Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,413
- 23,592
Katika hali ya kuonyesha kuwa uongozi wa CCM hauheshimu Katiba wala Utawala wa sheria, umetoa ifuatayo kama taarifa rasmi ya vikao vyake vya Dodoma:-
Katiba inaendelea vile vile kumlazimisha Mbunge kula kiapo cha uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za Bunge. Katiba hiyo hiyo inatoa uhuru kwa mawazo, majadiliano na utaratibu katika bunge na huo uhuru hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika mahakama au mahali pengine popote nje ya Bunge.
Ni katiba ndio imewezesha uwepo wa CCM na vyama vingine vya siasa na pamoja na CCM kuwa na utaratibu wake wa kichama, kama itatokea taratibu hizo zikapingana na katiba, zinakuwa batili. CCM kama hairidhiki na uendeshaji ndani ya Bunge inaweza kuitumia kamati ya wabunge wa CCM kuwasilisha hoja bungeni.
Kwa CCM kuunda kamati nje ya Bunge eti kuangalia masuala ya uendeshaji wa shughuli za Bunge, imezidi kukiuka katiba ya nchi na adhabu yake ni kupoteza sifa kama chama cha siasa kulingana na sheria kama zilivyotungwa na bunge hilo hilo na yafaa ifutwe kwenye daftari la msajili wa vyama.
Kamati ya Mwinyi Rais Mstaafu, Msekwa Makamu Mwenyekiti CCM (Bara) na Ndugu Abdulhaman Kinana kama zitatekeleza majukumu waliyopewa watakuwa wanafanya makosa ya jinai - waitwe na wahojiwe na Bunge. Taifa haliwezi kuendelea kuongozwa kihuni bila kufuata sheria na taratibu kama katiba inavyoagiza.
Katiba ya Tanzania inatambua Serikali, Bunge na Mahakama kama mihimili mikuu ya dola na kulipa Bunge madaraka kwa niaba ya wananchi wote kuisimamia na kuishauri serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii.Kwa kutambua kuwepo matatizo ya matamshi na vitendo visivyoridhisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Baraza la Wawakilishi, Halmashauri Kuu ya Taifa imeamua kuunda Kamati Ndogo ya kutafuta undani wa matatizo hayo na kupendekeza kwa Kamati Kuu njia za kuyatatua. Aidha, Kamati hiyo pia itaangalia utendaji kazi wa Kamati za Chama katika Bunge na Baraza la Wawakilishi kwa nia ya kubaini upungufu uliopo ili kupendekeza kwa Kamati Kuu kuhusu njia za kurekebisha. Pia, Kamati itaangalia masuala ya uendeshaji wa shughuli za Bunge na Baraza la Wawakilishi na kushauri namna ya kuimarisha, pale panapostahili.
Kamati hiyo itaongozwa na Mzee Alli Hassan Mwinyi Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Wajumbe wengine ni Mzee Pius Msekwa Makamu Mwenyekiti CCM (Bara) na Ndugu Abdulhaman Kinana.
Katiba inaendelea vile vile kumlazimisha Mbunge kula kiapo cha uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za Bunge. Katiba hiyo hiyo inatoa uhuru kwa mawazo, majadiliano na utaratibu katika bunge na huo uhuru hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika mahakama au mahali pengine popote nje ya Bunge.
Ni katiba ndio imewezesha uwepo wa CCM na vyama vingine vya siasa na pamoja na CCM kuwa na utaratibu wake wa kichama, kama itatokea taratibu hizo zikapingana na katiba, zinakuwa batili. CCM kama hairidhiki na uendeshaji ndani ya Bunge inaweza kuitumia kamati ya wabunge wa CCM kuwasilisha hoja bungeni.
Kwa CCM kuunda kamati nje ya Bunge eti kuangalia masuala ya uendeshaji wa shughuli za Bunge, imezidi kukiuka katiba ya nchi na adhabu yake ni kupoteza sifa kama chama cha siasa kulingana na sheria kama zilivyotungwa na bunge hilo hilo na yafaa ifutwe kwenye daftari la msajili wa vyama.
Kamati ya Mwinyi Rais Mstaafu, Msekwa Makamu Mwenyekiti CCM (Bara) na Ndugu Abdulhaman Kinana kama zitatekeleza majukumu waliyopewa watakuwa wanafanya makosa ya jinai - waitwe na wahojiwe na Bunge. Taifa haliwezi kuendelea kuongozwa kihuni bila kufuata sheria na taratibu kama katiba inavyoagiza.