Kwa nini wafanyabiashara mtandaoni hamjibu wateja wenu?

Kwa nini wafanyabiashara mtandaoni hamjibu wateja wenu?

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Kuna vitu vya ajabu hili nalo ni la ajabu, kuna wafanyabiashara wanafanya biashara kwa kuzitangaza mitandaoni ila wanazima simu, au unakuta wengine hawapokei simu au hawajibu meseji au kusoma jumbe za mitandaoni na kuzijibu ikiwemo maswali hii ni ajabu kabisa.

Hivi hawa wanakuwa hawajui wajibu wao au wanajaribu biashara? Maana unapoamua kufanya biashara kwa njia ya mtandao simu unatakiwa kuwa nayo karibu maana ndio kama injini ya biashara ya kukupatia wateja wako sasa wewe unaweka simu sijui chumbani unaenda kukaa nje nani apokee hiyo simu?

Hebu badilikeni muende sawa na matangazo yenu, unakuta mtu kapost karibu viatu na picha kama zote, bei hajaweka mara oo njoo inbox, nije inbox kufanya nini na ungeweza kuweka kila kitu wazi tukamalizana hapo, au hujaweka mahali pa duka lilipo wala mkoa na meseji za wanaouliza maswali kama bei gani hajibu pia mnakera sana na kufukuza wateja wanaojitambua.

Badilikeni bwana, mnakera mjue mnakera sana.
 
Baadhi yao wanafanya kama mchezo tu. Walio serious wanapiga sana hela kupitia biashara mtandao.
 
Wengi wao hawana elimu ya ujasiliamali, customer care ,na wala hawajui skills za kumhandle na kumretain mteja mtandaoni. Kama Wanawake wanyodo sana wanahisi kila wakati wanatongozwa

Sasa wanajitamgazaga kwa nini, kuna wale wanatangaza biashara hawaweki bei ukiulizwa wanakukimbia inbox. kwa nn wasiwe committed na wanachokifanya tangazs biashara weka bei umeweuka mawasiliano pokea simu kwa wakati jibu maulizo ya wateja. Ila Tz biashara ya mtandaoni bado sana hasa customer care ni zero kabisa
 
Wateja wa bongo nao huwa wanasumbua unakuta tangazo lina Bei anaenda kwenye comment anauliza Bei Halafu bado anapiga kuuliza bei. Biashara mtandao bongo bado.
 
Wateja na nyie miyeyusho, mnapiga simu kuuliza Bei tu na kununua hamnunui.....bei tuiweka kwenye Tangazo ila bado mnapiga simu kuuliza Bei.
Ukiwa na elimu ya huduma kwa wateja ungeelewa kuwa unatakiwa kumjibu kila mtu anayeuliza swali kuhusu biashara yako hata kama umeweka maelezo kwenye biashara.

Kumbuka si kila mtu anasoma kila kitu, na kuna watu wanakuwa hawajaona pages zenu ila wamepewa namba na watu ivyo kulazimika kuuliza taarifa ili wapate taarifa sahihi.

Mfanyabiashara makini hawezo choka kutoa taarifa za biashara yake kwani ni sehemu ya biashara, hao wasumbufu watakusumbua leo, kesho watanunua au kuwapa taarifa watu wengine waje kununua hata kama si wao.
 
Kuna vitu vya ajabu hili nalo ni la ajabu, kuna wafanyabiashara wanafanya biashara kwa kuzitangaza mitandaoni ila wanazima simu, au unakuta wengine hawapokei simu au hawajibu meseji au kusoma jumbe za mitandaoni na kuzijibu ikiwemo maswali hii ni ajabu kabisa.
Bahati yako ulitaka wakupige
 
Hawa watakuwa wameiga ubosi kwenye mitandao huduma kwa wateja (Voda, Tigo, Airtel, Halotel) na mabosi feki wengine.

Baadhi ya watu hudhani kwamba akimpuuza mtu anayempigia simu, ndipo yeye huonekana wa maana na mwenye kuhitajika zaidi.

Watu wa namna hiyo hukadiria heshima yao kulingana na vile ambavyo wanam-ignore mwingine. Shame on you!
 
Wateja wa bongo nao huwa wanasumbua unakuta tangazo lina Bei anaenda kwenye comment anauliza Bei Halafu bado anapiga kuuliza bei. Biashara mtandao bongo bado.
Wateja wa Bongo? Please, tuambie hao wa hapo London wakoje?

NB: Kama unaogopa usumbufu wa wateja, funga tu biashara yako, kazi imekushinda.
 
Back
Top Bottom