Kwa Mh. Rais Samia,Salamu

Denis Swai

Member
Joined
Sep 9, 2024
Posts
27
Reaction score
67
Mheshimiwa Rais Samia ninakutumia salamu za pongezi nchi hii unaiongoza vizuri sana, tangu nianze kupiga kura sijawahi kuipigia CCM ila safari hii kutokana na uongozi wako mzuri mama nitaipigia CCM, wewe ni RAIS wa kiwango cha dunia, siyo wa kiwango cha Afrika mashariki wala Africa.

Kiashiria kwamba uongozi wako ni mzuri uliotukuka ni kiwango cha wahamiaji haramu wanaoongezeka mfano wachezaji wa mpira wengi wanaomba urai ni kwa sababu wanaona nchi hii ni mahali salama pa kuishi.

Ninachokuomba mama ni umshauri mkurugenzi wa uhamiaji akaze boot wahamiaji haramu wanaongezeka kwa kasi, wasione vianaelea vimeundwa.

Wanaokulaumu wanataka waongozweje? Jamani,

Salamu sana mama na mungu akubariki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…