Kwa nini TFF hawataki Yanga na Simba kucheza Chamazi?

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,703
Reaction score
1,724
Azam FC wana kiwanja tena cha kisasa na CAF bosi wa TFF wameidhinisha mechi zao kuchezwa hapo. Ajabu TFF hataki Yanga na Simba kucheza hapo kama uwanja wa nyumbani wa Azam kama kanuni zinavotaka kunani?
Nahisi ni masuala ya pesa tu na wanene wamelenga kunufaika hasa kwa kuwa uchaguzi umekaribia. Mfano ni ung'ang'anizi wa mechi ya Azam na Simba jumamosi hii!
 
Pesa mwana haramu, me kwa kweli hili siliafiki kabsa, viongoz wameweka agenda ya Pesa mbele kuliko Mpira. na wanasingizia usalama kitu ambacho hakipo.
 
raisi wa TFF kua mwenyekiti wa TFF mkoa wa Kagera kwa pamoja hilo umeshindwa kulishangaa?
 
TFF hawana hoja za msingi. Haiwezekani uwanja unaoandaa mashindano ya Africa ushindwe kuandaa mechi ya ligi ya soka kwa kile kinachoitwa sababu za kiusalama. Nafahamu ilivyo rahisi kuandaa mechi Uwanja wa Taifa kuliko Chamazi lakini pia ni vizuri Azam wakalipwa 'fao' lao la kumiliki uwanja. TFF na bodi ya ligi lazima iweke masharti mapema ya mechi kubwa za ligi kuchezewa Chamazi ili Azam itekeleze au ishindwe kutekeleza kwa hasara yao wenyewe.
 
Capacity ya uwanja ni ndogo chamazi pia hali ya usalama wa RAIA na weachezaji na LA mwisho ni kwamba TFF wanategemea Sana hizi timu mbili simba na yanga ili kuingiza kipato katika viingilio hivyo basi uwanja wa azam hautoingiza mashbiki wa kutosha kutokana na udogo wake.. Ni mtazamo wangu
 
Hilo la uwanja wa Chamazi kusingiziwa kuwa mdogo nalikataa kabisa, ni kipimo gani wamekitumia? Angalia mechi za timu za Yanga na Simba zinapocheza na timu nyingine idadi ya watazamaji uwanjani ni aibu.
 
Pesa mwana haramu, me kwa kweli hili siliafiki kabsa, viongoz wameweka agenda ya Pesa mbele kuliko Mpira. na wanasingizia usalama kitu ambacho hakipo.
Hilo la usalama Polisi ndo walipaswa kutamka lakini kwa wao TFF kuingilia kazi hizo ni kulidhalilisha jeshi letu.
 
Mie ni mshabiki wa Yanga lakin kwa suala hili TFF wanawaonea sana Azam. Kama wamekubali viwanja vya mikoani tena vibovu kweli kwa nn wanawazuia Azam wasiutumie uwanja wao wa chamanzi kwa mechi za nyumbani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…