Kwa matokeo haya ya mwaka 2010, je Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 tutegemee nini?

Kwa matokeo haya ya mwaka 2010, je Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 tutegemee nini?

Mag3

Platinum Member
Joined
May 31, 2008
Posts
13,413
Reaction score
23,592
Toka kuanza kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, tumeingia kwenye Uchaguzi Mkuu mara nne, 1995, 2000, 2005 na 2010 na katika chaguzi zote hizi hakuna uliokuwa na changamoto na wenye msisimko kama wa mwaka 2010. Naweza kusema, ingawa kuna wanaoweza kudai tofauti, kuwa hakuna wakati chama tawala kilijikuta kwwenye hatihati na hofu ya kupigwa chini kama mwaka 2010. Pia kama kuna wakati wananchi kwa ujumla wao walihamasika na kuwa na shauku ya kushiriki katika zoezi hilo, bila shaka yoyote mwaka 2010 hauna mpinzani. Lakini ilikuwakuwaje hadi walioweza kujitokeza kupiga kura wasitimie hata nusu (wakawa pungufu ya asilimia 50%) ya waliojiandikisha?

MwakaWaliojiandikishaWaliopiga kuraAsilimiaKura halali
19958,928,8266,846,68177%
200010,088,4848,517,59884.43%
200516,407,31811,365,47772.4%
201020,137,3038,397,96342.8%

Lakini linaloleta hofu kuliko hata hayo matokeo ni kukosekana kwa tathmini ya hali kama hiyo ilivyoweza kujitokeza; si Tume ya Uchaguzi, si serikali, si bunge, si vyama vya siasa, si wanaharakati, si wasomi...hakuna kikundi chochote kilichoweza kukaa kujadili, kutafakari na kutoa tathmini ya uchaguzi huo na kutoa sababu kwa nini hali kama hiyo ilijitokeza. Kama kawaida yetu Watanzania inaonekana hakuna mtu, kundi, taasisi wala jumuiya iliyostushwa na hali hiyo na kuhoji kulikoni hivyo leo nimeamua kulileta jambo hili kwenye hili jamvi letu wana JF; tusaidiane kwa mawazo tusiruhusu tena hali hiyo kujirudia huko baadaye tukielekea kutakiwa kupitisha Katiba kwa kura ya maoni.

Kwa mara ya kwanza hebu tujitahidi kutanguliza maslahi ya taifa mbele ya chama, karibuni.

cc: Mchambuzi, Nguruvi3, EMT, Mzee Mwanakijiji, Pasco, Jasusi, JokaKuu, Bongolander, Kobello, Mkandara, Dingswayo, Mimibaba,tpaul, chama, MwanaDiwani, ZeMarcopolo, zomba, Ritz, Pasco, Alinda, steveDii, Kichuguu, Elli, Crashwise, Kitila Mkumbo, Zitto, Mtanganyika, Mr Rocky, Tuko, zumbemkuu, nyabhingi, lynxeffect22, MTAZAMO, Bulldog, Tized, Erythrocyte, MEANDU, jmushi1
 
Ndugu Mag3 ukweli ni kuwa watu wengi sana walijitokeza kupiga kura kuliko hata mwaka 1995 wakati wa NCCR-Mageuzi na Mrema wao. Tatizo ni kuwa kura nyingi ambazo hazikuwa za CCM mwaka 2010 hazikuhesabiwa kabisa na wala haziko kwenye data zako hizo. Siri yote ya kura hizo iko kwenye tume ya uchaguzi na kwa vile Mwenyekiti wake ameshatangulia mbele ya haki, basi hatutakuja kupata nafasi adimu kama tuliyopata klutoka kwa Profesa Mbilinyi hivi majuzi kujua ukweli halisi, itabaki hivyo hivyo!

Kilichotakiwa sasa ni kushupalia sana swala la katiba mpya kusudi tume ya uchaguzi isiwe tegemezi ya serikali iliyoko madarakani na kuwa inaingiwa katika utendaji wake.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mag3

Kuna kundi jingine tunalisahau. Hawa wasomi wanaofanya tafiti za kisiasa hata siku moja hawajawahi kuliongelea hilo.
Kuna taasisi lukuki zinazotoa mitazamo ya kisiasa, hasa wagombea wa vyama, tathmini za chaguzi n.k.
Hutasikia wakiongelea suala hili la kujiandikisha bila kupiga kura.

Tatizo lililopo si la bahati mbaya ni la kupangwa. Tume ya uchaguzi inajua hilo kikamilifu lakini wafanyeje ikiwa wametumwa na ''mzee'' !!

