Kwa Jenister Mhagama na Prof. Joyce Ndalichako

Kwa Jenister Mhagama na Prof. Joyce Ndalichako

Bajeti ya kunguru

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2014
Posts
1,379
Reaction score
1,069
Wasalaam waheshimiwa mawaziri, waziri wa kazi,ajira, vijana na walemavu mh. Jenister Mhagama na waziri wa elimu sayansi na teknolojia mh. Prof. Joyce Ndalichako. Awali ya yote ninayo furaha kutoa pongezi zangu kwenu kwa uteuzi mlioupata, ni kwamba mpaka sasa taifa lina matumaini na mategemeo makubwa kutoka kwenye utendaji wenu na usimamizi wenu. Nisiwachoshe kwa salamu naomba niende moja kwa moja kwenye kusudio la pili la kalamu hii.

Tanzania kwa sasa si miongoni mwa nchi maskini ulimwenguni, kutokana na hatua hii nzuri tuliyopo tumeanza kupata heshima walau kidogo kwa kuvuka sifa za kinachoitwa misaada kwa nchi maskini, ambayo ni hatua kuelekea heshima kamili ambayo tunastahili kuwanayo.

Maendeleo ya nchi yana uwanja mpana wa kuyaelezea katika njia kuu zake mbili KIBEPARI na KIJAMAA. Changamoto kubwa ni kuwa makundi yote huwa yamo ndani ya kila taifa ila kwenye kipaumbele cha taifa ndipo kundi moja hulazimishwa ku surrender.

Ni wazi akili na mioyo ya watanzania waliowengi ipo ki mfumo wa ujamaa,unaweza ukasema ni wavivu lakini hakuna ukweli, wengi hutegemea serikali ndiyo yenye mamlaka na maamuzi ya mustakabali wa maendeleo ya maisha yao na vijana wao.

Kutokana na mantiki hiyo ilijengeka ndani ya jamii yetu watanzania, kuna sehemu imeonekana mambo yamesimama. Hakuna ubishi idadi ya wananchi inazidi kuongezeka kila uchwao. Kuongezeka kwetu Sio mzigo bali ndio utajiri wetu.

Jitihada za kuongezeka kwetu zipo, jitihada za kuwasomesha watoto wetu zipo ila tatizo linakuja kutokuwa na lengo la kumtegemeza kijana tuliyemsomesha ili awe na uwezo wa kujitegemea na kurudisha mchango serikalini wa gharama zilizotumika kumuwezesha.

Kama nilivyoeleza awali,jamii ya watanzania inamizizi ya mfumo wa kijamaa, mfano pale serikali ilipoamua elimu ya sekondari ikuzwe/iboreshwe ili kufanya watoto wengi waweze kuipata, watanzania waliitikia na hata pale walipokwama gharama serikali iliwasaidia mpaka sasa tupo kwenye mfumo wa elimu bure. Haihitaji kueleza kinaga ubaga watanzania tulipata mshangao wa namna gani na faraja kiasi gani kutoka kwa serikali yetu (hivi ni viashiria vya ujamaa ndani ya mioyo ya watanzania).

Baada ya kuwasomesha watoto wetu wanaturudia majumbani kukaa huku wakiwa na matumaini ya ajira na miaka inazidi kwenda. Hapa kuna tatizo la kiufundi. Haiwezekani serikali iendelee kula hasara kwa kuwasomesha watoto wetu na kuwaacha tu hivi hivi. Turudi kwenye makini zetu, kila jambo tunalolifanya tujue namna ya kupata return chanya yake, tusiendelee kufanya jambo ambalo hatujauandaa mwisho wenye manufaa.

Maoni yangu binafsi ni kuwaunganisha nyie wawili muweze kutuletea mfumo wa elimu ambao utakaolazimisha elimu ya ufundi/ujuzi kuwa ya lazima kwa kila mtoto atayeshindwa kuendelea na masomo ya sekondari. Madhumuni ya mfumo huo uwe ni

(i). Kurudisha gharama za serikali zilizotumika kuwaelimisha watoto wetu kwa kuchukua asilimia fulani ya mapato watayoyapata kutokana na shughuli za ujuzi walioupata.

(ii). Kuwategemeza watoto wetu watuondokee majumbani. Mtoto/ kijana anapokuwa na ujuzi fulani anakuwa anauwezo hata wa kupata senti kadhaa hivyo atakuwa na hamu ya kutoka kwa wazazi wake na kwenda kuanza maisha yake (jeuri ya pesa).

