GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Kama kuna Mtu ambaye atakuwa na furaha Kubwa na ya Kifani pale Timu ya Taifa ya Tanzania ( Taifa Stars ) ikifungwa na Kushindwa Kufuzu AFCON basi bila Kupepesa Macho, Kumung’unya Maneno wala Kutikisa Masikio nitakuwa ni Mimi GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE “ Purely Talented, Charismatic Fella, Game Changer and Entertainer “.
Sababu zangu zaweza zikawa zipo lukuki / nyingi ila Kubwa ni hizi mbili tu ambapo ya Kwanza ni kwamba sina Imani na Kocha Emanuel Amunike kwani ameshaanza Kuonyesha wazi wazi kuwa ana Chuki za wazi ( Kisununu ) kwa Wachezaji wa Simba SC ambao Mimi naona ndiyo Wachezaji bora kuliko Wachezaji wote waliopo katika Ligi Kuu ya Tanzania.
Sababu yangu ya Pili na ambayo ndiyo imenikera hadi kunifanya nizidi Kutomkubali huyu Kocha Amunike ni Kitendo chake cha Kuchagua Wachezaji wengi wa Timu mbovu ya Yanga SC na ambao pia hawana Uwezo hata wa 25% tu ya Kuwafiki Uwezo walionao Wachezaji wa Timu iliyobarikiwa na Mwenyezi Mungu ya Simba Sports Club.
Ni Tusi Kubwa leo hii Kocha wa Taifa Stars unachangua Wachezaji Wanne ( 4 ) wa Yanga SC na unachagua Wachezaji Watatu ( 3 ) tu wa Simba SC wakati Kiufundi tu alitakiwa achague Wachezaji kati ya Saba ( 7 ) au Tisa ( 9 ) wa Simba SC ila hakufanya hivyo.
Na tayari nimeshatoa Siri zote za Ushindi kwa Uganda Cranes na kama kuna Mtanzania ambaye labda anadhani Taifa Stars itashinda Jumapili pale Kwa Mkapa ( zamani kwa Mchina ) au Uwanja wa Taifa basi atakuwa si tu kwamba amepotea bali pia ni bonge la Popoma kwani ukweli ni kwamba Uganda Cranes wanaenda Kutufunga Goli kati ya Tano ( 5 ) au Saba ( 7 ) hiyo Siku.
Kocha Amunike alipashwa awaite Wachezaji hawa Aishi Manula, Jonas Mkude, John Boko, Paul Bukaba, Hassan Dilunga, Mohammed Hussein Tshabalala, Adam Salamba, Said Ndemla, Adam Salamba na Rashid Juma ila alichofanya Yeye kawaita akina Manula, Mkude na Boko tu pekee huku akitujazia Michezaji mibovu tupu ya Yanga SC.
Na ole wake nimuone mwana Simba SC hiyo Jumamosi anaishangilia Taifa Stars badala ya Uganda Cranes na kwa wale ambao mnahitaji Jezi nzuri za Uganda Cranes ambazo pia zina Rangi Nyekundu mnitafute PM ili niwapeni kwani ninazo nyingi sana na ole wake tena Siku ya Jumapili ambapo nitaingia Uwanjani nikiwa nimevalia Jezi yangu ya Uganda Cranes nione Mtanzania yoyote ananishangaa au ananitibu kwani huenda Siku hiyo ndiyo atajua kwanini Nyoka hana Ugoko kwa Kitakachompata.
Nitarudi tena Kuishangilia Taifa Stars pale tu ama TFF wakimfukuza Kocha Amunike au Kocha Amunike awaongeze hao Wachezaji tajwa hapo juu au Kocha Amunike awe si Mpenzi bali ikiwezekana awe pia ni Mwanachama wa Simba SC ndipo nitamkubali lakini zaidi ya hapo nitamchukia kwa muda wote ambao atakuwepo hapa Tanzania. Ni bora hata basi angeitwa Wachezaji Tisa ( 9 ) au hata Kumi ( 10 ) wa Azam FC ningemuelewa ila siyo Kutujazia tu Michezaji mibovu ya Yanga SC ambayo haifikii hata tu 25% ya Uwezo walionao Wachezaji wa Simba SC.
