Kwa kauli zinazotolewa dhidi ya Hayati Magufuli ni wazi kuna wenye wivu na aliyofanya kwa miaka 6 ya utawala wake

Kwa kauli zinazotolewa dhidi ya Hayati Magufuli ni wazi kuna wenye wivu na aliyofanya kwa miaka 6 ya utawala wake

Manelezu

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2015
Posts
1,908
Reaction score
2,774
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri. Nimekuwa nikifuatilia kauli mbalimbali zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa dhidi ya hayati Magufuli. Ni wazi kabisa kuna chuki kubwa dhibi yake. Na ukichunguza kwa undani zaidi utaona wanataka kupandikiza hiyo chuki hata kwa wananchi wa kawaida.

Ukweli ni kwamba wananchi wengi wa kawaida hawawezi mchukia magufuli, utamchukiaje kiongozi aliyejenga zahanati nchi nzima? Shule, madaraja, Barabara? Viwanja vya ndege? Shule? Miradi mikubwa ya umeme? Kujenga makao makuu ya Dodoma kwa kiwango kile tena kwa muda mfupi? Treni ya mwendo kasi?

Kichaa anawezaje kufanya yote haya? Haya tuonyesheni hao wengine wamefanya nini katika miaka 10?

Ujambazi, mauaji ya albino yaliisha, umeme kukatika kulikoma, kichaa anawezaje kufanya yote haya?

Mungu atatuhukumu siku moja, na hakika tutahukumiwa kwa matendo yetu.

Lazima Magufuli achukiwe na matajiri na wanasiasa. Utawezaje tetea masikini huku ukifurahisha matajiri? Haipo hata siku moja.

Ukiniuliza leo viongozi waliolifanyia makubwa taifa hili toka liwepo list yangu iko hivi

1. Julius Nyerere
2. John P. Magufuli
3. Benjamin Mkapa
4. Ally Hassan Mwinyi
5 Jakaya Kikwete

Mama Samia sijamuweka sababu bado yupo madarakani. Anaweza kuwa wa Kwanza au wa mwisho inategemea atalifanyia nini taifa hili.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Hata wakimchukia JPM haitasaidia kitu, yeye amepumzika na mtoa hukumu ni mmoja tu nae hukumu zake ni za haki.
Exactly, yule Mzee kwa yale aliyowafanyia masikini wa taifa hili na kuwa tetea, yeye aliye Juu sana atamkumbuka. Watu walivyomlilia kiasi kile naamini kilio chao kimefika sehemu husika.
 
Mika sita ya taabu. sana kwa watanzania, kawastaafisha siasa manguli woote wa siasa including wanaCCM.

Acha akaongoze malaika huko
Acha uvivu chief

Lakini hata hivyo, hayupo sasa, ni vyema tukaonyesha uwezo mara tano zaidi yake ili aendelee kupuuzwa zaidi
 
Una chuki na Kikwete.
Kama ulinunua Kiwanja Chato, niuzie aisee, kabla hakijageuka pori, Nina shilingi 70,000/- taslimu
Kwanini nimchukie kikwete, yani moyo wangu ni msafi mno. Sina chuki na kiongozi yoyote yule. Nimetoa maoni yangu na wewe toa yako.

Kikwete ana yake mazuri na mabaya vile vile. Ndio maana sijamuweka Rais Samia sababu najua utawala wake ndio umeanza.
 
Kumpuuza Dr JPM ni kujibu mambo kwa matendo zaidi, la sivyo ni wivu tu unaowasumbua baadhi ya watu.

Kama kuna miradi ilikuwa ikisuasua wakati wake, sasa twende kwa kasi zaidi, biashara vilevile, pesa kuwa nyingi mitaani nayo iwe hivyo, wawekezaji, bidhaa kushuka zaidi ya ilivyokuwa, wafanyakazi waongezwe mishahara n.k, hapo tutampuuza kwa wepesi,
Vinginevyo,

tusipofanya hivyo, ni vyema tukamwacha jemedari huyu apumzike, na watanzania mlivyo, mnamnanga kwenye vitu ambavyo yeye mwenyewe kazifanya, kujinyima kwake kwa ajili ya nchi yetu, imekuwa nongwa

Aligoma kabisa kutumia mabilioni kwa ajiri ya safari za nje ili ziongezwe kwenye miradi mikubwa, na sasa hatupo, miradi hakuondoka nayo, ipo kwa ajiri yetu,

Tusipofanya zaidi yake, Tutakuwa wanafiki tusio na maana

Embu tumwacheni bana
 
Kaburu Pieter Botha wa Afrika kusini alifanya mara elfu ya Magufuli huko Afrika kusini, nenda kawaulize weusi wa nchi ile wanampenda kwa kiasi gani. Hivi mnadhani hatujui ukweli au mnadhani tumelala sana?
Magufuli hakuwa kaburu.
 
Mleta uzi utajisikiaje siku ya hukumu itakapofika unamkuta jiwe ni nyapara wa wale wanao enda kuchomoa kwenye kaa la moto. Kila mtu aplay part yake, Mana wanadamu wote tunamapungufu
 
Kaburu Pieter Botha wa Afrika kusini alifanya mara elfu ya Magufuli huko Afrika kusini, nenda kawaulize weusi wa nchi ile wanampenda kwa kiasi gani. Hivi mnadhani hatujui ukweli au mnadhani tumelala sana?
Hakuna cha maana alichofanya zaidi ya maigizo
 
Mwendazake aliwahi sema kuwa kamchagua mpina kichaa mwenzie
 
Back
Top Bottom