Kwa nini watahiniwa wa kujitegemea wanafeli

Joined
Aug 19, 2012
Posts
86
Reaction score
17
Habari wanajamii naombeni msaada wenu katika hili je ni kwanini watahiniwa wa kujitegemea(private candidate) wanafeli sana au kuna upendeleo katika kusahisha na je maksi zao zinatofautiana vp na school candidate yaani katika watu 100 afaulu 1 sio kwamba walikuwa hawasomi
 
Tatizo ni overconfidence na kutojisomea plus lack of determination.!
 
Mm nafikiri inachangiwa na mambo yafuatayo:- private candidate hawana continues assesment ambazo zinachukua 50% hivyo yeye anafanyia marks 100
-kutokaa darasani
-kutojua cha kusoma na cha kuacha
-not committed
-usahihishaji wa mitihani yao often is violently way
-passing mark is above 51(c) o level,bt not sure indeed,mimi nafikiri hizo sababu juu zinapelekea kufeli kwa pc.
 
Wengi hawapo makini na masomo, na unakuta hawana msingi mzuri wa elimu
 
Hawapati athari ya continuous assessments. Tofauti ya P na S katika hili ni kwamba P yeye 100 yake na 0 yake ni siku ya mtihani. Hivyo akifaulu anakuwa amefaulu na kama amefeli amefeli. S wao continuous assessments zinasaidia kustandardize marks zao. Matatizo ya P:1. Wanakosa mwongozo sahihi wa kitaaluma kwa walimu:2. Wanaosoma elimu ya miaka miwili kwa mwaka mmoja au miaka minne kwa miaka miwili hawawazi kuiva kama S aliyefundishwa vizuri kwa miaka miwili au minne:3. Kutojua muhtasari wa masomo (syllabus) hapa huishia kusoma hata mambo yasiyotakiwa.4. Kubanwa na kazi au majukumu ya kifamilia wakati wa maandalizi.5. Kukosa ufahamu wa mifumo mipya ya mitihani, kwa mfano - maswali ya arts siku za leo kwenye essay yanakutaka ujadili pointi chache mfano 4,5,6,7 au 8 kulingana na swali lilivyoulizwa. Hivyo ajibuye mambo mengine na kuongezea kidogo majibu hufeli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…