Kwa makusanyo yaliyopatikana kupitia ofisi ya DPP ni dhahiri Wapinzani muache kupinga kila jambo

Kwa makusanyo yaliyopatikana kupitia ofisi ya DPP ni dhahiri Wapinzani muache kupinga kila jambo

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Wanabodi hapa JF ninyi ni mashahidi jinsi wapinzani Tanzania walivyopinga utaratibu wa kisheria wa mtuhumiwa wa baadhi ya makosa ya jinai hasa uhujumu uchumi kuingia mkataba na DPP ili kukiri kisha kulipa na kurejesha walichokuwa wamewaponza watanzania.

Utaratibu huu ulipata baraka za Bunge la Tanzania. Kifungu cha 194 cha CPA kilifanyiwa marekebisho,na mtuhiwa wa makosa hasa jinai anaweza kuingia makubaliano na Dpp kisha kulipa kile acho hujumu.

Nia hasa ya kuleta huu utaratibu ni kuwezesha kesi kuisha kwa uharaka na kupunguza msongamano wa mahabusu gerezani. Lakini jambo ambalo wapinzani wa hapa Tanzania walikengeuka na kuanza kueneza uongo kuwa huu utaratibu umewekwa ili kumnufaisha DPP.

Maneno na porojo nyingi zimetangazwa hapa Tanzania. Mara DPP amepewa mtaji wa kujinuisha,mara huu utaratibu wa kisheria umewekwa kuwakamua wapinzani na wakosoaji wa serikali iliyipo madarakani.

Leo hii kuna gazeti la hapa Tanzania limetoa takwimu kuwa Bil 123.6 zimekusanywa kupitia ofisi ya DPP. Hii ni habari njema sababu pesa hizi zimekusanywa kwa mujibu wa sheria. Na nia kuu ni kuhakikisha waliofanya makosa hawakai rumande muda mrefu,huku magereza yakipumua maana mrundikano wa wafungwa na mahabusu ni mkubwa.

Oni langu, wapinzani msiwe mnakurupuka kupinga kila kitu kisa tu mnatafuta kick kwa wanachi.
 
Unapokusanya pesa kwa sheria kandamizi kisha ukatokea na kusifia huo ukandamizaji, huo ni upunguani. Sio kwamba hatujui mazingira ya ukandamizaji na vitisho yanayopelekea watu kukiri huo ukandamizaji.
 
Unapokusanya pesa kwa sheria kandamizi kisha ukatokea na kusifia huo ukandamizaji, huo ni upunguani. Sio kwamba hatujui mazingira ya ukandamizaji na vitisho yanayopelekea watu kukiri huo ukandamizaji.
Hii kitu ilipita bungeni,wabunge wakapitisha. Unaposema sheria kandamizi una maana gani? Hakuna mtuhumiwa anayelazimishwa kufanya plea bargaining.
 
Uporaji na ukusanyaji ni vitu viwili.
Kupora ni mtuhumiwa kulazimishwa kununua Uhuru wako kwa kukaa mezani uwape chao
 
Mbona hilo bunge halibadilishi sheria ili kina MGUFULI warudishe nyumba za umma warudishe nyumba za umma walizowauzia mahawala zao ????
Hii kitu ilipita bungeni,wabunge wakapitisha. Unaposema sheria kandamizi una maana gani? Hakuna mtuhumiwa anayelazimishwa kufanya plea bargaining.
Changu,acha kujifanya zezeta,
Kina Rugemalila ni mwaka wa ngapi wako jera na upelepezi haujakamilika hadi kesho,na walilazimishwa wakili ili wawapole pesa zao kwa njia ya DPP,lakini walikataa,
Je Kama walitenda makosa ,mbona upeleleIezi haujakamilika hadi leo?
Je Rugemarila na Seth wangekuwa waoga huoni wangekuwa wameibiwa pesa zao kupitia DPP au Kama walivyopolwa wenye maduka ya kubadilishia fedha?
 
Changu,acha kujifanya zezeta,
Kina Rugemalila ni mwaka wa ngapi wako jera na upelepezi haujakamilika hadi kesho,na walilazimishwa wakili ili wawapole pesa zao kwa njia ya DPP,lakini walikataa,
Je Kama walitenda makosa ,mbona upeleleIezi haujakamilika hadi leo?
Je Rugemarila na Seth wangekuwa waoga huoni wangekuwa wameibiwa pesa zao kupitia DPP au Kama walivyopolwa wenye maduka ya kubadilishia fedha?
🖕
 