(iii). Utulivu wa jamii yetu kama watanzania. Vijana wengi ambao hawana ajira wengi wao hujikuta tena hawana familia (kuoa/kuolewa) hivyo huwa wanakuwa watu rahisi kuwashawishi katika mambo ya uvunjifu wa amani kwani huwa hawana jasho la kulilinda.

Kuna faida nyingi zitazopatikana kutokana na kurekebishwa kwa tatizo hilo la kiufundi.

Nyinyi ndio mpo hapo juu na mnaona kwa mapana zaidi tofauti na mimi ila wote dhumuni letu kubwa litabaki lile lile KUIJENGA TANZANIA MOJA.

Nawasilisha.


MAGUFULI4LIFE.
 
Ni bahati mbaya sana kuwa hapo hakuna mbunifu hata mmoja. Wote ni wa kusubiri maagizo kutoka juu.
Mawaziri ni kama Prof. Sospita Muhongo, mtu wa kazi, anajiamni na ana maono.
 
Ni bahati mbaya sana kuwa hapo hakuna mbunifu hata mmoja. Wote ni wa kusubiri maagizo kutoka juu.
Mawaziri ni kama Prof. Sospita Muhongo, mtu wa kazi, anajiamni na ana maono.
Wa hivyo ndio hawatakiwi kwa jiwe.
 
Huyo Ndalichako na Jenister mhagama warekebishe upande wa ajira, wao wenyewe wamewahi kujiajiri?
Hamis WA Nzega Yupo Wapi Sasa Hivi?
Alikuwa Anasema Vijana Mjiajiri 😀😁😂😅😏
 
"Tanzania kwa sasa si miongoni mwa nchi maskini ulimwenguni, kutokana na hatua hii nzuri tuliyopo tumeanza kupata heshima walau kidogo "

Acha uongo na upuudhi wewe mpumbavu sijui umetumia vigezo gani,embu soma hapo chini ujue ukweli
Tanzania ni miongoni mwa nchi kumi maskini zaidi duniani tukiwa chini ya utawala wa Chama Cha Majambazi tokea uhuru wetu.

"jamii ya watanzania inamizizi ya mfumo wa kijamaa, mfano pale serikali ilipoamua elimu ya sekondari"
nakufahamisha kwamba nchi nyingi zinazofuata sera za kibepari zinatoa elimu bure tena "elimu bora" na sio bora elimu ya kwetu kuanzia chekechea,sekondari , hadi chuo kikuu

" Kurudisha gharama za serikali zilizotumika kuwaelimisha watoto wetu kwa kuchukua asilimia fulani ya mapato watayoyapata kutokana na shughuli za ujuzi walioupata." kuna kitu kinaitwa SDL kipo waajiri wanalipiswa iyo kodi kitambo tu .

Hao uliowataja wapo madarakani kwa zaidi ya miaka 5 hakuna chochote cha maana walichofanya kwa taifa zaidi ya kujinufaisha wao na familia zao.

Kama unawategemea wao eti utendaji wao wa kazi utakuletea maendeleo unajidananya au umeleta mapambio ya kisiasa tu apa , ii nci ina mawaziri ao kwa zaidi ya miaka 60 ila bado ipo kati ya nci 10 maskini zaidi duniani.

Nakushauri achana na wanasiasa tena hizo siasa zako za upambe eti MAGUFULI4LIFE (utakuwa mpuudhi sana wewe halafu)
hawana mpango na wewe zaidi ya kukutumia na kukudanganya, fanya kazi kwa bidii wewe binafsi, jitume ili upate maendeleo na upunguze maumivu ya maisha na kuongeza furaha kwako na familia yako.

Usimtegemee mwanasiasa akuletee maendeleo tena awa ambao wapo madarakani tokea nchi ipate uuru, hao wapo kwa maslahi yao binafsi na sio kwa maslai yako na taifa.

usiponielewa utaendelea kuwa maskini wewe na kizazi chako chote , amka acha kuwa mpambe wa wanasiasa
 
"Tanzania kwa sasa si miongoni mwa nchi maskini ulimwenguni, kutokana na hatua hii nzuri tuliyopo tumeanza kupata heshima walau kidogo "

Acha uongo na upuudhi wewe mpumbavu sijui umetumia vigezo gani,embu soma hapo chini ujue ukweli
Tanzania ni miongoni mwa nchi kumi maskini zaidi duniani tukiwa chini ya utawala wa Chama Cha Majambazi tokea uhuru wetu.

