Kwa nini Afrika inazidi kuporomoka huku Asia ikizidi kupaa?

Noor

Senior Member
Joined
Feb 5, 2012
Posts
146
Reaction score
49
Ukipitia maandiko mengi ya uchumi yanasema miaka ya sitini nchi nyingi za bara la Asia, zilikuwa na uchumi level moja na nchi nyingi za kiafrika kiuchumi. La kushangaza hivi leo wao kwetu ni maboss! sisi tumekuwa watu wa kuwapigia magoti. Tujiulize wao waliwezaje na sisi tunashindwaje?
 
Mkuu swali hili watu huwa wanalipa majibu mepesi kama yaliyotangulia hapo juu, lakini ambacho wenzetu wamefanya na ambacho sisi hatufanyi ni kwamba wenzetu wamewekeza kwenye technology. Bila teknology hatuwezi kufika huko. Wameanzisha research and develpment institution ambazo ziko integrated na manufacturing. Taasisi za namna hii zinawawezesha kukifanyai vitendo kile ambacho wamekisoma na kukibuni na kinazalishwa kwenda kwa mtumiaji wa mwisho.

Sisi hatujiwekei malengo kama wenzetu, hawa Asian countries wanasoma kwa malengo fulani lakini sisi tunasoma bila malengo ndo maana unakuta madoctor na maprof. wanaongeza vipatao vyao kwa kuanzisha bar, kufuga kuku, kujenga guest house n.k

Inatakiwa tujiwekee malengo kwa mfano kwamba kufikia mwaka fulani nchi ijitosheleze kuzalisha trekta ndogo kwa ajili ya wakulima wetu, tuzalishe vigae vyetu wenyewe, tuunde gari letu wenyewe n.k. Kwa kufanya hivyo tutaandaa wataalamu wa kuwezesha kufikia malengo hayo. Bila malengo makubwa kama hayo hatuwezi kufika popote.

Kwa hiyo ndugu yangu hakuna mmujiza, Asia walifanya hivyo wakajikuta wanazalisha ziada ya kuuza nje ya nchi wakaongeza foreign reserve zao, watu wao wakapata ajira na maisha yao yakaboreka.

Sisi tumeuza viwanda vyote, tukajitoa kwenye public investment na World bank wakatuletea structural adjustment program ambayo ndo inazidi kutufanya masikini zaidi.

To conclude research and development integrated with manufacturing is the answer, what we need and what is mostly lacking in Africa is a visionary leadership to know what i am talking about.
 
Vyooooote tutaongea lkn msingi Mkuu ni uongoz, hakuna cha maana kinachofanyika chini ya uongozi wa hovyo, uongoz usiokua na maono. Viongoz wetu karibu wote afrika hakuna kitu wanachukua madaraka bila kuwa na vision na dhamira ya dhati kusimamia shughuli za maendeleo. Vingine ni nyongeza lkn zenye tija ktk kuleta maendeleo. Mfano elimu, unapokutana na profesa anashindana na mwanafunzi wa mwaka wa kwanza unategemea nn!? kiujumla elimu hovyo, wafundishaji hovyo tegemea kupata zao hovyo.
Uvivu uliojengeka miongoni mwetu nayo issue. Hatutaki kujishughulisha vyakutosha tumezoea kufanya kazi kwa mazoea, hatutaki kujifunza zaidi na kubwa wabunifu bila kukata tamaa.
Nidhamu mbaya ya fedha,
Na mengineyo mengi
 

Ni kweli uongozi ni tatizo lakini na sisi wananchi tusilaumu kwa lugha ya jumla jumla tu ya uongozi mbovu lazima tuseme ni kitu vitu gani hasa viongozi wafanye ili nchi iweze kuendelea.
 
 
Asia imewekeza ktk elimu tena kwa kutumia lugha zao za asili. Mfano mzuri ni South Korea katika kila watu 100 watu 68 Wana elimu ya chuo kikuu. Hali hii inaongeza tija na ufanisi sio tu ktk sekta ya umma bali hata kwenye sekta binafsi. Afrika (kusini mwa jangwa la Sahara) katika kila watu 100 watu 3 Wana elimu ya chuo kikuu. TZ 38% ya watu hawajui kusoma na kuandika.
Ni bara la Afrika pekee ambapo wizi na mafisadi Wanashangiliwa. Ndio maana haishangazi kuona bara hili ndilo lenye kuongoza kwa umaskini. Mwaka 2013 pesa zilizoingia kwenye mzunguko wa rushwa ni trilioni zaidi ya 1 US$. Hali hii inaongeza inachochea udumavu wa maendeleo na URASIMU.
Ni kweli tuna tatizo la kutokuwa na viongozi wenye maono. Lakini tatizo hili ni la jamii kwa ujumla wake kwani jamii hupata viongozi inaowasitahili. Viongozi hao ni tunda la jamii yetu kwani jamii ya waongo hupata viongozi waongo.
Mipango mingi inayotekelezwa inatoka nje ya Africa na tunaletewa na wahisani kama IMF, EU, USAID WORLD BANK N.K. Hata ya hapa nchini ni Ups down mf: BRN.
 
Nakubalianana aliyesema point ya R&D japokuwa pia huwa inakuwa na gharama kubwa.
Mimi naona pia utegemezi wa misaada kutoka nje katika budget yetu. Tena hata watoa misaada wenyewe wanatudekeza kwa kutokutubana sana ili tuonyeshe jinsi tulivyotekeleza miradi tuliyop[anga na kupeleka mikakati na mipango kuwa lini tutajitegemea.
Pia kizazi cha vijana kimesaauhuliwa sana. Naamini tukiamua kuinvest kwa vijana na Talent development tutafika mbali kama nchi.
 
Ukweli ni kuwa waafrika tuna asili ya uvivu na kuridhika mapema...vile hatupendi kujituma kazini....mwafrika ukimuhamasisha kazi anakuona unamnyanyasa au unamtesa yaani kila kazi mpaka umsimamie....wengi wetu tunaishi kwa sababu tupo hai...nimefanya kazi na hawa watu hasa hasa wachina..kiukweli jamaa wanastahii kuwa hapo walipo kwa kuwa wanajituma sana na wanafanya kazi kama watumwa na kwa bidii sana kwa kuwa wanaamini maisha hayana shotikati.....sisi waafrika tunapenda shotikati
Tunapenda kurahisisha mambo...na kuyachukulia mepesi....hatupendi kufanya kazi na tukifanya kazi hatukawii kuridhika kwa vitu vidogo....
Mwafrika au mtanzania akipata gari na nyumba kwake yeye ndio kilele cha mafanikio.....hapo ataanza kufuga kitambi na kuzaa watoto mfululizo.....
Nimejifunza mengi sana kutoka kwa hawa jamaa.....
POOR AFRICA...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…