Nkobe
JF-Expert Member
- Feb 17, 2013
- 2,204
- 3,277
Kama ningekuwa mwalimu nikatambua kuwa mbunge anaingiza si chini ya milioni 8 kwa mwezi, anamiliki v8 ndani ya miezi mitatu baada ya uchaguzi, anapewa sitting allowance ya laki mbili, anapewa perdiem mamilioni ya kwenda malaysia kuangalia kilimo cha mpunga wakati mbunge si afisa kilimo (afundishi wakulima), baada ya miaka mitano akistaafu anapwa milioni 50 mimi nimetumikia miaka 30 napewa milioni 13. Nisingekubali kufundisha kwa bidii
Mimi mwalimu nalipwa laki 3 wakati maisha ya hapa mjini kodi ya nyumba laki na nusu kwa mwezi, chakula bei juu, mavazi bei juu, shule bora kwa mwanangu ada milioni 1 kwa mwaka, kwa hali hii nisingefundisha kwa bidii
Wakati niko darasani nafundisha naingiwa na kumbukumbu kuwa niliomba kuongezewa mshahara lakini Serikali ikanipeleka mahakamani. Wakati huohuo nasikia kuwa walioninyima nyongeza ya mshahara wamepeleka mabilioni ya pesa uswis, kwenye mikataba ya gesi Mtwara tayari wamevuna mabilioni ya pesa na kuyakimbizia nje ya nchi. haaa, nisingefundisha kwa bidii
Naingiwa kumbukumbu kuwa kwenye change ya rada wanafunzi wangu wangeletewa vitabu angalau wanafunzi wangu wafanye home work zao vizuri, lakini mpaka sasa sisikii tena hizo pesa zimekwenda wapi. Hii ingenipunguzia kasi ya kufundisha
Nikiwa naandaa leson plan, nasikia mbunge wangu aliepewa uwaziri amejenga nyumba ya dola 400,000 (sawa na milioni 600) na hakuna hatua imechukuliwa kweli nakata tamaa ya kufundisha.
Nikiwa napata ugumu jinsi ya kubajet mshahara wangu wa laki 3, mara nasikia kiongozi wangu mabilioni ya fedha anayaita vijisent.Hii nayo inanikatisha tamaa ya kufundisha kwa bidii
Mimi mwalimu nalipwa laki 3 wakati maisha ya hapa mjini kodi ya nyumba laki na nusu kwa mwezi, chakula bei juu, mavazi bei juu, shule bora kwa mwanangu ada milioni 1 kwa mwaka, kwa hali hii nisingefundisha kwa bidii
Wakati niko darasani nafundisha naingiwa na kumbukumbu kuwa niliomba kuongezewa mshahara lakini Serikali ikanipeleka mahakamani. Wakati huohuo nasikia kuwa walioninyima nyongeza ya mshahara wamepeleka mabilioni ya pesa uswis, kwenye mikataba ya gesi Mtwara tayari wamevuna mabilioni ya pesa na kuyakimbizia nje ya nchi. haaa, nisingefundisha kwa bidii
Naingiwa kumbukumbu kuwa kwenye change ya rada wanafunzi wangu wangeletewa vitabu angalau wanafunzi wangu wafanye home work zao vizuri, lakini mpaka sasa sisikii tena hizo pesa zimekwenda wapi. Hii ingenipunguzia kasi ya kufundisha
Nikiwa naandaa leson plan, nasikia mbunge wangu aliepewa uwaziri amejenga nyumba ya dola 400,000 (sawa na milioni 600) na hakuna hatua imechukuliwa kweli nakata tamaa ya kufundisha.
Nikiwa napata ugumu jinsi ya kubajet mshahara wangu wa laki 3, mara nasikia kiongozi wangu mabilioni ya fedha anayaita vijisent.Hii nayo inanikatisha tamaa ya kufundisha kwa bidii