Kwa kesi hii ya ugaidi ya akina Mbowe: Je, Kitengo cha propaganda ndani ya Serikali wamefaulu au wamefeli?

Kwa kesi hii ya ugaidi ya akina Mbowe: Je, Kitengo cha propaganda ndani ya Serikali wamefaulu au wamefeli?

Namichiga

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2017
Posts
356
Reaction score
526
Ndugu wana jukwaa, kwenye kichwa cha habari hilo ni swali, hivyo katika kutoa hoja naomba kwanza tutangulize kwanza kujibu na baadae ndio zifuatie hoja za uchambuzi.

Katika maswala mazima ya mifumo ya kiutawala katika nchi za Kiafrika, hili neno la propanda linapewa kipaumbele kikubwa pindi inapojitokeza mihemko ya jamii ya watawaliwa, na idara maalum zinazohusika na mipango hii ya propaganda hukaa chini na kuibua jambo litakalokuwa midomoni mwa wananchi na kwenye vyombo vyote vya habari kwa wakati huo, dhamira kuu ni kuiacha serikali ipumue dhidi ya masimango na maneno kutoka kwenye jamii kwa wakati huo!

Nije kwenye kiini cha mada,kwa mtazamo wangu mimi, hili swala la serikali kumtia nguvuni mwenyekiti wa Chadema Bw. Mbowe na kumpandisha kizimbani na watuhumiwa wengine katika makosa ya ugaidi, serikali kwa ujumla imejaribu kuhamisha goli ili wanaoshambulia wakose muelekeo.

Sote tunajua, baada ya kukamata usukani wa madaraka Rais Samia, kipaumbele chake chake cha kwanza mkononi kilikua ni kuirudisha Tanzania kwenye nafasi yake katika ramani ya Kidemokrasia ulimwenguni.Na matamshi yake akauthibitishia ulimwengu kwamba yale mambo yote yasiyokuwa ya kiungwana katika utawala wake hayatakuwepo.

Hapa sasa,kiujumla hadi mwenda zake anatangulia mbele ya haki, uwanja wa demokrasia nchini ulishajaa tope na vyama vya upinzani vilikua hoi bin taabani.Miongoni mwetu watanzania wa kawaida hakuna asie fahamu hilo.

Hivyo basi upinzani upinzani ukajaribu kusuka ajenda kuu itayowapa kick ili kutembelea nyota ya Samia na kurudisha umaruufu wao uliopokonywa kwa mabavu, na katika kuzichanga karata zao wakaona ajenda namba moja ni katiba mpya.

Wakaanza kuliamsha dude nchi nzima tena kwa spidi kubwa huku wakijaribu kuwatumia hadi watu mbalimbali wenye ushawishi kwa jamii ili kupata attention. Na serikali kadri ilivyojaribu kutumia maneno ya hekima na busara ili waachane na jambo hilo,ndio kwanza wakazidi kupata kick.

Hapo ndio serikali ikaamua kuwakabidhi jukumu watu wa kitengo ili kuhamisha goli la mjadala huo waliokuwa nao wapinzani.

Na watu wakainama, wakainuka na wakaamua kufukua makaburi kwa kuirudisha tena ubaoni kesi ya ugaidi ambayo kwa maneno ya ndani inasemekana, walishaichumbua na kujiridhisha kwamba haina ukweli.

Na baada ya Bw. Mbowe kupandishwa kizimbani hatimaye lengo lao limetimia kwani upande wote wa upinzani umeshatawanyika na wanahaha na kesi ya mwenyekiti.
 
Siku zote epuka kutengeneza propaganda which can be proved.

Tena kuwa makini ikiwa proved isikurudie wewe...
Binafsi hakuna propaganda ninazoziogopa kama zinazoweza kuleta madhara kwa umma siku za mbeleni

Mfano propaganda ya #Babu wa Loliondo, ilifumwa ili kuinusuru serikali ya wakati huo kwenye makashfa ya Richmond na EPA yaliyokuwa yametanda anga zima la siasa za Tanzania.

Lakini matokea tuliyaona, serikali ilifanikiwa kuhamisha goli lakini mamia ya wananchi wakapoteza uhai kwa kuamini dawa isiyokuwa na uthibisho wa kikemia na kuacha matibabu yao.
 
