Mkuu, na picha za 2015 zinahusikaje hapa tena?
Tuongezeni juhudi ya Kampeni na kuhamasisha watu ili tuondokane na aibu ya kutumua picha na video za nyomi ya Lowasa
Huu ndio ukweli, kwa watu waonao mbali.Wengi washangaaji tu, Lissu uwezo wa kuongoza nchi hana, CHADEMA ni dhahifu sana na ikitokea siku wakaongoza watakuwa mafisadi wakubwa sana, walionesha madhaufu yao makubwa sana 2015
Nafurahi kwa kuwa umekubaliana na mimi kwamba hakuna demokrasia nchini,kwa kisingizio kuwa ni mpango wa mataifa ya magharibi. Kama ndivyo hatuna haja ya kufanya maigizo haya ya uwepo wa vyama vingi vya siasa kama ninyi mnaamini kuwa demokrasia inaleta umaskini.Siasa zilizuiwa ili watu wajikite katika kuendeleza maeneo yao, wajikite katika kuufikiria umaskini wao na kutatua shida zao badala ya mwaka mzima kuwa wa mikutano majukwaani wakati ambao ni wa kutumika kufanya kazi.
Siasa za mwaka mzima ni mtaji wa vyama vya siasa kwa muendelezo wa umaskini wa yule anayejazwa siasa kwa kigezo cha demokrasia na uhuru na haki. Hii ni mbinu ya kimagharibi ya kudhoofisha utaifa wa nchi za Afrika.
😂😂😂 Eti vijana wengi..? Ubaya Ni kwamba higher officers kwenye vitengo mbalimbali jeshini, kwa asilimia kubwa Ni wafuasi lialia wa CCM, na Marafiki wa huyo mnaemuita jiwe na masirahi yao Ni makubwa kuliko mnavyofikiri(hawana njaa).Ni ngumu Sana kulitumainia jeshi hapa TZ, hasa kwa mfumo huu wa uongozi ambao rais Ni Amri jeshi mkuu.Umesema kweli mkuu ila Kuna jamaa yangu mjeda anakuambia vijana wengi walioko jeshini intake mpya mpya wanapenda haki na mabadiliko sasa sielewi anamaanisha nini.
Hata hivyo akitakiwa aishie mwaka wa pili tu.Mchato miaka 5 inamtosha sana
Sawa Mkuu! Kwa hiyo msimamo wako ni upi Kati haya mawili?Magharibi waligawana afrika mwaka 1884 maana yake wakati babu zetu wanatembea uchi wao walikuwa na dunia ya viwanda.
Hawa kuja afrika kutembea Bali kutafuta maligafi. Huwezi kufanana na mzungu kwenye masuala ya utamaduni, siasa na hata masuala ya kijamii..mzungu katutawala haipo namna ya sisi kufanana nae kwenye suala la demokrasia.
Tufanye kazi tusipumbazwe na watu waliowajua babu zetu tangu wakitembea uchi.
Wanayo malengo yao ambayo historia imekuwa ikiyaanika licha ya kuwa ni somo lenye maumivu kwa wale wanaohadaiwa na pipi ya demokrasia.
Nawaomba sana NEC na Vyombo vyote vya Dola, chondechonde kwa idadi ya Watanzania wanaojitokeza kumpokea na kumsikiliza Lissu kwa furaha na mapenzi yao ya dhati kwake na kwa chama chake nawaomba sana enyi watumishi wa NEC na Majeshi yetu, ruhusuni Haki ichukue mkondo wake, msiwanyime Watanzania haki yao ya kuongozwa na mtu wanaemtaka. Msiwanyime maelfu kwa mamilioni ya Watanzania furaha kwa kuwabadilishia mtu wanaemtaka na kumweka mtu wasiyemtaka.
Hata kikiingia chama kingine madarakani stahiki zenu mtapata tu, tena yaweza kuwa zaidi. Na mtu akishashindwa kihalali hawezi kuwafanya lolote,msiogope. Umati wote unaojitokeza kumlaki Lissu kuwakosesha Raha Mungu hata kaa kimya nasema.
Au maafa yakitokea kwa umati huo kuona umedhulumiwa, nyie mtapata faida gani kiuchumi na kiroho? Tazameni mapokezi ya Lissu tangu anarudi nchini na hata sasa wakati wa Kampeni,tazama Kawe,Arusha na leo Mwanza.
Kama atashindwa kihalali sawa, nyie simamieni Haki, lakini kama atashinda, mpeni Haki yake nanyi mtapata heshima ya milele na tuzo huko kwa Mungu.
Najua hata sasa hivi hatendewi Haki mtu huyu, kwa sababu hujuma juu yake Ni kubwa mno, kuliko Uchaguzi wowote uliowahi kutokea,ingawa bado watu wengi sana wanamuunga mkono.
Enyi NEC na Vyombo vya dola ruhusuni Haki itendeke.
Ni gharama nafuu mno kuruhusu Haki itendeke, lakini Ni gharama kubwa mno kuzuia Haki isitendeke.
Mkiruhusu Haki ikatendeka, mtakumbukwa Kama mashujaa wa Haki. Nayo majina yenu yataandikwa kwa wino wa dhahabu.
Vizazi vijavyo vitapenda kusoma habari zenu kwa furaha na majigambo,nayo mataifa yataja jifunza juu ya maamuzi yenu ya haki, nanyi mkiendelea kuheshimika.
Duh! Unatumia ushahidi gani kusema tukitumia demokrasia hatutapiga hatua? Acheni kuingizwa mkenge na waroho wa madaraka. Kila pambio wanaloimba mnadakia tu, vinginevyo na wewe labda ni mnufaika wa udikteta uchwara ndiyo maana unatetea huu ubakaji wa demokrasia.Mnataka demokrasia gani nyie watu🤔?
Amini nakwambieni, kwa nature ya watanzania demokrasia ikiendekezwa sana, hatutapiga hatua.Hiki kiwango Cha demokrasia kinatosha Sana.
Duh! Nilidhani napeana changamoto na mtu mvumilivu kisiasa,kumbe sivyo. Pole Mkuu, maana nikiendelea zaidi naona dalili za kukoseana heshima. Nakubali kutokukubaliana nawe.Kwani wewe tukiachana na uwezo wako wa kubweka🗣️ hapa, unatumia ushahidi gani kuamini kwamba bila demokrasia nchi haiwezi kuendelea..? Au unadhani nchi zisizo fungamana na mfumo wa marekani wa democracy, zenye chama kimoja haziendelei🤔?
Nimekujibu Kama ulivyokuja bila kuchunguza jibu langu.Hakuna sehemu niliyosema, tuongozwe bila demokrasia.