Kwa hiyo nikarisiti au nisubiri tume???

Zacharia Kifyasi

Senior Member
Joined
Dec 23, 2012
Posts
135
Reaction score
24
Wakuu naomba mawazo yenu, nilifanya mtihani kama mtahiniwa wa kujitegemea na matokeo ndo kama hivyo, Pinda anaunda tume kuchunguza kilicho tokea. Je nisubiri matokeo ya tume ya pinda au nikarisiti? Pia Nimeona hotuba ya mkuu wa kaya, ya mwisho wa mwezi wa february, Dah inakatisha tamaa!
 
We nenda karisiti tume za kibongo hazitabiriki!
 
Karisti mdogo wangu usipoteze muda hiyo tume majibu mpka mwakani.
 
Mkuu wangu Zacharia Kifyasi pole kwanza kwa matokeo hayo japokuwa naamin ulikuwa na uwezo kufanya vyema zaidi ya hapo sema tu mfumo mbovu wa baraza letu la mitiihani, kwa ushauri ni vyema kabisa ukajiandikishe kurisiti kabisa ili tarehe ya mwisho isije kupita na kipindi hicho unakuwa tayari umerisiti basi unaanza kusubiria majibu ya tume na kwa kufanya hivi itakuhakikishia uhakika wa wewe kuliko kusbiria hawa wanasiasa wapumbavu ambao kazi yao ni propaganda tu ili upepo upite.
 
Last edited by a moderator:
Tarehe ya mwisho kwa hawa watoto wetu kujiandikisha kurisiti ni nilini wadau? ninakajomba kamepata four.
 
Nenda karisiti ndugu ripoti itakuja baada ya mwaka na nusu! Time is not for you!
 
Tume haija undwa kutengua matokeo hasha imeundwa kwa ajili ya kuchunguza sababu ya wanafunzi kufeli kwa kikubwa hivi.We nenda kajiandikishe tu kwenye hivyo vituo vya ku resit.
 

pole man.
>Kurisiti ni mradi wa baraza,utapoteza pesa hadi ujute.
>Kwan kunawatu ninaowajua wamerisiti zaidi ya x6
>ukiweza tafuta ishu nyingne kwa hiyo four yako.
>Mf. Kuna dogo kafanya mpango na sasa anasomea Nursing. Alimaliza mwaka juz.
 

Mkuu, we angalia ustaarabu wa maisha yako ya mbele. Ukikaa na. Kungoja matokeo ya tume utapoteza muda wako bureee na usipate majibu tofauti na yaliyopo.
Kama credit zipo za kutosha kukuwezesha kuendelea nakushauri uulizie CBE certificate entry requirements zikoje.
Ukianza na certificate itakusaidia then unaendelea from there

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 

lakini D mbili zitanisaidia nini mkuu! Naumia sana mtihani ulikuwa simple lakini majibu ni tofauti na nlivyo tegemea..... Government ya masharobaro hii ndo iliyo sababisha haya.
 
hiyo tume ni ya kuchunguza kwanini mmefeli haitabadilisha hayo matokeo kuwa ziro ziwe div four na four ziwe three matokeo yatabaki hivyo hivyo sana sana watakachoamua kwa kuwahurumia pengine hamtalipa ile fees ya exam kama wakiamua lakini kurudia upo pale pale hakuna shortcut kwenye elimu ndugu yangu labda uende ukajiunge na certificate mwaka 1 then diploma miaka 2 halafu na degree miaka 3 mwisho kama na masters miezi 18 (mwaka mmoja na nusu) total 7.5 years hii haikwepeki mdogo wangu. kila la kheri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…