huoni hiyo picha nyingne na vee money ni mpya kuliko iyo ya peke ake?

Achaga uongo basi aisee. Unapata faida gani ukiongea kitu usichokua na uhakika nacho?
 
Ndio nazidi ona jinsi gani chuki na u-mm unaendelea kutukurupusha.
 
Yaani chuki inafanya mtu asijikite ktk hoja anaanzisha hoja nyingine....

Tembelea bongo5.com usome hiyo habari.
 
Hii imenoga nayo...

Umeona eeh!!watu wameanza kuacha hoja wamekurupuka wananiita dimpoz hahaha....nataka wakisha kurupuka nawapa my real name plus evidence waendelee kukurupuka zaidi.
 
Sijui na mimi nimekurupuka?? maana hata sielewi nini kinaongelewa aliyeelewa asamaraizi
 
Trousers aliyovaa Dimpoz kwenye picha ya juu si ile iliyovaliwa kwenye picha ya chini,hata rangi ni yofauti..angalia kwa umakini utabaini..
 
mhh unafki unakusumbua. wakat omy dimpoz mwenyewe kakiri ni kweli alipigwa hyo picha kitambo na uncle wake akiwa anatoka msiban kigoma...... na huoni hiyo picha nyingne na vee money ni mpya kuliko iyo ya peke ake?

hahahaha picha ya mwenyewe ni ya zamani kuliko aliyopiga na mdee???? OMG!! kwa hiyo alizihifazi hizo nguo toka zamani hizo akijua ipo siku atakuwa msanii aje aziigizie??? aliyetuloga watanzania Mungu asimsamehe milele.
 
hahahaha picha ya mwenyewe ni ya zamani kuliko aliyopiga na mdee???? OMG!! kwa hiyo alizihifazi hizo nguo toka zamani hizo akijua ipo siku atakuwa msanii aje aziigizie??? aliyetuloga watanzania Mungu asimsamehe milele.

Kwa kweli
 
Back
Top Bottom