Kwa mara ya kwanza kabisa, fainali ya Kombe la Dunia 2026 itakuwa na show wakati wa mapumziko kama Super Bowl

Kwa mara ya kwanza kabisa, fainali ya Kombe la Dunia 2026 itakuwa na show wakati wa mapumziko kama Super Bowl

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu

Soka linaongezewa tuvitu vitu🤩

Rais wa FIFA, Gianni Infantino, amethibitisha kuwa fainali ya Kombe la Dunia la 2026 itakuwa na onyesho maalum kwa mara ya kwanza katika historia ya mashindano hayo kwenye muda ambao timu zinaenda kupumzika.

IMG_3384.jpeg

IMG_3385.jpeg

Kombe la Dunia 2026 litakuwa toleo la 23 la michuano hiyo na litaandaliwa kwa ushirikiano wa Marekani, Kanada, na Meksiko. Hii itakuwa mara ya kwanza kwa nchi tatu kushirikiana kuandaa Kombe la Dunia.

Maelezo Muhimu:

• Tarehe: Mashindano yataanza Juni 11, 2026, na fainali itachezwa Julai 19, 2026.

• Nchi Mwenyeji: Marekani, Kanada, na Meksiko.

• Idadi ya Timu: 48 (imeongezeka kutoka 32 kwenye michuano iliyopita).

• Miji na Viwanja: Kutakuwa na jumla ya viwanja 16 vilivyochaguliwa katika miji tofauti, ikiwemo New York/New Jersey (MetLife Stadium), Los Angeles (SoFi Stadium), na Mexico City (Estadio Azteca).


• Mfumo Mpya: Timu zitagawanywa katika makundi 12 ya timu 4 kila moja, na timu mbili bora pamoja na nne bora kutoka nafasi ya tatu zitaingia raundi ya 32 bora.

Kombe hili linatarajiwa kuwa kubwa zaidi katika historia ya FIFA kutokana na ongezeko la timu na idadi ya mashabiki wanaotarajiwa kuhudhuria.
 
Refalii atakayechezesha Yanga vs Simba a.k.a Kariakoo Derby. Huenda akachezesha fainali hizi za FIFA? Tupate muongozo
 
Ngoja tuone msanii gani atapewa tenda
 
tatizo mechi nyingi zitakua usiku wa ma8, kwa saa za tandale. World Cup itavunja mahusiano na ndoa nyingi sana hapa bongo, kwa wale wasiojitambua.
 
Back
Top Bottom