Kwa nini kabila la Wakurya bado wana mila za kizamani za kuwachagulia watoto wao wake/waume?

Vituka

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2011
Posts
2,266
Reaction score
1,264
Naombeni ushauri wana jammii. Nimeishi na mwanaume wa kikurya kwa miaka saba sasa na tuna mtoto mmoa. Familia ya mwanaume huyu ni ya ajabu sijawahi kuona!Ndugu na wazazi wake ni watu wa ajabu kiasi kwamba nashindwa kuelezea!Kilichonisikitisha ni kitendo cha kuzuia harusi iliyokuwa ifanyike mwisho wa mwaka huu, sababu eti kwanza mie msomi, pili kijana wao akinioa (sio mkurya mwenzie) basi wao watampoteza mtoto wao na hawatapata tena msaada toka kwake. Jamani hebi nipeni mawazo yenu, nifanyeje?
 
Duh!!me najipitia zangu tu.
 
mmh! nakuombea dada angu hakuna linaloshindikana kwa maombi!!
 
Ikishindikana ng'oa figa weka kitandani kwa mama mkwe hapo umewaweza hawakufukuzi ng'o. Mi mkurya najua mila na desturi zetu. Ila hao bado wako nyuma ya wakati maana siku hizi hayo mambo yamepungua sana ukuriani.
 

Sikubaliani nawe kwani hayo unayoyasema ume-generalize tu.
 
Huo ni mfano hai ulonitokea mimi, nina mifano ya watu watano pia yamewatokea kama hayo!! To be honest, hili kabila bado linahitaji elimu! Angalia mfano wa female genital mutilation, bado wanapractice hayo mambo! Kweli nawaambia huyu mama mkwe mngepata kumuona physically I swear ungemchapa viboko! :hatari:
 
Ha ha ha, mama mkwe hana shukurani hata chembe!! Wiki moja kabla hajaleta hizo habari, nimemtumia Laki mbili amalize matatizo yake madogo madogo!Ntang'oa figa niweke kitanda na bado atantafia majambazi wani geche! Ha ha ha!
 

They look like this........usually.....this is my own inlaw

 

Hii tabia ya kuongelea kabila zima wakati tatizo ni la familia ya mme wako halikubaliki. Huu ni unyanyapaa au "stereotyping" kwa lugha ya wale wafadhili mashoga. Swali sahih lingekuwa "hivi kwa nini familia ya mme wangu wana mila za kizamani hivi"?
 

hizo ni mila zao, ni utamaduni wao. na wao wanakushangaa wewe kwanini unataka kuolewa na "mkurya"?
wao wakiacha hizo mila manake kabila la wakurya litakuwa limepotea. tunawaita wakurya si yo kwasababu ni wakurya bali kwasababu ya identity yao, na moja ya identity yao ni hayo unayoyaona toka kwa hao wakwe zako.

tunnaposema tuwe makini kuchagua wenza wetu, hatumaanishi ukabila, tunamaanisha ku zuia vitu kama hivyo ambavyo kwa bahati mbaya vinatokea kwako leo
 
 

Kwa karne hii ya 21 sidhani kama bao tunatakiwa kukumbatia mila na destury za aina hii, sio kwa wakrya tu hata kwa makabila mengine. Hata sisi pia makabila yetu yalikuwa na mila za aina hiyo ila kwa sasa wanajamii wameelimika na wameshachana na mila hizo.

Kwa mtindo huu, familia hii haitajikomboa kutoka katika utumwa wa fikra potofu na maendeleo kwao utakuwa ni msamiati kizazi hadi kizazi.
 

Well at least umekuja na statistics kidogo. Kwa hiyo ukichukua wewe jumlisha hao wengine watano mnakuwa jumla watu sita. Sasa kama kweli uko objective unaweza kutumia mfano wa watu sita kuhukumu kabila zima lenye idadi ya watu takriban laki tano? Je kuna kabila nchi hii ambalo limeshiba elimu na halihitaji kabisa? Kwa taarifa yako female genital mutilation ni tatizo la makabila mengi tu hapa nchini we fanya utafiti mdogo tu utapata majibu.
 
 
Ikishindikana ng'oa figa weka kitandani kwa mama mkwe hapo umewaweza hawakufukuzi ng'o. Mi mkurya najua mila na desturi zetu. Ila hao bado wako nyuma ya wakati maana siku hizi hayo mambo yamepungua sana ukuriani.

wewe siyo mukurya,nyakebhono,unatuharibia mila zetu urumurisya/oghosaghane.
 

thanks ! Mkuu..kwani si ukaolewe na mchagga mwenzio? Na jf trust me,huyu dada ni mchagga tu,wakurya na wachaga ni vitu viwili tofauti sana linapokuja suala la ndoa.
 
wewe siyo mukurya,nyakebhono,unatuharibia mila zetu urumurisya/oghosaghane.

Umurisya ono omokangi sana mura yani no obhokangi akogamba hao..wivu tu..kurya the great tribe we are proud of being kuryans..asietupenda ajinyonge...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…