Kwa nini serikali inawahamisha wananchi wanaoishi kwenye Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro?

Kwa nini serikali inawahamisha wananchi wanaoishi kwenye Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro?

LAZIMA NISEME

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2015
Posts
240
Reaction score
267
Kuwahamisha wananchi wa jamii ya Kimasai katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro ni suala lenye uzito wake kwa taifa linaloweka maslahi mapana ya utunzaji wa mazingira. Baadhi ya sababu ni kama ifuatavyo:-

Uhifadhi wa Mazingira, Serikali inawahamisha wananchi kwa lengo la kuhifadhi mifumo ya ikolojia na wanyamapori katika hifadhi hiyo. Kwa kuondoa shughuli za kibinadamu zinazofanyika katika hifadhi hiyo kama vile, ufugaji wa ng’ombe au kilimo cha jadi, hivyo kwa kufanya hivyo kuna uwezekano wa kupunguza uharibifu wa mazingira.

27.jpg

Kukuza Utalii, Ngorongoro ni moja ya maeneo ya utalii wa kimataifa. Serikali inawahamisha wananchi hao ili kuweza kutunza hifadhi na kuongeza faida za kiuchumi kupitia utalii. Hii ni njia ya kuwapa maisha bora wananchi kwa kuhamasisha shughuli zinazohusiana na utalii badala ya ufugaji.
ngorongoro-crater-is.jpg

Mkataba wa Kimataifa, Hifadhi ya Ngorongoro ni eneo lililosajiliwa kama Urithi wa Dunia na inaweza kuhitaji kutekeleza mikataba ya kimataifa ya uhifadhi. Hivyo, Kitendo hicho kinachagiza Serikali kuwahamasisha wananchi kuhamia maeneo mengine ili kulinda urithi wa asili.
simba-pic.jpg

Usalama wa Watu na Wanyama, Katika maeneo ambayo kuna wanyama wakali kama simba, Chui na fisi, kuhamisha jamii za watu wanaoishi karibu na maeneo hayo kunaweza kusaidia kupunguza vifo vinavyotokana na wananchi kuuawa na wanyama hao wakali.
 
Acha uongo
Hao Masai wapo hapo Toka Dunia inaumbwa
Mbona hawahamishi warugulunMikumi,
Mbona hawahamishi wakurya Serengeti
Mbona hawahamishi waarusha Arusha
 
Kuwahamisha wananchi wa jamii ya Kimasai katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro ni suala lenye uzito wake kwa taifa linaloweka maslahi mapana ya utunzaji wa mazingira. Baadhi ya sababu ni kama ifuatavyo:-

Uhifadhi wa Mazingira, Serikali inawahamisha wananchi kwa lengo la kuhifadhi mifumo ya ikolojia na wanyamapori katika hifadhi hiyo. Kwa kuondoa shughuli za kibinadamu zinazofanyika katika hifadhi hiyo kama vile, ufugaji wa ng’ombe au kilimo cha jadi, hivyo kwa kufanya hivyo kuna uwezekano wa kupunguza uharibifu wa mazingira.

View attachment 3074259Kukuza Utalii, Ngorongoro ni moja ya maeneo ya utalii wa kimataifa. Serikali inawahamisha wananchi hao ili kuweza kutunza hifadhi na kuongeza faida za kiuchumi kupitia utalii. Hii ni njia ya kuwapa maisha bora wananchi kwa kuhamasisha shughuli zinazohusiana na utalii badala ya ufugaji.
View attachment 3074260
Mkataba wa Kimataifa, Hifadhi ya Ngorongoro ni eneo lililosajiliwa kama Urithi wa Dunia na inaweza kuhitaji kutekeleza mikataba ya kimataifa ya uhifadhi. Hivyo, Kitendo hicho kinachagiza Serikali kuwahamasisha wananchi kuhamia maeneo mengine ili kulinda urithi wa asili.
View attachment 3074261
Usalama wa Watu na Wanyama, Katika maeneo ambayo kuna wanyama wakali kama simba, Chui na fisi, kuhamisha jamii za watu wanaoishi karibu na maeneo hayo kunaweza kusaidia kupunguza vifo vinavyotokana na wananchi kuuawa na wanyama hao wakali.
Siyo tu hifadhi ya Taifa. Ngorongoro ni urithi wa dunia.

Haiwezi ikaharibiwa na wajivuni wachache.
 
Serikali inawahamisha wananchi hao ili kuweza kutunza hifadhi na kuongeza faida za kiuchumi kupitia utalii.
Hao hao Wamasai ni kivutio cha utalii kutokana na mila zao, mavazi, nk. Wasikilizwe bhana..
 
Hii ni insha iliyo andaliwa na mtoto wa darasa la saba bila shaka
 
Waondoke tu,

Mbona wasukuma wamezungukwa na hifadhi kibao ila hawaruhusiwi kuingiza mifugo? Wao ni kina nani hadi waruhusiwe kufuga kwenye hifadhi?

Mbona hao wafugaji wengine wanaotaabika na mifugo yao kutaifishwa hakuna anaepiga kelele?

Kama wataruhusiwa kuendelea kufuga ndani ya hifadhi, matabaka mengine yaruhusiwe pia kuingiza mifugo kwenye hifadhi zilizowazunguka.
 
Kwa mazingira ya eneo lile ni sahihi kabisa wahamishwe,tatizo ni kuwa Serikali inatumia sababu ya ecology kuwahamisha huku Wakikaribisha wawekezaji wa kigeni katika hayo hayo maeneo.
Hapa ndio shanzo cha tatizo.
 
Serikali ya TZ Isha hamisha sana watu kwa manufaa ya umma.
Wakati wa kuanzisha vijiji vya ujamaa watu walihamishwa.

Pia vijiji vingi tu vimewahi kuhamishwa.
Ilimradi tu uhamisho ufanywe kwa kutingatia kanuni zilizo wekwa.
Ngongoro ni lazima ihifadhiwe kwa maslahi ya Taifa.
Kuongezeka sana kwa watu wakiwa na WA nchi jirani kufuata malisho ya mifugo kungeiharibu kabisa hifadhi hiyo muhimu.
Naunga mkono
 
Ngorongoro iwe eneo maalum lenye restricted access. Hawa wamasai waliacha kuchunga mifugo wakawa wanakesha kutongoza wazungu, na kujikoki na mikuyati, hovyo kabisa
 
Wamasai sio special case,
Kuachwa hapo watajaa sana na kuharibu uoto,
Tukiacha siasa hawa jamaa waondolewe tu
Naunga mkono hoja . Ngorongoro ilikuwa inafutika .....jamaa walifikia hatia ya kujenga nyumba za bati kabisa katikati ya hifadhi
 
Bado sijawaelewa hapo, kwamba wamasai watolewe kwenye hifadhi ili waarabu waingie kusaidia uhifadhi?!
 
Back
Top Bottom