Kwa nini 'articles' kwenye Lugha ya Kiswahili zinajitokeza kwa hali ambayo siyo rasmi?

Kwa nini 'articles' kwenye Lugha ya Kiswahili zinajitokeza kwa hali ambayo siyo rasmi?

hata mimi

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2017
Posts
1,356
Reaction score
1,442
Habari...
Kiswahili ni Kibantu, lugha nyingi za kibantu zina articles zao kama ilivyo kwa lugha zisizo za kibantu. Sasa huwa najiuliza sana ni kwanini Lugha ya Kiswahili inakosa articles rasmi badala yake zinajitokeza katika hali ambayo si sanifu mfano article huwa zinajitokeza katika kutukuza na kutweza/kubeza tu?

Kutukuza/kukubwaisha
Kisu.... likisu
Jiwe... mjiwe
(M)toto... litoto
Shule... mishule
Dagaa... madagaa


Kubeza/kudogoisha
Sufuria... kasufuria
Mwiko... kimwiko
Mawe... vimawe
 
Basi unachojaribu kujieleza hakieleweki. Article ni mada. Sasa inshusiana vipi na hayo maneno?
Article sio mada (topic) mzee; ni aina ya kivumishi - huvumisha nomino.
 
Hivi form 3 hukusoma hizi mada? Au bas
 
Back
Top Bottom