Unachekesha sana, hivi kenya jeshi lenu halina wana-maji, na kama mnao je, hawana vifaa..? Nyambizi huwa zinapita chini ya maji mnawezaje muwe na nyamizi zisizo na vifaa sisi mwanza ferry ili binuliwa na vifaa vyetu vya kijeshi faster.
Mwenye hekima akivuliwa nguo huchuchumaa,hakimbizani.Utakua umedandia bila kusoma nilichokiandika, unaonekana huna hata habari nini kinazungumzwa kuhusu. Ukanda wote huu hamna jeshi la wana maji lenye uwezo zaidi ya wetu.
Unajikanganya!Japo pia maswali yanafaa yapate majibu ili kubaini uzembe uliosababisha huo mkasa.
Utakua umedandia bila kusoma nilichokiandika, unaonekana huna hata habari nini kinazungumzwa kuhusu. Ukanda wote huu hamna jeshi la wana maji lenye uwezo zaidi ya wetu.
Tangu hilo gari lizame na huyo mama, kuna Watanzania wamekua wakibeza sana kama kwamba wanashangilia tukio na ingekua furaha sana kwao kama juhudi za uopoaji zingeshindwa kufaulu, roho nyeusi kupita maelezo, wao wamesahau huko kwao kipindi cha mkasa wa MV Nyerere kuna watu wangeokolewa ila kwa ukosefu wa taa usiku, ilibidi waachwe wafe tu ili miili yao iopolewe, na pia haikuopolewa yote, kunao wengi waliachwa waliwe na samaki.
Inategemea uwezo wa kutumia ubongo na kudadisi huu mkasa wa Kilifi ulikua kwenye mazingira gani, kina cha mita 50 na mzunguko mrefu wa mraba, ukizingatia hayo maji yana kitu tunaita 'rapid under current', hiyo ina maana gari halikuzama moja moja kwenda chini, lilisafirishwa humo humo ndani na kupelekwa mbali, pia kuna kitu kinaitwa 'zero visibility', ilibidi watumie special vision equipment maana kwa macho ya kawaida hauwezi kuona kitu.
Nguvu na gharama nyingi zilitumika kuopoa maiti ya huyo mama, ni faraja kuona serikali yetu inaweza kwenda hatua zote hizo kuopoa maiti ya Mkenya mmoja.
Japo pia maswali yanafaa yapate majibu ili kubaini uzembe uliosababisha huo mkasa.
Nchi karibu zote za Afrika ziko dhaifu sana ktk kupambana NA majanga au ajali za kwenye maji, suala Hili lipo wazi NA Ni ukweli mchungu.Hakuna vituo madhubuti vya dharula za kupambana NA ajali za ghafla.Lakini Ni ukweli mchungu pia kuwa kwenye ajali hii ya kuzama hilo gari ktk feri ya Likoni, Kenya imeonyesha uzembe mkubwa zaidi.Uzembe mkubwa sana ulifanyika ktk kuokoa uhai WA yule mama NA mwanaye, kulikuwa NA muda WA kutosha tu WA kuweza kuokoa uhai wao kwani ile gari haikuzama ghafla tu Mara moja kama nanga
Wahusika WA kitengo cha uokozi kwenye hiyo feri wanatakiwa kuwajibishwa bila kuwaonea huruma kutokana na uzembe mkubwa waliofanya kwenye tukio hilo.