Kwa nini Benk zinakuwa na Rate mbaya kuliko Bureau de change

Rate ya dollar inategemea nguvu ya soka yaani muuzaji na muhitaji, Pia kukadiria hali ya soka kesho itakuaje ni rahisi sana, Tambua pale Sisi tunapofunga biashara zetu kuna nchi Ndio kwanza wanafungua biashara hivyo kwa ufupi biashara ya fedha hasa dollar ni 24 hours non stop

Kwa Bank hasa Commercial Bank, wao dollar wanapokea na kuuza kwa wateja hakuna sheria inawalazimisha wawe na akiba Bank kuu ya fedha za kigeni, hivyo Bank moja ikiishiwa inanunua kwa Bank yenye ziada, Sasa gharama za kuuza au kununua inategemea na Bank husika, kuna gharama nyingi za utunzaji, uchakavu pia za ununuzi, Hizo zote zitaongezwa kwenye Standard rate iliyopo. kwa upande mungine Bank inahitaji taarifa Kamili unaponunua au kuuza Lengo ni kukidhi sheria za Fedha zilizopo kuna sheria za utakatishaji fedha yaani money laundering, Sheria zinahusiana na kumfahamu mteja kulingana na Bank kuu husika ili mambo yakiharibika Bank ipate pa kushika na kujitetea,

Kwa upande wa bureau de change, Wao mambo ni tofauti kidogo ingawa siku za karibuni sheria zimeanza kuwabana, sheria ilikuwepo lakini ilikuwa haifutiliwi Sana, kwa sasa wanalazimishwa mambo mengi Sana Ndio maana naona zinalegalega kwa sasa. Wao wanataliwa na Open market, Soko huru Walikuwa hawatonzi Exercise duty mtu akinunua dollar hivyo gharama zilikuwa chini za uendeshaji
 
sawa mkuu,,, nimekuelewa
 
Kaka hii folex account inakuwaje kuwaje mkuu naweza kunufaika
Namaanisha mtu anaweza kufungua akaunti ya fedha ya kigeni eg usd,,pound au euro mostly,,anaweka na kutoa kama kawaida,,vigezo ni tofauti kufuatana na bank husika but kwa bank kama yangu mfano account ya usd unakuja na cash initial deposit isiyopungua usd 100,,Id,barua ya utambulisho na picha,,then tunakufungulia usd account
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…