"jamii ya watanzania inamizizi ya mfumo wa kijamaa, mfano pale serikali ilipoamua elimu ya sekondari"
nakufahamisha kwamba nchi nyingi zinazofuata sera za kibepari zinatoa elimu bure tena "elimu bora" na sio bora elimu ya kwetu kuanzia chekechea,sekondari , hadi chuo kikuu

" Kurudisha gharama za serikali zilizotumika kuwaelimisha watoto wetu kwa kuchukua asilimia fulani ya mapato watayoyapata kutokana na shughuli za ujuzi walioupata." kuna kitu kinaitwa SDL kipo waajiri wanalipiswa iyo kodi kitambo tu .

Hao uliowataja wapo madarakani kwa zaidi ya miaka 5 hakuna chochote cha maana walichofanya kwa taifa zaidi ya kujinufaisha wao na familia zao.

Kama unawategemea wao eti utendaji wao wa kazi utakuletea maendeleo unajidananya au umeleta mapambio ya kisiasa tu apa , ii nci ina mawaziri ao kwa zaidi ya miaka 60 ila bado ipo kati ya nci 10 maskini zaidi duniani.

Nakushauri achana na wanasiasa tena hizo siasa zako za upambe eti MAGUFULI4LIFE (utakuwa mpuudhi sana wewe halafu)
hawana mpango na wewe zaidi ya kukutumia na kukudanganya, fanya kazi kwa bidii wewe binafsi, jitume ili upate maendeleo na upunguze maumivu ya maisha na kuongeza furaha kwako na familia yako.

Usimtegemee mwanasiasa akuletee maendeleo tena awa ambao wapo madarakani tokea nchi ipate uuru, hao wapo kwa maslahi yao binafsi na sio kwa maslai yako na taifa.

usiponielewa utaendelea kuwa maskini wewe na kizazi chako chote , amka acha kuwa mpambe wa wanasiasa
Dhumuni letu kubwa ni kuijenga Tanzania moja. Ukishindwa kujadiliana unaweza ukakaa kimya tu.



MAGUFULI4LIFE.
 
Dhumuni letu kubwa ni kuijenga Tanzania moja. Ukishindwa kujadiliana unaweza ukakaa kimya tu.



MAGUFULI4LIFE.
hakuna haja ya kujadili kitu ambacho hakiwezekani kupitia hao uliowataja na genge lao la wahuni,
unaleta blabla zako za kipuudhi eti Tanzania sio nci maskini, nimekupatia source uone tulipo kidunia kutokana natafiti za mangnuli wa ucumi duniani .
siwezi kukaa kimya nikiona wapuudhi, washenzi na wazindiki kama wewe unatoa posti za kupotosha na za kipuudi
acha kutumika vibaya mpuudhi mkubwa wee na msenzx
 
hakuna haja ya kujadili kitu ambacho hakiwezekani kupitia hao uliowataja na genge lao la wahuni,
unaleta blabla zako za kipuudhi eti Tanzania sio nci maskini, nimekupatia source uone tulipo kidunia kutokana natafiti za mangnuli wa ucumi duniani .
siwezi kukaa kimya nikiona wapuudhi, washenzi na wazindiki kama wewe unatoa posti za kupotosha na za kipuudi
acha kutumika vibaya mpuudhi mkubwa wee na msenzx
Kwa 👆👆👆 basi kutumika vizuri hakufai na ni tusi kwa mtu yeyote ambaye anajiheshimu. Ila umeuvamia uwanja.


MAGUFULI4LIFE.
 
Unategemea mwanasiasa akutatulie changamoto zako mkuu.
Mwl. Nyerere alisema
Wanasiasa wote wa nyakati hizi ni malaya malaya tu.
Ajira sahivi labda utokee muujiza tu mkuu lakini sio hao wanawake -
 
Kubadili mfumo siyo kitu rahisi, unahitaji watu kama Dkt Magufuli. Kama wanapita hapa jukwaani wasome ujumbe wako na huu wangu, yaani wawe na akili na uelewa wa Dkt Magufuli ili waweze kuwa wabunifu kwenye wizara zao.
 
Back
Top Bottom