Mbona hilo bunge halibadilishi sheria ili kina MGUFULI warudishe nyumba za umma warudishe nyumba za umma walizowauzia mahawala zao ????
Kwenye hili la nyumba serikali inaweza pata pesa nyingi Sana,maana ule ni uhujumu uchumi.Uhujumu uchumi sio kuiba pesa zetu bali ikiwemo na matumizi mabaya ya raslimali zetu ikiwemo uuzwaji wa nyumba za serikali kwa thamani ya bei ya kiwanja kijijini tena kwa mkopo
 
Kwenye hili la nyumba serikali inaweza pata pesa nyingi Sana,maana ule ni uhujumu uchumi.Uhujumu uchumi sio kuiba pesa zetu bali ikiwemo na matumizi mabaya ya raslimali zetu ikiwemo uuzwaji wa nyumba za serikali kwa thamani ya bei ya kiwanja kijijini tena kwa mkopo
Duh..!
 
Wanabodi hapa JF ninyi ni mashahidi jinsi wapinzani hapa Tanzania walivyopinga utaratibu wa kisheria wa mtuhumiwa wa baadhi ya makosa ya jinai hasa uhujumu uchumi kuingia mkataba na Dpp ili kukiri kisha kulipa na kurejesha walichokuwa wamewaponza watanzania.

Utaratibu huu ulipata baraka za bunge la Tanzania. Kifungu cha 194 cha CPA kilifanyiwa marekebisho,na mtuhiwa wa makosa hasa jinai anaweza kuingia makubaliano na Dpp kisha kulipa kile acho hujumu.

Nia hasa ya kuleta huu utaratibu ni kuwezesha kesi kuisha kwa uharaka na kupunguza msongamano wa mahabusu gerezani. Lakini jambo ambalo wapinzani wa hapa Tanzania walikengeuka na kuanza kueneza uongo kuwa huu utaratibu umewekwa ili kumnufaisha Dpp.

Maneno na porojo nyingi zimetangazwa hapa Tanzania. Mara Dpp amepewq mtaji wa kujinuisha,mara huu utaratibu wa kisheria umewekwa kuwakamua wapinzani na wakosoaji wa serikali iliyipo madarakani.

Leo hii kuna gazeti la hapa Tanzania limetoa takwimu kuwa Bil 123.6 zimekusanywa kupitia ofisi ya Dpp. Hii ni habari njema sababu pesa hizi zimekusanywa kwa mujibu wa sheria. Na nia kuu ni kuhakikisha waliofanya makosa hawakai rumande muda mrefu,huku magereza yakipumua maana mrundikano wa wafungwa na mahabusu ni mkubwa.

Oni langu, wapinzani msiwe mnakurupuka kupinga kila kitu kisa tu mnatafuta kick kwa wanachi .
Mbona inaonekana mkurupukaji ni wewe.

Usiangalie tu upatikanaji wa hela. Hata jambazi huua, hupora, na kisha hupata hela. Na anaweza kuitumia pesa hiyo kuchangia arusi na kwenye misiba.

Asilimia kubwa ya hawa waliotoa hiyo pesa, wameporwa. Wamekubali kununua uhuru wao kutokana na kushindwa kuhimili maisha ya mateso yaliyopo magerezani. Wengi wamesoteshwa mahabusu za magerezani kwa zaidi ya mwaka mzima ili kuwalazimisha wakubali.

Walitengenezwa makosa, wakasoteshwa mahabusu kwa muda mrefu, DPP alikosa uthibitisho wa kuwatia hatiani kwa mujibu wa sheria. Wamelazimika kulipa ili wawe huru, wakaungane na familia zao. Na Jiwe alisema watakaokataa kukiri na kutoa pesa, wasoteshwe mahabusu bila huruma!!

Kufurahia unyama ni kushiriki ushetani. Mungu wa haki, asimame na wale walionewa, na awalipie kisasi kwa aliyewaonea. Waliokuwa na makosa, hao ni haki yao kulipia makosa waliyoyafanya. Lakini tunajua kuwa wengi wao wameonewa, ndiyo maana DPP alishindwa kuwasilisha ushahidi mahakamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuanze na nyumba za serikali thamani ya zilivyouziwa hazilingani na thamani halisi ya maeneo husika ni ufisadi Mkubwa sana umetumika pale. Tunaomba yeyeto atakaeshika madaraka haijalishi ni lini arudishe nyumba zote hizi ziliuzwa kihuni, atumie sheria ya utaifishaji. Kama kuna aliyeziendeleza ile kwake abebe jengo lake atuachie nyumba zetu.
 
Mbona inaonekana mkurupukaji ni wewe.

Usiangalie tu upatikanaji wa hela. Hata jambazi huua, hupora, na kisha hupata hela. Na anaweza kuitumia pesa hiyo kuchangia arusi na kwenye misiba.

