Kwa nini Hersi anawatamani sana watu waliopo Simba?

Kwa nini Hersi anawatamani sana watu waliopo Simba?

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Ukiwa na aibu kuna mambo fulani utajizuia kufanya mbele za watu hata kama unatamani sana na una haki ya kuyafanya.

Miaka hii miwili matatu tunaona wimbi la watu kutoka Simba kuelekea Yanga kwa kurubuniwa na Rais wao aliyekataliwa na mahakama Hersi Said. Imekuwa kama lile wimbi la "waunga mkono juhudi" enzi zile.

Tukianza kutoa mifano, haikuleta maana kwa Yanga kumrudisha Morrison kipindi kile ila alirudi na mwisho wa msimu ikaonekana haukuwa uamuzi mzuri sana ingawa mimi naamini goli lake kwenye CAFCL lilichangia sana Yanga kuvuka hatua inayofuata.

Tukaja kwa Haji Manara. Ni kwenye siasa zetu pekee ndiyo unaweza kukuta kile tulichokiona kwa Manara. Aliikandia sana Yanga, walipata kila aina ya kejeli ila alipoondoka Simba, tukashangaa amepokelewa upande wa pili.

Msimu uliopita akamleta Augustine Okrah pamoja kujua sababu zilizomuondoa Simba. Matokeo yake Okrah akapotea mazima na sijui kama alicheza hata mechi 5.

Tumefika kwa Clatous Chama. Huyu amemtamani kitambo sana na nafikiri msimu huu hata asiposhinda chochote, kitendo tu cha kumpata Chama ni kama anajiona ameshatimiza ndoto zake. Nimeangalia interview yake kule Afrika Kusini, kajisifu sana kumsajili Chama.

Kuna Baleke. Huyu naona kama wanagwaya kutamba naye ndiyo maana mpaka leo utambulisho rasmi haujaja.

Nasikia Kibu naye huyooo inasemekana anaenda vyurani. Huyu Kibu alipokuwa Mbeya City, Yanga walimteka ili kumsajili akawatoroka akaenda kusajili Simba na kwa maneno ya Kibu mwenyewe Hersi ndiyo alikuwa injinia wa zoezi zima la kutekwa kwake, pun intended. Inaonyesha hii ilibaki kuwa ndoto ya Hersi kuwa na Kibu.

Na kuna watu wengine wakiwemo viongozi ambao ninafahamu Hersi ameshawahi kujaribu kuwavuta upande wa pili. Kwa wachezaji waliobaki naamini kuna siku atamvuta Mohamed Hussein Zimbwe. Ni suala la muda kabla hatujamsikia Aubin Kramo na Moses Phiri upande ule. Pia sitashangaa kama siku moja hatamchukua Miqssone.

Hii obssession kwa watu wa Simba inasababishwa na nini? Kama anadhani ataibomoa Simba kwa njia hii nadhani anapoteza muda wake na pesa za klabu. Apunguze mapenzi binafsi yaliyojificha kwa Simba, ajue Wazee wa Yanga wanasubiri tu siku yoyote watekeleze amri ya mahakama.

EDIT: Nilimsahau na Jonas Mkude. Huyu alitambulishwa kwa mbwembwe zote kama vile kinda atakayeenda kutikisa nyanja za soka kwa miaka 20 ijayo....
 
Ukiwa na aibu kuna mambo fulani utajizuia kufanya mbele za watu hata kama unatamani sana na una haki ya kuyafanya.

Miaka hii miwili matatu tunaona wimbi la watu kutoka Simba kuelekea Yanga kwa kurubuniwa na Rais wao aliyekataliwa na mahakama Hersi Said. Imekuwa kama lile wimbi la "waunga mkono juhudi" enzi zile...
Comments reserved
 
Ukiwa na aibu kuna mambo fulani utajizuia kufanya mbele za watu hata kama unatamani sana na una haki ya kuyafanya.

Miaka hii miwili matatu tunaona wimbi la watu kutoka Simba kuelekea Yanga kwa kurubuniwa na Rais wao aliyekataliwa na mahakama Hersi Said. Imekuwa kama lile wimbi la "waunga mkono juhudi" enzi zile...
Ajib, Kakolanya, Gadiel, Morrison mkapora hawa wachezaji baada ya kugundua Yanga watawasajili, Mugalu, Kagere, Bwalya na Inonga, hiyo inaitwa kumnyong'onyeza adui yako
 
Ukiwa na aibu kuna mambo fulani utajizuia kufanya mbele za watu hata kama unatamani sana na una haki ya kuyafanya.

