Kwa lawama anazopewa Hayati Magufuli na Antony Diallo wa Sahara Media ni wazi CCM ya 2015 - 2021 ina Dhambi za Dhuluma

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kama muda huu unatizama 'Mubashara' Star Tv Mahojiano ya Mmiliki wa Sahara Media na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Tajiri Antony Dialo huhitaji Elimu Kubwa kujua ya kwamba 'ameteseka' sana na 'kudharauliwa' mno na uliokuwa Utawala wa Hayati Rais Dkt. Magufuli na CCM yake.

Na 99% ya Mazungumzo yake Tajiri Antony Dialo wa Sahara Media ( Wamiliki wa Vyombo vya Habari vikubwa Kanda ya Ziwa na nchini ) vya Star Tv, Radio Free Afrika na Kiss FM anaelezea jinsi Hayati Rais Dkt. Magufuli alivyomtumia ipasavyo katika Kampeni zake za mwaka 2015 na alipoupata Urais akasahauliwa, hakulipwa Pesa zake hadi leo na kujikuta hata akidharaulika ndani ya CCM.

" Hakuna Vyombo vya Habari ambavyo vilifanya Kazi Kubwa ya Kumkapenia Hayati Rais Dkt. Magufuli kama vyangu na nakumbuka mara Mbili tena akiwa Jukwaani Hayati aliahidi Kukusaidia kwa Kutuinua zaidi Sahara Media ila nikashangaa amenisahau, amenitupa huku nikiwa nimeingia Hasara kubwa na Kushindwa kujiendesha mpaka Wafanyakazi wangu wakawa wananidai na wengine kunikimbia na mpaka hii leo nadai Pesa zangu nyingi tu za Malipo yangu kwa Kazi niliyomfanyia "

Hata hivyo pamoja na Tajiri Antony Dialo ( wa Sahara Media ) Kuonekana kuwa na Masikitiko mengi juu ya yote yaliyomtokea Jicho Kali la Kisaikolojia la GENTAMYCINE limenionyesha kuwa kwa 'body language' yake Runingani ni kama vile anaifurahia Kazi yake Israeli kwa Mdaiwa wake Sugu na kwamba hata kama asipolipwa Poa tu barida na haina noma.

Tafadhali CCM ya Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan nawe ( nanyi ) msije kurudia hili Kosa ya Kuvitumia baadhi ya Vyombo vya Habari ipasavyo wakati wa Kampeni zenu kama Condoms na baada ya Shughuli yenu Muhimu na Tamu Kukamilika mnawasahau / mnawatupa.

Kwani kwa Kufanya hivi Kwao huenda mkawa mnajilimbikizia tu Dhambi na Laana ya Mwenyezi Mungu ambae nae pia bila ajizi anamuagiza Mtekelezaji wake wa Kutukuka Israeli afanye yake kama ya 17 Machi, 2021 Wodini Mzena Makumbusho Wilayani Kinondoni Mkoani Dar es Salaam nchini Tanzania.
 
Huwa napenda sana kusoma post zako! Na huwa kuna vitu najifunza sana kupitia wewe gentamycine. Ila naomba nikuambie kwa post yako ya leo umeenda sana wrong na umeiyandika kiuchochezi.

Kuwa makini sana kiongozi kwa post zako . Watu wataanza kukuzarau kwa post zako!

Kama yule mwamba pascal ambaye alikuwa anaeshimika sana hapa Jamii forum! Lkn cku hizi anazaraulika. Hii ni kutokana na tabia kama hizi unazotaka kuzianzisha wewe.

Achana na hizi tabia jombaa. Simamia maadili yako
 
Magufuli kama akukugusa basi wewe ulikuwa ni labda kijakazi wake

Ila naamini hata vijakazi wake walitukanwa na kudhalilishwa kwa kula bure pale ikulu

Mama Janeth kanenepa kweli nimependa na tabasamu limerudi

Mungu amlaze panapostahili huyu dicteta alinipa machungu sana huyu jamaa!!
 
Mkuu nimewasilisha 'Mawaidha' ya Tajiri wa Sahara Media na Mwenyekiti wa CCM Mkoani Mwanza Antony Dialo aliyotoka Kuyasema muda si mrefu Star Tv katika Mahojiano yake je, tatizo la GENTAMYCINE lililokukwaza ni nini? Nasubiri mrejesho wako upesi.

Cc: mwengeso
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…