Dr.Slaa hata akiongea usimsikize kwa umakini,kwani yeye mwenyewe alishawahi kutumiwa kimkakati na wapishi wa propaganda kule kitengo!!!.
Na kwa sasa amejaa kila sehemu, kwenyeTBC na hata online media, anasema yeye ni mtu wa principles, sijui ni principles zipi alizotumia kuukacha upadri wake, mke wake (Rose), CDM na mazagazaga mengineyo, ni kama vile yeye ni Malaika humu duniani ni principle tupu.
 
Hii kesi inampaisha zaidi MBOWE pia inamfitinisha zaidi SASHA na wananchi.

SASHA alijinasubu anakuja kuponya taifa, akamuajiri na Tony Blair aje asafishe taswira ya nchi iliyokuwa imehaeibiwa na mwendazake, wakati naye pia anafanya yakeyale

Mikutano ya vyama vya upinzani hairuhusiwi huku CCM wako wakifanyanya mikutano yao bill bugudha.

Kesi ya MBOWE NI ya kubumba na tunaona kabisa mwenendo wake jinsi jaji anavyopendelea upande mmoja.

Sasa Mungu anampiga SASHA. Kila kitu kinapanda Bei, nchi inakuwa ngumu zaidi.

Biblia inasema HAKI HUINUA TAIFA. Hutendi Hali taifa linaporomoka kila uchao.

Hii kesi itufumbue fikra zetu na macho pia ya rohoni
 
Hii kesi inampaisha zaidi MBOWE pia inamfitinisha zaidi SASHA na wananchi. SASHA alijinasubu anakuja kuponya taifa, akamuajiri na Tony Blair aje asafishe taswira ya nchi iliyokuwa imehaeibiwa na mwendazake...
Nifikiriavyo mimi ameamua kumfedhehesha mbowe kwa inferiority aliyonayo ktk uchaguzi ujao, imagine hata jaji anashindwa kuficha mahaba yake juu ya upande wa mashtaka.

Chief hangaya ana roho mbaya sana ugaidi wa kufadhiliwa na laki na nusu, mara laki mbili! Na bastola moja yenye risasi tatu! Bastola ambayo mama mbege anaielezea kuifahamh vizuri utafikiri anaimiliki!
 
Na kwa sasa amejaa kila sehemu , kwenyeTBC na hata online media, anasema yeye ni mtu wa principles, sijui ni principles zipi alizotumia kuukacha upadri wake, mke wake (Rose), CDM na mazagazaga mengineyo, ni kama vile yeye ni Malaika humu duniani... ni principle tupu.
Lowasa anakuja chadema ni asset au liability ....hapo ndipo aliamua kusimamia analolijua Hadi Leo kwakweli mhuuuu
 
Lkn kwny upadri alishindwa kusimama anachoamini baada ya kuona mbunye ni tamu sio?
Cdm kwenye bandiko nililojibu ni kifupi Cha nn imemanishwa ,unamshangaa padri slaa badala umshangae Martin Luther senior au papa Benedict x na 6.....
 
Cdm kwenye bandiko nililojibu ni kifupi Cha nn imemanishwa ,unamshangaa padri slaa badala umshangae Martin Luther senior au papa Benedict x na 6.....
Kwa hio Benedict x na Martin Luther ndio walichanganywa na mbunye ya huyo rose?
 
Siku zote epuka kutengeneza propaganda which can be proved.

Tena kuwa makini ikiwa proved isikurudie wewe.

Ndicho kinachotokea sasa kwenye hii kesi.

Ngoma imebackfire, bamutu batalokota kinyavu vere vere soon.
hatari sn
 
Ndugu wana jukwaa,kwenye kichwa cha habari hilo ni swali,hivyo katika kutoa hoja naomba kwanza tutangulize kwanza kujibu na baadae ndio zifuatie hoja za uchambuzi...
Kumbe kazi ya TISS ni kufanya Propaganda? Yawezekana basi hata CIA nao kazi yao Kubwa huko Marekani ni Kufanya tu Propaganda.

Kazi kweli kweli.....!!
 
Back
Top Bottom