Miaka hii miwili matatu tunaona wimbi la watu kutoka Simba kuelekea Yanga kwa kurubuniwa na Rais wao aliyekataliwa na mahakama Hersi Said. Imekuwa kama lile wimbi la "waunga mkono juhudi" enzi zile...
Hata CEO Senzo walimvuta utopoloni.
 
Yanga ya sasa ni Simba B,GSM family wote ni Simba, Bakhresa ni ni Simba kwa ufupi Top cream ote nimnyama
 
Siyo wachezaji na viongozi hata akiona timu yoyote inapambana na Simba anaunga nayo urafiki.
As vita, Kaizer Chief, Sevilla, Cska Moscow. Hata Afrika super league alipoona Simba kaalikwa akaanza kujipenyezapenyeza.
 
Siyo wachezaji na viongozi hata akiona timu yoyote inapambana na Simba anaunga nayo urafiki.
As vita, Kaizer Chief, Sevilla, Cska Moscow. Hata Afrika super league alipoona Simba kaalikwa akaanza kujipenyezapenyeza.
Ni kweli kabisa. Anatembea mule mule inapopita Simba. Labda hajiamini sana kukubalika kwake ndani ya Yanga anaona akifanya hivyo atawafanya wenye Yanga yao wamuone mtu wa maana, maana zamani mchezaji kutoka timu moja kwenda nyingine kati ya hizi timu mbili ilikuwa big deal siyo kama sasa.
 
Ukiwa na aibu kuna mambo fulani utajizuia kufanya mbele za watu hata kama unatamani sana na una haki ya kuyafanya.

Miaka hii miwili matatu tunaona wimbi la watu kutoka Simba kuelekea Yanga kwa kurubuniwa na Rais wao aliyekataliwa na mahakama Hersi Said. Imekuwa kama lile wimbi la "waunga mkono juhudi" enzi zile...
Usimu under rate Hersi.
Hersi kwa kutumia pesa kutoka kwa mafisadi papa yaliyo na yaliyokuwa serikalini,wanatumia mabilioni ya pesa kuua brand ya Simba kwa namna nyingi.

Wachezaji wanashawishiwa wacheze chini ya kiwango na kwa kuwa wao ndio wanawashawishi,wanaujua vizuri uwezo wao na ndio maana wanawasajili.
 
Usimu under rate Hersi.
Hersi kwa kutumia pesa kutoka kwa mafisadi papa yaliyo na yaliyokuwa serikalini,wanatumia mabilioni ya pesa kuua brand ya Simba kwa namna nyingi.

Wachezaji wanashawishiwa wacheze chini ya kiwango na kwa kuwa wao ndio wanawashawishi,wanaujua vizuri uwezo wao na ndio maana wanawasajili.
Simu under rate. Najua nguvu iliyo nyuma yake ni kubwa sana lakini kwa kuwa yeye ndiyo yupo front inabidi tumjadili yule tunayemuona.
 
Tumefika kwa Clatous Chama. Huyu amemtamani kitambo sana na nafikiri msimu huu hata asiposhinda chochote, kitendo tu cha kumpata Chama ni kama anajiona ameshatimiza ndoto zake. Nimeangalia interview yake kule Afrika Kusini, kajisifu sana kumsajili Chama.
Mkuu huna taarifa sahihi kuhusu Chama.
Msimu huu Chama ndie kaitaka Yanga . Kitu unachotakiwa ujue Chama na Hersi ni marafiki wa nje ya uwanja kwa muda mrefu.

Urafiki wao ni wa kusaidiana kwa lolote na imesimama hivyo kwa kipindi chote Chama yuko simba. Nakubali Hersi alikuwa anaonyesha kumtaka Chama, lakini ni kibiashara zaidi kwa swahiba yake ndio maana hawakuwa wanaweka figisu sana.

Wakishaona amewekewa dau zuri na Simba wanapotezea ila this time ni Chama mwenyewe aliomba kubadilisha upepo na ndie alitoa hata tarehe ya kutambulishwa.
 
Usimu under rate Hersi.
Hersi kwa kutumia pesa kutoka kwa mafisadi papa yaliyo na yaliyokuwa serikalini,wanatumia mabilioni ya pesa kuua brand ya Simba kwa namna nyingi.

Wachezaji wanashawishiwa wacheze chini ya kiwango na kwa kuwa wao ndio wanawashawishi,wanaujua vizuri uwezo wao na ndio maana wanawasajili.
Hii ni fact au mawazo yako?
 
Back
Top Bottom