Amunike aondoke na Wachezaji wa Yanga SC wapunguzwe Taifa Stars.
Nawasilisha.
Cc: Ulimakafu , hazard cfc , Balantanda , Prince Kunta , Tui , logframe , SUPER EMILY
Sababu zangu zaweza zikawa zipo lukuki / nyingi ila Kubwa ni hizi mbili tu ambapo ya Kwanza ni kwamba sina Imani na Kocha Emanuel Amunike kwani ameshaanza Kuonyesha wazi wazi kuwa ana Chuki za wazi ( Kisununu ) kwa Wachezaji wa Simba SC ambao Mimi naona ndiyo Wachezaji bora kuliko Wachezaji wote waliopo katika Ligi Kuu ya Tanzania.
Sababu yangu ya Pili na ambayo ndiyo imenikera hadi kunifanya nizidi Kutomkubali huyu Kocha Amunike ni Kitendo chake cha Kuchagua Wachezaji wengi wa Timu mbovu ya Yanga SC na ambao pia hawana Uwezo hata wa 25% tu ya Kuwafiki Uwezo walionao Wachezaji wa Timu iliyobarikiwa na Mwenyezi Mungu ya Simba Sports Club.
Ni Tusi Kubwa leo hii Kocha wa Taifa Stars unachangua Wachezaji Wanne ( 4 ) wa Yanga SC na unachagua Wachezaji Watatu ( 3 ) tu wa Simba SC wakati Kiufundi tu alitakiwa achague Wachezaji kati ya Saba ( 7 ) au Tisa ( 9 ) wa Simba SC ila hakufanya hivyo.
Na tayari nimeshatoa Siri zote za Ushindi kwa Uganda Cranes na kama kuna Mtanzania ambaye labda anadhani Taifa Stars itashinda Jumapili pale Kwa Mkapa ( zamani kwa Mchina ) au Uwanja wa Taifa basi atakuwa si tu kwamba amepotea bali pia ni bonge la Popoma kwani ukweli ni kwamba Uganda Cranes wanaenda Kutufunga Goli kati ya Tano ( 5 ) au Saba ( 7 ) hiyo Siku.
Kocha Amunike alipashwa awaite Wachezaji hawa Aishi Manula, Jonas Mkude, John Boko, Paul Bukaba, Hassan Dilunga, Mohammed Hussein Tshabalala, Adam Salamba, Said Ndemla, Adam Salamba na Rashid Juma ila alichofanya Yeye kawaita akina Manula, Mkude na Boko tu pekee huku akitujazia Michezaji mibovu tupu ya Yanga SC.
Na ole wake nimuone mwana Simba SC hiyo Jumamosi anaishangilia Taifa Stars badala ya Uganda Cranes na kwa wale ambao mnahitaji Jezi nzuri za Uganda Cranes ambazo pia zina Rangi Nyekundu mnitafute PM ili niwapeni kwani ninazo nyingi sana na ole wake tena Siku ya Jumapili ambapo nitaingia Uwanjani nikiwa nimevalia Jezi yangu ya Uganda Cranes nione Mtanzania yoyote ananishangaa au ananitibu kwani huenda Siku hiyo ndiyo atajua kwanini Nyoka hana Ugoko kwa Kitakachompata.
Nitarudi tena Kuishangilia Taifa Stars pale tu ama TFF wakimfukuza Kocha Amunike au Kocha Amunike awaongeze hao Wachezaji tajwa hapo juu au Kocha Amunike awe si Mpenzi bali ikiwezekana awe pia ni Mwanachama wa Simba SC ndipo nitamkubali lakini zaidi ya hapo nitamchukia kwa muda wote ambao atakuwepo hapa Tanzania. Ni bora hata basi angeitwa Wachezaji Tisa ( 9 ) au hata Kumi ( 10 ) wa Azam FC ningemuelewa ila siyo Kutujazia tu Michezaji mibovu ya Yanga SC ambayo haifikii hata tu 25% ya Uwezo walionao Wachezaji wa Simba SC.
Amunike aondoke na Wachezaji wa Yanga SC wapunguzwe Taifa Stars.
Nawasilisha.
Cc: Ulimakafu , hazard cfc , Balantanda , Prince Kunta , Tui , logframe , SUPER EMILY