Barnabas Mashamba
JF-Expert Member
- Jul 4, 2020
- 797
- 2,233
Ndugu wanaJF
Nimeona nishirikishe wasio na ajira rasmi kazi nitakayoieleza kwa mapana katika uzi huu (kwa vitendo kuanzia ufanyaji wa hali ya chini (kiwango duni) hadi kiwango cha juu) huku tukisubiri mirija ya asali (kazi tulizoomba) ifunguke.
Ndugu wanaJF
Natambua kuna fursa nyingi sana mtaani, kuna zinazohitaji mitaji na zinazohitaji uthubutu wako tu (hata kama huna mtaji). Hapa nitakuletea fursa ambayo unaweza ifanya hata kama huna mtaji ila una uthubutu pekee.
Ndugu wanaJF
Fursa yenyewe ni upigaji wa picha kwenye matukio mbalimbali (sherehe, mahafali n.k).
Ndugu wanaJF
Kwa kuanzia, leo darasa la saba wanahitimisha elimu yao ya hatua ya msingi ili mwakani waendelee na elimu ya upili (sekondari), sasa hiyo ni pesa.
Ndugu wanaJF
Kwa hali ya chini kabisa, ili uweze kupiga picha kwa wanafunzi wapate kumbukumbu za siku hii, unahitaji uwe na smartphone, kuna mtu anajiuliza, mbona huo tayari ni mtaji, kama sina smartphone huoni itanihitaji niwe na pesa ya kununua smartphone kwanza?
Ndugu mwanaJF
Namna ya kupata kifaa cha kupigia picha (kama huna ama kamera au smartphone) fanya yafuatayo.
1. Azima smartphone ya ama rafiki yako au ndugu aliye karibu, au mwanakanisa au mwanamziki mwenzako. Mweleze unaenda kufanyia nini, utapata.
2. Nenda kwenye photo studio iliyokaribu nawe na uulize swali hili "wapi nitapata kamera ya kukodi", utaelekezwa.
Ukishapata kifaa elekea sehemu ya tukio (shuleni) mida ambayo wanafunzi wanamaliza mtihani (around saa 10), kama una kamera ivae shingoni na mchezo utaanzia hapo. Kama una smartphone, utahitajika kuwatangazia wanafunzi kuwa unapiga picha.
Saa kumi nitaleta update humu ya namna mimi binafsi nitakavyokuwa nimeandaa eneo la kupigia picha.
Usisahau hili, piga picha chukua pesa, usipochukua pesa nakuhakikishia kuna picha utasafisha na hazitalipiwa (no matter how good they appear), kuna wanafunzi wanapiga kujifurahisha tu. Hivyo ukipiga picha na kuchukua pesa itakurahishia kwenye zoezi la kusafisha picha (means utasafisha tu zile zilizolipwa).
Nimeona nishirikishe wasio na ajira rasmi kazi nitakayoieleza kwa mapana katika uzi huu (kwa vitendo kuanzia ufanyaji wa hali ya chini (kiwango duni) hadi kiwango cha juu) huku tukisubiri mirija ya asali (kazi tulizoomba) ifunguke.
Ndugu wanaJF
Natambua kuna fursa nyingi sana mtaani, kuna zinazohitaji mitaji na zinazohitaji uthubutu wako tu (hata kama huna mtaji). Hapa nitakuletea fursa ambayo unaweza ifanya hata kama huna mtaji ila una uthubutu pekee.
Ndugu wanaJF
Fursa yenyewe ni upigaji wa picha kwenye matukio mbalimbali (sherehe, mahafali n.k).
Ndugu wanaJF
Kwa kuanzia, leo darasa la saba wanahitimisha elimu yao ya hatua ya msingi ili mwakani waendelee na elimu ya upili (sekondari), sasa hiyo ni pesa.
Ndugu wanaJF
Kwa hali ya chini kabisa, ili uweze kupiga picha kwa wanafunzi wapate kumbukumbu za siku hii, unahitaji uwe na smartphone, kuna mtu anajiuliza, mbona huo tayari ni mtaji, kama sina smartphone huoni itanihitaji niwe na pesa ya kununua smartphone kwanza?
Ndugu mwanaJF
Namna ya kupata kifaa cha kupigia picha (kama huna ama kamera au smartphone) fanya yafuatayo.
1. Azima smartphone ya ama rafiki yako au ndugu aliye karibu, au mwanakanisa au mwanamziki mwenzako. Mweleze unaenda kufanyia nini, utapata.
2. Nenda kwenye photo studio iliyokaribu nawe na uulize swali hili "wapi nitapata kamera ya kukodi", utaelekezwa.
Ukishapata kifaa elekea sehemu ya tukio (shuleni) mida ambayo wanafunzi wanamaliza mtihani (around saa 10), kama una kamera ivae shingoni na mchezo utaanzia hapo. Kama una smartphone, utahitajika kuwatangazia wanafunzi kuwa unapiga picha.
Saa kumi nitaleta update humu ya namna mimi binafsi nitakavyokuwa nimeandaa eneo la kupigia picha.
Usisahau hili, piga picha chukua pesa, usipochukua pesa nakuhakikishia kuna picha utasafisha na hazitalipiwa (no matter how good they appear), kuna wanafunzi wanapiga kujifurahisha tu. Hivyo ukipiga picha na kuchukua pesa itakurahishia kwenye zoezi la kusafisha picha (means utasafisha tu zile zilizolipwa).