Asilimia kubwa ya hawa waliotoa hiyo pesa, wameporwa. Wamekubali kununua uhuru wao kutokana na kushindwa kuhimili maisha ya mateso yaliyopo magerezani. Wengi wamesoteshwa mahabusu za magerezani kwa zaidi ya mwaka mzima ili kuwalazimisha wakubali.

Walitengenezwa makosa, wakasoteshwa mahabusu kwa muda mrefu, DPP alikosa uthibitisho wa kuwatia hatiani kwa mujibu wa sheria. Wamelazimika kulipa ili wawe huru, wakaungane na familia zao. Na Jiwe alisema watakaokataa kukiri na kutoa pesa, wasoteshwe mahabusu bila huruma!!

Kufurahia unyama ni kushiriki ushetani. Mungu wa haki, asimame na wale walionewa, na awalipie kisasi kwa aliyewaonea. Waliokuwa na makosa, hao ni haki yao kulipia makosa waliyoyafanya. Lakini tunajua kuwa wengi wao wameonewa, ndiyo maana DPP alishindwa kuwasilisha ushahidi mahakamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
None sense.
 
Unapokusanya pesa kwa sheria kandamizi kisha ukatokea na kusifia huo ukandamizaji, huo ni upunguani. Sio kwamba hatujui mazingira ya ukandamizaji na vitisho yanayopelekea watu kukiri huo ukandamizaji.

Unaongea nini Mkuu? Plea guilty unaijua au huijui? Mtu amekiri kosa na akawa tayari kulipa faini kwa DPP shida iko wapi? Kama anaona kulipa faini anaonewa asubiri aende mahakamani. Nchi ilikuwa shamba la bibi hii. Kuna muda namkubali JPM sana, kuna wakati tajiri alikuwa na uwezo wa kufanya chochote na hakuna wa kuhoji.
 
Unapokusanya pesa kwa sheria kandamizi kisha ukatokea na kusifia huo ukandamizaji, huo ni upunguani. Sio kwamba hatujui mazingira ya ukandamizaji na vitisho yanayopelekea watu kukiri huo ukandamizaji.
Mwambie mbowe nae akiri arudishe pesa za wabunge na ruzuku alizokula mambo yaishe.
 
Unaongea nini Mkuu? Plea guilty unaijua au huijui? Mtu amekiri kosa na akawa tayari kulipa faini kwa DPP shida iko wapi? Kama anaona kulipa faini anaonewa asubiri aende mahakamani. Nchi ilikuwa shamba la bibi hii. Kuna muda namkubali JPM sana, kuna wakati tajiri alikuwa na uwezo wa kufanya chochote na hakuna wa kuhoji.
Nashukuru,umempa makavu.
 
Wanabodi hapa JF ninyi ni mashahidi jinsi wapinzani hapa Tanzania walivyopinga utaratibu wa kisheria wa mtuhumiwa wa baadhi ya makosa ya jinai hasa uhujumu uchumi kuingia mkataba na Dpp ili kukiri kisha kulipa na kurejesha walichokuwa wamewaponza watanzania.

Utaratibu huu ulipata baraka za bunge la Tanzania. Kifungu cha 194 cha CPA kilifanyiwa marekebisho,na mtuhiwa wa makosa hasa jinai anaweza kuingia makubaliano na Dpp kisha kulipa kile acho hujumu.

Nia hasa ya kuleta huu utaratibu ni kuwezesha kesi kuisha kwa uharaka na kupunguza msongamano wa mahabusu gerezani. Lakini jambo ambalo wapinzani wa hapa Tanzania walikengeuka na kuanza kueneza uongo kuwa huu utaratibu umewekwa ili kumnufaisha Dpp.

Maneno na porojo nyingi zimetangazwa hapa Tanzania. Mara Dpp amepewq mtaji wa kujinuisha,mara huu utaratibu wa kisheria umewekwa kuwakamua wapinzani na wakosoaji wa serikali iliyipo madarakani.

Leo hii kuna gazeti la hapa Tanzania limetoa takwimu kuwa Bil 123.6 zimekusanywa kupitia ofisi ya Dpp. Hii ni habari njema sababu pesa hizi zimekusanywa kwa mujibu wa sheria. Na nia kuu ni kuhakikisha waliofanya makosa hawakai rumande muda mrefu,huku magereza yakipumua maana mrundikano wa wafungwa na mahabusu ni mkubwa.

Oni langu, wapinzani msiwe mnakurupuka kupinga kila kitu kisa tu mnatafuta kick kwa wanachi .
Ukishafanya ofisi ya DPP kuwa ninofisi ya kujusanya mapato, mfumo wako wa haki una matatizo makubwa sana.
 
Back
Top Bottom