Nasi Watanzania ni watu wa matukio. Uchaguzi wa Mbeya vijijini tuliona hilo.
Waliojiandikisha walikuwa karibu 75% waliopiga kura 35%. Tulipaza sauti hakuna aliyesikia, si vyama vya siasa, tume au serikali.

Kuna 'voter suppression'' hilo linahitaji majibu.
 
Toka kuanza kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, tumeingia kwenye Uchaguzi Mkuu mara nne, 1995, 2000, 2005 na 2010 na katika chaguzi zote hizi hakuna uliokuwa na changamoto na wenye msisimko kama wa mwaka 2010. Naweza kusema, ingawa kuna wanaoweza kudai tofauti, kuwa hakuna wakati chama tawala kilijikuta kwwenye hatihati na hofu ya kupigwa chini kama mwaka 2010. Pia kama kuna wakati wananchi kwa ujumla wao walihamasika na kuwa na shauku ya kushiriki katika zoezi hilo, bila shaka yoyote mwaka 2010 hauna mpinzani. Lakini ilikuwakuwaje hadi walioweza kujitokeza kupiga kura wasitimie hata nusu (wakawa pungufu ya asilimia 50%) ya waliojiandikisha?

MwakaWaliojiandikishaWaliopiga kuraAsilimiaKura halali
19958,928,8266,846,68177%
200010,088,4848,517,59884.43%
200516,407,31811,365,47772.4%
201020,137,3038,397,96342.8%

Lakini linaloleta hofu kuliko hata hayo matokeo ni kukosekana kwa tathmini ya hali kama hiyo ilivyoweza kujitokeza; si Tume ya Uchaguzi, si serikali, si bunge, si vyama vya siasa, si wanaharakati, si wasomi...hakuna kikundi chochote kilichoweza kukaa kujadili, kutafakari na kutoa tathmini ya uchaguzi huo na kutoa sababu kwa nini hali kama hiyo ilijitokeza. Kama kawaida yetu Watanzania inaonekana hakuna mtu, kundi, taasisi wala jumuiya iliyostushwa na hali hiyo na kuhoji kulikoni hivyo leo nimeamua kulileta jambo hili kwenye hili jamvi letu wana JF; tusaidiane kwa mawazo tusiruhusu tena hali hiyo kujirudia huko baadaye tukielekea kutakiwa kupitisha Katiba kwa kura ya maoni.

Kwa mara ya kwanza hebu tujitahidi kutanguliza maslahi ya taifa mbele ya chama, karibuni.

cc: Mchambuzi, Nguruvi3, EMT, Mzee Mwanakijiji, Pasco, Jasusi, JokaKuu, Bongolander, Kobello, Mkandara, Dingswayo, Mimibaba,tpaul, chama, MwanaDiwani, ZeMarcopolo, zomba, Ritz, Pasco, Alinda, steveDii, Kichuguu, Elli, Crashwise, Kitila Mkumbo, Zitto, Mtanganyika, Mr Rocky, Tuko, zumbemkuu, nyabhingi, lynxeffect22, MTAZAMO, Bulldog, Tized, Erythrocyte, MEANDU, jmushi1


Matukio haya yataendelea kutokea mkuu. Bahatio mbaya hatujui kilichofanyika kwenye uchakachuaji wa matokeo, lakini inaonekana kabisa kuwa wananchi waliamka, lakini ili CCM iendelee kuwepo madarakani kilifanyika kitu kama voters suppression ameeleza Nguruvi3. Tatizo ni kwamba tunapojiandikisha hawa hatujali sana kama tunapiga kura, au kama kura tulizopiga zinahesabiwa kama tulivyopiga na zinaonesha kile tunachochagua.

Tunahitaji elimu zaidi ya uhamasishaji. Kama tukiifanya JF imfikie kila mwenye simu ya mkononi itakuwa kazi nzuri sana. Nadhani ongezeko la watu kujiandilisha kwenye uchaguzi wa mwaka 2010. Lilitokana na watu kuchoshwa na kukasirishwa na CCM na Chadema kupiga kampeni vizuri.
 
Wakati tunaendelea kujadili zoezi la upigaji kura mwaka 2010 na namna sisi kama wananchi tunavyoweza kuangalia namna ya kuhakikisha hali kama hiyo haijitokezi mwaka 2015, naomba tujikumbushe matukio mawili yafuastayo;

images


1. Mkumbwa Ally

Miezi miwili kabla ya Uchaguzi na hali ikionekana tata kwa chama tawala Mkumbwa Ally, akiwa Kaimu Mhariri Mtendaji wa Tanzania Standard Newspapers Ltd., alitoa tahariri kupitia gazeti la serikali la Daily News akidai, nanukuu, "Na ukweli ni kwamba Dk Willibrod Slaa hatakuwa rais wa tano wa Tanzania." Alitoa tahariri hii kwa niaba ya serikali akiwa na maana kwamba ushindi wa Dr. Slaa kwa namna yoyote ile haukubaliki na hautakubalika.

