Kwa mara ya kwanza nitavaa suti kwenye harusi ya dada. Naomba ushauri wako rafiki!

Kwa mara ya kwanza nitavaa suti kwenye harusi ya dada. Naomba ushauri wako rafiki!

kilambimkwidu

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2017
Posts
6,097
Reaction score
7,199
Ndugu wana Chit-Chat,

Tangu nimeijua dunia sijawahi kuvaa vazi la suti, hua naona watu tu wamevaa. Inasemekana ni vazi rasmi kwa shughuli maalum kama harusi. Mimi zangu ni: chini sandoz, suruali kadeti/jeans/kodrai na tisheti hasahasa tisheti ya jezi au shati ya mikono mifupi, basi. Sijawahi kuvaa suti wala hata tu kuchomekea suruali na shati sijawahi. Na hata shati la mikono mirefu kwangu ni mwiko.

Ninao mtihani siku ya harusi ya dada mwezi wa kumi. Jana kenye kikao cha familia kaka wa bibi harusi nimeamrishwa kuvaa suti siku hiyo. Naambiwa imetengwa hela nikashoneshe suti na nimeambiwa rangi nichague mwenyewe. Sina ujanja, imebidi nikubaliane na jambo hilo.

Nafahamu hapa kuna wataalamu wa mitindo na wenye uzoefu na vazi hili. Naomba ushauri wenu kuhusu mambo ya kuzingatia ninaposhonesha hiyo suti ili fundi asiniharibie nguo. Pia nawaza, je ni dizaini gani ya suti inaweza kunifaa na mwonekano wangu siku hiyo utakuwaje?

Kama kuna mtu alivaa akapendeza naomba unisaidie picha ya fashion yake ili nimpelekee fundi wangu ageze mshono huo. Mimi ni mrefu futi 5 na ni mweusi.

Natanguliza shukrani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu wana Chit-Chat,

Tangu nimeijua dunia sijawahi kuvaa vazi la suti, hua naona watu tu wamevaa. Inasemekana ni vazi rasmi kwa shughuli maalum kama harusi. Mimi zangu ni: chini sandoz, suruali kadeti/jeans/kodrai na tisheti hasahasa tisheti ya jezi au shati ya mikono mifupi, basi. Sijawahi kuvaa suti wala hata tu kuchomekea suruali na shati sijawahi. Na hata shati la mikono mirefu kwangu ni mwiko.

Ninao mtihani siku ya harusi ya dada mwezi wa kumi. Jana kenye kikao cha familia kaka wa bibi harusi nimeamrishwa kuvaa suti siku hiyo. Naambiwa imetengwa hela nikashoneshe suti na nimeambiwa rangi nichague mwenyewe. Sina ujanja, imebidi nikubaliane na jambo hilo.

Nafahamu hapa kuna wataalamu wa mitindo na wenye uzoefu na vazi hili. Naomba ushauri wenu kuhusu mambo ya kuzingatia ninaposhonesha hiyo suti ili fundi asiniharibie nguo. Pia nawaza, je ni dizaini gani ya suti inaweza kunifaa na mwonekano wangu siku hiyo utakuwaje?

Kama kuna mtu alivaa akapendeza naomba unisaidie picha ya fashion yake ili nimpelekee fundi wangu ageze mshono huo. Mimi ni mrefu futi 5 na ni mweusi.

Natanguliza shukrani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Futi 5
 
Sasa si wakununulie suti spesheli kabisa!! achana na mambo ya kushonesha bwana!!!!
 
mkuu kwenye kuvaa suti sipawezi ila ingekua mavazi ya kisasa ata ningekupa ushauri
ila usivae bwanga mkuu utaboa
Naomba mwenye picha ya suti za mheshimiwa Kangi Lugola aweke hapa zinaweza kumfaa mwenzetu kwenye harusi ya dada yake.
 
Back
Top Bottom