Kwa hili namuunga mkono Mheshimiwa Mbowe.

Kwa hili namuunga mkono Mheshimiwa Mbowe.

Rwebo

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2015
Posts
1,418
Reaction score
1,820
Ni kuhusu swala la Polisi wetu kukamata watu kihuni. Mara nyingi tume shuhudia Polisi wakikamata watu kihuni, hapa sizumgumzii mambo ya utekaji nyala, isipokuwa ule ukamataji wa kawaida labda mtu anahisiwa kuwa mwizi na makosa mengine. Polisi wa nakuja na gari lina namba ya nchi za nje hasa South Africa na Singapore. Polisi wamevaa Jeans wana rasta na mizula kichwani, serikali ya Mtaa haina habari wala mjumbe wa nyumba kumi hana habari. Sasa imetosha serikali iseme hadharani kuwa ni marufuku Polisi kwenda kwa mtu iwe usiku au mchana kumueka chini ya ulinzi na kuondoa naye bila kuwepo uongozi wa serikali ya Mtaa au kitongoji na mjumbe wa nyumba kumi. Na pawepo kitabu/Register ambapo kiongozi wa operation hiyo ataandika jina jake kamili na cheo chake, sababu za kutaka kutaka kuondoa na mtuhumiwa na anapelekwa kituo gani. Na lazima wawe na vitambulisho halali vya kazi na ikiwezekana vya NIDA kwani vya kazi anaweza kughushi. Mbowe umesema Ukweli kuwa tunashikwa ' Kihuni na Kiboya'. Itoshe kusema Watanzania tupaze sauti imetosha.
 
Kuna MTU Jana kule Twitter kasema kuwa "tumewajua kwa Sura na majina watekaji, tunaapa this time nao familia zao zitalia". Nikaogopa Sana maana tunakoelekea sio kuzuri, tunawapa nafasi wahuni kutumia Polisi kuleta shida kwenye jamii
 
Ni kuhusu swala la Polisi wetu kukamata watu kihuni. Mara nyingi tume shuhudia Polisi wakikamata watu kihuni, hapa sizumgumzii mambo ya utekaji nyala, isipokuwa ule ukamataji wa kawaida labda mtu anahisiwa kuwa mwizi na makosa mengine. Polisi wa nakuja na gari lina namba ya nchi za nje hasa South Africa na Singapore. Polisi wamevaa Jeans wana rasta na mizula kichwani, serikali ya Mtaa haina habari wala mjumbe wa nyumba kumi hana habari. Sasa imetosha serikali iseme hadharani kuwa ni marufuku Polisi kwenda kwa mtu iwe usiku au mchana kumueka chini ya ulinzi na kuondoa naye bila kuwepo uongozi wa serikali ya Mtaa au kitongoji na mjumbe wa nyumba kumi. Na pawepo kitabu/Register ambapo kiongozi wa operation hiyo ataandika jina jake kamili na cheo chake, sababu za kutaka kutaka kuondoa na mtuhumiwa na anapelekwa kituo gani. Na lazima wawe na vitambulisho halali vya kazi na ikiwezekana vya NIDA kwani vya kazi anaweza kughushi. Mbowe umesema Ukweli kuwa tunashikwa ' Kihuni na Kiboya'. Itoshe kusema Watanzania tupaze sauti imetosha.

Kukomaa dhidi ya kutekwa sawa, lakini kumshauri chura kiziwi, kwani hawajui watekaji?
 
Mtu amepata Dv 4 ,akaenda polisi kwa kuunga unga,mara akarisiti mara paap kapata credit.Huyoo form 6.Chaap kapata 4 pia kaunga ungaa kapata credit paap Chuo,

Mara paap IGP then utegemee nini hapo😂😂
 
Mtu amepata Dv 4 ,akaenda polisi kwa kuunga unga,mara akarisiti mara paap kapata credit.Huyoo form 6.Chaap kapata 4 pia kaunga ungaa kapata credit paap Chuo,

Mara paap IGP then utegemee nini hapo😂😂
Mkuu Kuna std 7 wana akili na busara kuliko wasomi. Suala si kufeli mitihani ya makaratasi, suala ni namna tunavyoendesha mambo yetu ndani ya nchi.
Hata wewe kama umesoma ukipewa huo uigp unaweza jikuta unaendeshwa na siasa na mifumo yake na ukaishia kukamata watu hovyo hovyo ukaweka elimu pembeni.
 
