Kwa hili wazazi wa ki-Tanzania na wengine wenye tabia hizi mjifunze!

Kwa hili wazazi wa ki-Tanzania na wengine wenye tabia hizi mjifunze!

Ryzen

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2012
Posts
7,301
Reaction score
8,706
Habari za usiku,

Nisiposema hili nitalaaniwa hata, Katika makuzi yetu kwa Namna moja ama nyingine tumeweza kuwakosea wazazi wetu hasa kina mama..

Hawa mama zetu ukiwakosea wanakimbilia Haraka Kulaani, Leo nikiwa napita Mtaa mmoja Nilisikia Dirishani kwenye Nyumba za Kupanga Mama Mmoja akimuadhibu kwa fimbo binti yake ambaye yupo shule ya Msingi na kwa mazungumzo yao Nadhani Binti yupo darasa la Nne..

Binti huyu anaadhibiwa kwa fimbo randomly kwa sababu ya kuficha makaratasi ya matokeo yake ambayo mama yake anahisi amefeli..Kilichonisikitisha ni lugha alokuwa akitumia Mama yake lugha iliyokaa kama kumlaani na maneno kama Sugu, Jambazi na hata kumlalamikia Mungu kwanini kampa mtoto kama huyo..

Hii ikanikumbusha mbali, enzi hizo mama yangu pia alikuwa akitumia maneno ambayo kweli mzazi hupaswi kumtamkia mwanao maana hayabariki, Maneno kama Kumuita mwanao Jambazi,Malaya,Muhuni au hata kumlaumu Mungu kwa aina ya Mtoto wako na mengine mengi ambayo kwa kweli hayabariki!

Mara Pengine Ndugu wazazi haya maneno yenu huumba, unamtamkia mwanao maneno maovu na yasiyobariki mwisho wa siku akiishia kubaya ni sawa na wewe umemlaani na akiharibika ni matokeo ya laana yako na atakuwa mzigo wako tena.

Ndugu wazazi Nashauri Mwanao anapokosea kwanini usiseme hata Kimoyomoyo ya kwamba Mungu amsamehe kwa kuwa hajui atendalo na amjalie aindee njia iliyo sawa?

Tujifunze.. zama zimebadilika..Zungumzeni kwa upole na busara na Wanenu kuliko kuishia kuwapa maneno yasiyobariki!


Mungu Mwenyezi Awajalie Usiku Mwema!
 
Tukana matusi yote ila usiniite mjinga au sijitambui..
 
Sasa katika hayo mzazi wako alikuita ukiwa mdogo lipi limeshaumba sasa hivi!!!
 
Hili ni janga mkuu hizi jamii zetu tunazoishi Mungu atusaidie Nina dada yangu Sasa amepotea kabisa yani sababu ya maneno machafu ya baba yake wazazi hata mtoto akifel shule tafuteni njia nzuri za kumsaidia sio kila saa unamsimanga badala ya kujali Utu wake wewe unaangalia garama zako tu alafu unamuuacha tu nyumbani hamsaidii kwa chochote unaamka unamuona badala hata ya kumpa msaada wewe unajifanya haujali eti hasira akipotea kabisa Sasa Na kuanza jiingiza kwenye makundi ya hovyo lawama zinaenda kwa akina mama akina baba tunajitoa kabisa kwenye hili, ni wakati Sasa wa kuachana Na Yale malezi yamazoea Dunia imebadilika Na nyie mbadilike wasaidieni watoto wenu wafikie ndoto zao Na sio rahisi watoto wako wote wakawa Na akili sana watakuwepo ambao ni slow learner Ila nenda nao hivo hivo polepole mpaka wafikie ndoto zao
 
Hili ni janga mkuu hizi jamii zetu tunazoishi Mungu atusaidie Nina dada yangu Sasa amepotea kabisa yani sababu ya maneno machafu ya baba yake wazazi hata mtoto akifel shule tafuteni njia nzuri za kumsaidia sio kila saa unamsimanga badala ya kujali Utu wake wewe unaangalia garama zako tu alafu unamuuacha tu nyumbani hamsaidii kwa chochote unaamka unamuona badala hata ya kumpa msaada wewe unajifanya haujali eti hasira akipotea kabisa Sasa Na kuanza jiingiza kwenye makundi ya hovyo lawama zinaenda kwa akina mama akina baba tunajitoa kabisa kwenye hili, ni wakati Sasa wa kuachana Na Yale malezi yamazoea Dunia imebadilika Na nyie mbadilike wasaidieni watoto wenu wafikie ndoto zao Na sio rahisi watoto wako wote wakawa Na akili sana watakuwepo ambao ni slow learner Ila nenda nao hivo hivo polepole mpaka wafikie ndoto zao
Pure truth
 
Umesema vyema muungwana. Hili suala ni changamoto sana kwenye jamii yetu hasa hii ya kipato cha chini.
 
Kuna mdada alikuwa na kaka yake wote tulikuwa darasa moja sasa yule mdada alikuwa ni slow learner na hata nyumbani alikuwa akichelewa kufika, basi kaka yake alikuwa akijitahidi kufanya vizuri huku akimuacha mbali dada yake. Baba yake Mkurya alikuwa akipendezwa sana na mwanae huku akiwa anamgombeza mara kwa mara bintiye kwa kumuita majina mabovu na mabaya, alikuwa akimuita Kiazi au Tikiti maji, mara nyingine alikuwa akimwambia kichwani kwake hakuna ubongo yamejaa maji tu, akimaanisha hana akili.

Ilifikia hatua yule mdada akaikosa amani ya nafsi ila ndio keshakuwa hivyo atafanyaje, akajitahid hivyo hivyo tukamaliza darasa la saba, kaka yake hakuchaguliwa kuingia sekondari akapelekwa Thaqaafa, dada mtu akachaguliwa Mwanza Sec. Dada mtu akamuomba baba yake ahamishiwe Nganza akahamishwa akasoma mpaka form 4 akafaulu, kaka mtu akapiga chini akaanza mziki wa kurisiti. Leo hii dada mtu ni mwanasheria, kaka mtu alijikongoja akafanikiwa CBE lakin mpaka anakuja kumaliza, dada ake alikuwa anafanya kazi.

Mara nyingine mzazi waweza kuona tumaini lako ni kwa mtoto fulani, ukawapuuza wengine lakini Mungu alivyokuwa wa ajabu akawainua hao unaowaona dhaifu ukabaki kinywa wazi. Goodmorning
 
Back
Top Bottom