Kwa matatizo ya gari

Habari, sijui utakuwa una ifahamu hii cheapest full synthetic oil nimekuwa nikiitumia kwa muda sasa kwenye injini ya 1kr-fe lakini changamoto ni oil kuisha sana na kwakweli hakuna sign ya leakage japo kidogo huwa kuna moshi blue labda gari ikiwa katika very high revolution, sasa cjui ni oil nzuri?
 
Muunda gari/chombo hua ameandika kwenye owner/operator manual au/na kwenye mfuniko wa chupa pale kw master cylinder. Ni muhimu kuzingatia
Mkuu kuna uwezekano wowote nikapata operation manual ya toyota succeed iliyoandikwa kwa kiingereza?
 
Shukrani mkuu nikifanikiwa kulitia mikononi ndinga nitakupa mrejesho
 
Natafuta fundi wa gari (Mazda DEMIO 2003), kwenye dashboard inablink neno "HOLD" hii ni baada ya kuwa gari injini imepoa vya kutosha, na ukihamisha gia hasa kwenda kwenye R,inagonga sana (kama inastua) gari inakuwa nzito ila ikitembea kilometa kadhaa ukaizima na kisha kuiwasha hilo neno HOLD linatoweka na gari inakuwa vizuri, baada ya kufanya diagnosis nikapata majibu ya code: P0745 EPC Circuit Fault.
Baada ya kugoogle hilo tatizo nikakuta ni tatizo la Control Solenoids hasa " Pressure Conrol Solenoid) ambazo ziko kwenye GIA BOX. Naomba kama kuna mtaalam anaweza tatua hili tatizo tuwasiliane.
 
Vipi kaka,
Asante kw swali.
Oili hiyo ni ya quality nzuri. Hebu jaribu oili ya total quartz 9000 full synthetic pia kisha nipe mrejesho.
 
Hilo ni tatizo la solenoid hiyo ya pressure inayopunguza pressure wakati wa engagement toka P au N na pia wakati mwingine kwenye D. Yakaa tatizo lenyewe ni intermittent kw kua lapotea unapofanya Key Off reset. Fanyiwa uchunguzi upande wa circuit/wiring kabla ya kuibadili solenoid yenyewe.
 

Nikushukuru sana kiongozi , nitafuatilia hiyo halafu nitaleta mrejesho.
 
Hapa issue yaweza kua tuning, plugs zisizoifaa engine au kasoro/tatizo kw mfumo wa VVTI. Diagnosis kwanza.
Ahsante sana kwa ushauri Mkuu, nilibadilidili plugs kwa kuagiza kupitia agent wa Toyota bt tatizo liliendelea kuwepo pia kuna fundi alinichekia akadai tatizo liko kwenye Air Mass flow imechafuka aliposafisha tatizo liliisha baada ya muda likajirudia. Naomba ushauri wako zaidi
 
Tune-up itatatua issue yako.
 
Mkuu hebu nisaidie haya mataa yananiwakia kila nikitembea km 10-15.

Aina ya gari ni toyota rav 4 2006.

Nilifanya diagnosis
Check engine ni air filter sensor.
VSC sijui
4WD sijui but niliwahi toa propeller baada ya kujinyonga na nikairudishia baada ya kurudisha ndio mambo yote hayo yakaja...
Airbag imekuja tu from no where..

 
Ni wazi kua ile issue ya vacuum kuwa juu na kuvuta oili kw manifold haiko. Oili yaweza kua yatokea kwa gaskets au seal, fanya engine wash ya nguvu kisha ukague engine kw makini.
Nimerudi mkuu nilipitia engen yote haina leakage kabisa,wakati wa service nilibali oil ya engen ikipungua kwa litre nzima,
nimeweka quarz 9000 litre nne,na kubadili air cleaner matokeo niliyoyaona nimeshavuka km 1500 ipo 1940 oil bado ipo kwenye level na ilikuwa inapungukia kuanzia 1500 sasa nasubiri nione mpaka 3000 itabaki hivyohivyo au itapungua je kama italeta matokeo chanya baada ya kutoa air cleaner shida ni nini kitaalam.
 
Mkuu, asante sana kwa ushauri unaotoa hapa jukwaani

Swali langu ni je una maelezo yoyote kuhusu taa ya pembe tatu na alama ya mshanga ndani mwake inayowaka katika gari za toyota raum??! maana mwanzo nilidhani ni yangu tu ila nimefatilia kila raum inawaka hiyo taa hata kama imetoka japan jana, je technical problem toka kiwandani ama ni nini hasa!!!! Gari haisumbui

Pili, ni ATF ipi nzuri inayofaa kutumika kwenye raum??
 
Mkuu usituchoke kwa maswali yetu..
Ni mabo gani yanasababisha gari kukosa nguvu au niseme halichanganyi upesi kama ilivyokuwa mwanzo..
Naona gari linapick 100kph kwa kazi sana tofauti na ilivyokuwa mwanzo.. ..
Gari hili nimewahi kubadili plug mara moja tu mwaka 2016 mpka sasa...
Siku za karibuni nimeweka transmission fluid mpya na oil natumia total quarts 9000 ila sijaona mafanikio ya kuongeza nguvu ya engine..
ushauri wako tafadhali...nifanye service ya vitu gani hapa
 
Asante kwa maelezo.
Kuna rafiki yangu ana Harrrier old model engine 2990cc anataka kuibadilisha na kuweka engine ya harrier hybreed 2400cc. Jee itabidi abadilishe na gearbox?
 
Mkuu hii kitu niliipata katika raum yangu lakini niligundua ukiendesha pasipo kufunga mkanda hiyo Alama inaonekana. Jaribu kufunga mkanda then tupe mrejesho hapa jukwaani
 
Vipi kaka
Unahitaji kufanyiwa diagnosis vizuri ili kuisoma hiyo code iliyoashiriwa na taa. Karibu umtafute fundi ana Techstream au uende kw Toyota Tanzania waifanyie diagnosis.
Sio aipime mwenyewe ?? Kama bado haja lekebisha na yupo dar mm nampa ofa ya kumpimia bureee kabisa na mashine za kutosha kuanzia TIS launch pro3 autoboss v30.maxidas ,ucandas n.k but kwa kufika ofisini lkn kama atataka kufuatwa alipo basi garama yake itakuwa ni kulipa usafiri tuu basi.
 
Kuna rafiki yangu ana Harrrier old model engine 2990cc anataka kuibadilisha na kuweka engine ya harrier hybreed 2400cc. Jee itabidi abadilishe na gearbox?
Mkuu kama nimekuelewa basi hilo swala ni gumu sanaaa aachane nalo nigum sana garama zake ni bora akanunua gari yenye mfumo huo wa hybrid..

Lkn kama unamaanisha kubadili gari ya hybrid na kuwa ya kawaida basi inawezekana 100% mm binafsi nishafanya sana na juzi tuu nimefanya kwenye estima akitaka nitampa bajeti na vitu vyote vinavyotakiwa kikubwa cha kununua ni gearbox vingine kwenye engine ni vidogo dogo sana..na wiring unatumia ile ile ya hybrid mambo yanakuwa mswano
 
Toyota RAV4 ya 2002 iliisha brake pads, taa za ABS na Parking brake zikawaka. Baada ya kubadilisha pads hizo, taa hazijazima hata baada ya kutembea 2000km.

Wheel speed sensor seems like hazijawa disconnected.
 
Ahsante sana kwa ushauri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…