Mkuu Kuna std 7 wana akili na busara kuliko wasomi. Suala si kufeli mitihani ya makaratasi, suala ni namna tunavyoendesha mambo yetu ndani ya nchi.
Hata wewe kama umesoma ukipewa huo uigp unaweza jikuta unaendeshwa na siasa na mifumo yake na ukaishia kukamata watu hovyo hovyo ukaweka elimu pembeni.
Uwe unaelewa somo usinilishe maneno yako.

Ukifeli sarasa la saba umefeli reasoning ability(Tofautisha kufeli na kuchaguliwa kwenda kidato cha kwaza au hatua inayofuata)

Huyo njia umepitia kwa kuunga unga then upewe nafasi kubwa means uwezo wako wa kuchanganua mambo ni mdogo.
 
Uwe unaelewa somo usinilishe maneno yako.

Ukifeli sarasa la saba umefeli reasoning ability(Tofautisha kufeli na kuchaguliwa kwenda kidato cha kwaza au hatua inayofuata)

Huyo njia umepitia kwa kuunga unga then upewe nafasi kubwa means uwezo wako wa kuchanganua mambo ni mdogo.
Boss, Nakwambia hivi, nenda pale kapewe uigp halafu ukipewa maagizo ya kutawanya mkutano wa hadhara wa upinzani toa cheti chako sema mm nimesoma nina phd elimu yangu hairuhusu kutawanya mikutano kiholela ndo utaelewa kwanini suala si elimu ya makaratasi tu.
 
Boss, Nakwambia hivi, nenda pale kapewe uigp halafu ukipewa maagizo ya kutawanya mkutano wa hadhara wa upinzani toa cheti chako sema mm nimesoma nina phd elimu yangu hairuhusu kutawanya mikutano kiholela ndo utaelewa kwanini suala si elimu ya makaratasi tu.
Hapo unakuja kwenye point yangu.reasoning.Nyarandu alikataa Uwaziri akasema hawezi fanya kazi na magufuli,Straight ni reasoning.

Kama umefeli kuna uwezekano mkubwa ukashindwa namna ya kuwatawanya watu kwa amani.

Ili upewe nafasi lazima tuone cheti kwanza mzee ndio dunia ilivyo
 
Hapo unakuja kwenye point yangu.reasoning.Nyarandu alikataa Uwaziri akasema hawezi fanya kazi na magufuli,Straight ni reasoning.

Kama umefeli kuna uwezekano mkubwa ukashindwa namna ya kuwatawanya watu kwa amani.

Ili upewe nafasi lazima tuone cheti kwanza mzee ndio dunia ilivyo
Upo sawa mkuu, ila Tanzania unaweza pewa nafasi cheti kikafata. Jpm alifuta vyeti feki kibao. Yaani tunarudi pale pale, namna tunavyoendesha mambo yetu.
 
Tutengeneze taasisi imara badala ya kujenga majina ya watu!

Kama jeshi la polisi linafanya KAZI kinyume Cha Sheria maana yake sio taasisi imara Kwa wananchi bali ni taasisi ya majina makubwa inayofanya Kwa kuwafurahisha wenye majina makubwa!!
 
Tatizo linalotengenezwa litakuja kuwageuka wenyewe wanaolitengeneza.Siku itafika kibao kitawageuka kwasababu wananchi wanazidi kupoteza imani na jeshi la polisi.Itafika hatua kila mtu atajihami kwa jinsi anayoijua.
 
Back
Top Bottom