Kwa hili Zantel hamtendi haki kwa wateja wa modem zenu

Kwa hili Zantel hamtendi haki kwa wateja wa modem zenu

mhondo

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2011
Posts
968
Reaction score
354
Kitendo cha Kampuni ya simu za mkononi ya zantel kulazimisha wateja wao wa modem wanaolipia malipo ya internet kwa malipo ya kabla kupitia huduma ya/za Z-Mono na nyinginezo kwa ajili ya matumizi ya mwezi na ikatokea mtumiaji wa huduma hiyo kumaliza matumizi ya megabytes alizopewa kabla ya mwezi na akataka kulipia tena huduma hiyo kukataliwa kufanya hivyo siyo sahihi. Mteja anapomaliza megabytes alizopewa kabla ya muda analazimishwa kununua huduma nyingine yenye bei kubwa zaidi kuliko aliyotumia mwanzo. Kwa kitendo hiko ni wazi kuwa mnajikosesha mapato mengi kwani kwa wateja walio wengi wataacha kutumia hizo modem hadi kipindi alichozuiliwa kimalizike. Na ikumbukwe kwamba hata watumiaji hao wa internet wana uwezo tofauti wa fedha hivo siyo sahihi kulazimisha mtu kununua huduma ambayo hana uwezo nayo wa kuilipia.
 
Kitendo cha Kampuni ya simu za mkononi ya zantel kulazimisha wateja wao wa modem wanaolipia malipo ya internet kwa malipo ya kabla kupitia huduma ya/za Z-Mono na nyinginezo kwa ajili ya matumizi ya mwezi na ikatokea mtumiaji wa huduma hiyo kumaliza matumizi ya megabytes alizopewa kabla ya mwezi na akataka kulipia tena huduma hiyo kukataliwa kufanya hivyo siyo sahihi. Mteja anapomaliza megabytes alizopewa kabla ya muda analazimishwa kununua huduma nyingine yenye bei kubwa zaidi kuliko aliyotumia mwanzo. Kwa kitendo hiko ni wazi kuwa mnajikosesha mapato mengi kwani kwa wateja walio wengi wataacha kutumia hizo modem hadi kipindi alichozuiliwa kimalizike. Na ikumbukwe kwamba hata watumiaji hao wa internet wana uwezo tofauti wa fedha hivo siyo sahihi kulazimisha mtu kununua huduma ambayo hana uwezo nayo wa kuilipia.

Mkuu tuwaache mara ngapi???,
mimi walinipoteza walivyo-force nitumia voice calls elfu 5 kwa wiki ili niweze kujiunga Highlife, yaani hata modem sikumbuki ni wapi nilishaitupa
 
  • Thanks
Reactions: LAT
duh wanakera kweli now natumia ya voda ila sasa inawekewa line tena inanitoa hewani
 
i am an obedient user of airtel after realizing zantel's shit
 
Mwanzo niliwapenda sana walipoanza kulazimisha ni lazima utumie voice service ya 5000 kila wiki ndio uweze kujiunga na 2GB weekly nikihuzunika sana but kama kawa mlango mwingine ulikuw awazi sana Airtell wako fast kuliko mwanzo na wanatoa 3GB so just switch....
 
Mi nilishatupa modem zamani sasa hivi natumia cm yangu ya nokia kama moderm huwa natumia line ya voda. Wazembe hawajui biashara, wanafikiri tuko zenji hapa
 
Tatizo ni kuwa wamegundua hawana mpinzani kwenye data ndio maana wanafanya wanavyotaka,mimi nimetangatanga wee na sasa nimekubali yaishe nimerudi Zantel,kisa huko kote kwingine speed ya mtandao ni kama injini inayotumia mkaa wa mawe,mara mtandao uwe chini mara upotee kuattach kapicha utachukua mwaka mzima,na ukiwa mikoani ndio usiseme,na mwisho hasira zangu ni mijitu ya TCRA sijiu inafanya nini,uprofessa wa buure kabisa,sector ya mawasiliano nafikiri ndio sector inayomwiba mtumiaji kuliko sector yoyote hapa bongo,TACRA wako kwenye kuidhinisha masafa na kusajiri radio tu,hawana jipya hii ni AIBU kwao,nchi hii kila mwenye dhamana anaangalia tumbo lake tu,hapo nyuma nilifikiri wasomi watasaidia nji hii na wananchi wake lakini wapii
 
Hii ni balaa wadau yaani 1GB week moja imeisha harafu inabidi nisubili hadi mwezi uishe juzi nikaweka vocha ya buku mbili mh nusu saa kwisha kazi leo asubuhi nimetupa moderm nipo Airtel wacha niangalie upande wa pili!
 
jamani lazima mutumia mitandao ya simu for internet? kwanini musitumie uhuruone au powernet
 
Hii inakera sana!!! Ukweli kuwa modem za zantel ziko fast, lakini huku kulazimisha watu kutumia 5000 kwa siku 7 kujiunga na highlife weekly na 10000 kwa siku 15 kujiunga na 2GB monthly ni uhuni!!!!
 
Back
Top Bottom