Kwa sasa Mkumbwa Ally ni Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Wizara ya Mambo Nje.


images


2. Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo.



Wiki moja baada ya tamko la serikali kupitia gazeti lake la Daily News, Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa jeshi, (JWTZ) akifuatana na na Kamanda wa Kikosi cha Operesheni Maalumu cha Jeshi la Polisi nchini, Venance Tossi na Kaimu pamoja Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya jinai Peter Kivuyo, naye alitoa onyo kwa wananchi akitishia nanukuu;

Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) likishirikiana na Jeshi la Polisi nchini linavitaka vyama vya siasa kukubali matokeo baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba na kuonya kwamba vyombo vya ulinzi na usalama vimejiandaa kikamilifu kupambana na yeyote atakayejaribu kuyakataa matokeo.
Kwa sasa Abdulrahman Shimbo ni balozi wetu China.

Haya matukio mawili yaliweka historia katika taifa letu na duniani kwa serikali kutumia gazeti la umma kuwachagulia wananchi viongozi na kuvitumia vyombo vya dola kuwatisha wananchi kuwakubali hao viongozi. Kabla hatujaendelea zaidi na mjadala nimeona ni vizuri nikumbushe matukio haya ya kushangaza yaliyolikumba zoezi zima la uchaguzi mwaka 2010 na baadaye nitaonesha kwa ushahidi muitikio wa wananchi na walivyojitokeza kwa wingi kushiriki katika upigaji kura.

UDSM naamini kuna kitengo cha Political Science na pia tunao political scientists; naamini kwa namna fulani hiki kitengo ndicho kingeongoza kama think tank kwa maswala ya kisiasa hapa nchini. Ukimya wao kuhusu mchakato mzima wa zoezi la Uchaguzi Mkuu mwaka 2010 na kutoa tathmini na jinsi ulivyoendeshwa toka hatua za awali hadi mshindi kutangazwa hakika unasikitisha. Kwamba taifa linaweza kumpata Raisi anayetangazwa mshindi kwa kupata asilimia 25% tu za waliojiandikisha kupiga kura? Kama hawakujiandikisha hilo ni swali lingine lakini kwa 20,000,000 waliojiandikisha kupiga kura, 12,000,000 walipotelea wapi?

cc: Mchambuzi, Nguruvi3, EMT, Mzee Mwanakijiji, Pasco, Jasusi, JokaKuu, Bongolander, Kobello, Mkandara, Dingswayo,Mimibaba,tpaul, chama, MwanaDiwani, ZeMarcopolo, zomba, Ritz, Pasco, Alinda, steveDii, Kichuguu, Elli, Crashwise, Kitila Mkumbo, Zitto, Mtanganyika, Mr Rocky, Tuko, zumbemkuu, nyabhingi, lynxeffect22, MTAZAMO, Bulldog, Tized, Erythrocyte,MEANDU, jmushi1
 
Wakati tunaendelea kujadili zoezi la upigaji kura mwaka 2010 na namna sisi kama wananchi tunavyoweza kuangalia namna ya kuhakikisha hali kama hiyo haijitokezi mwaka 2015, naomba tujikumbushe matukio mawili yafuastayo;

images


1. Mkumbwa Ally​

...........


images


2. Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo.

........

Ndyo maana nilikwambia kuwa matokeo ya uchaguzi huo yalipangwa kwa kuondoa kura nyingi ambazo hazikuwa za CCM! Ilikuwa imekubaliwa kuwa kura zote ziripotiwe direct kutoka huko huko Wilayani lakini utaratiobu ukabadilika ghafla hesabu ikaminywa mpaka siku ya mwisho!
 
Jaji Lewis Makama amefariki bila ya kukamilisha matokeo. Hakuna anayejua kura za mwisho zilikuwaje.
Tunachokumbuka Jaji alisema kura haziwezi kubadili matokeo.

Tunachoshindwa kuelewa ni kuwa katika idadi hiyo ndogo JK alishinda kwa 60 akiwa incumbent president.
Nini kingetokea kama waliojiandikisha wangefikia 75%

Mag3 , idara zetu ni za akina Benson sasa sijui tutarajie nini
Na wala si UDSM, sasa hivi kuna vyuo lukuki kwanini hawafuatilii hili jambo? Au ni zito kutia mikono!
 
Ndyo maana nilikwambia kuwa matokeo ya uchaguzi huo yalipangwa kwa kuondoa kura nyingi ambazo hazikuwa za CCM! Ilikuwa imekubaliwa kuwa kura zote ziripotiwe direct kutoka huko huko Wilayani lakini utaratiobu ukabadilika ghafla hesabu ikaminywa mpaka siku ya mwisho!
Mkuu Kichuguu, je unadhani mbinu hii hii chafu inaweza kutumika tena wananchi watakapotakiwa kuipitisha katiba mpya kwa njia ya kura ya maoni? Je yawezekana kwamba jeuri ya chama tawala kuendelea na mchakato wa katiba mpya licha ya kususiwa na baadhi ya wananchi inatokana na mbinu hiyo chafu? Je wananchi watakubali kwa mara nyingine kushinda juani ili waweze kupiga kura halafu mwisho wa siku kura zao hazijulikani zimepotelea wapi?
 
Last edited by a moderator:
Wakati tunaendelea kujadili zoezi la upigaji kura mwaka 2010 na namna sisi kama wananchi tunavyoweza kuangalia namna ya kuhakikisha hali kama hiyo haijitokezi mwaka 2015, naomba tujikumbushe matukio mawili yafuastayo;

images


1. Mbelwa Kairuki

Miezi miwili kabla ya Uchaguzi na hali ikionekana tata kwa chama tawala Mkumbwa Ally, akiwa Kaimu Mhariri Mtendaji wa Tanzania Standard Newspapers Ltd., alitoa tahariri kupitia gazeti la serikali la Daily News akidai, nanukuu, "Na ukweli ni kwamba Dk Willibrod Slaa hatakuwa rais wa tano wa Tanzania." Alitoa tahariri hii kwa niaba ya serikali akiwa na maana kwamba ushindi wa Dr. Slaa kwa namna yoyote ile haukubaliki na hautakubalika.

Kwa sasa Mkumbwa Ally ni Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Wizara ya Mambo Nje.


images


2. Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo.



Wiki moja baada ya tamko la serikali kupitia gazeti lake la Daily News, Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa jeshi, (JWTZ) akifuatana na na Kamanda wa Kikosi cha Operesheni Maalumu cha Jeshi la Polisi nchini, Venance Tossi na Kaimu pamoja Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya jinai Peter Kivuyo, naye alitoa onyo kwa wananchi akitishia nanukuu;


Kwa sasa Abdulrahman Shimbo ni balozi wetu China.

Haya matukio mawili yaliweka historia katika taifa letu na duniani kwa serikali kutumia gazeti la umma kuwachagulia wananchi viongozi na kuvitumia vyombo vya dola kuwatisha wananchi kuwakubali hao viongozi. Kabla hatujaendelea zaidi na mjadala nimeona ni vizuri nikumbushe matukio haya ya kushangaza yaliyolikumba zoezi zima la uchaguzi mwaka 2010 na baadaye nitaonesha kwa ushahidi muitikio wa wananchi na walivyojitokeza kwa wingi kushiriki katika upigaji kura.

UDSM naamini kuna kitengo cha Political Science na pia tunao political scientists; naamini kwa namna fulani hiki kitengo ndicho kingeongoza kama think tank kwa maswala ya kisiasa hapa nchini. Ukimya wao kuhusu mchakato mzima wa zoezi la Uchaguzi Mkuu mwaka 2010 na kutoa tathmini na jinsi ulivyoendeshwa toka hatua za awali hadi mshindi kutangazwa hakika unasikitisha. Kwamba taifa linaweza kumpata Raisi anayetangazwa mshindi kwa kupata asilimia 25% tu za waliojiandikisha kupiga kura? Kama hawakujiandikisha hilo ni swali lingine lakini kwa 20,000,000 waliojiandikisha kupiga kura, 12,000,000 walipotelea wapi?

cc: Mchambuzi, Nguruvi3, EMT, Mzee Mwanakijiji, Pasco, Jasusi, JokaKuu, Bongolander, Kobello, Mkandara, Dingswayo,Mimibaba,tpaul, chama, MwanaDiwani, ZeMarcopolo, zomba, Ritz, Pasco, Alinda, steveDii, Kichuguu, Elli, Crashwise, Kitila Mkumbo, Zitto, Mtanganyika, Mr Rocky, Tuko, zumbemkuu, nyabhingi, lynxeffect22, MTAZAMO, Bulldog, Tized, Erythrocyte,MEANDU, jmushi1

A bit of correction hiyo picha si mkubwa Ally.
By the way ukweli ni kwamba kwa katiba ya sasa na mindset iliyopo kwa watawala, hata opposition wakishinda hali itakuwa ile ile CCM wataendelea kutawala.

Itakuwa kama Zanzibar CUF wanashinda CCM inatawala.
 
Back
Top Bottom