KWA PAMOJA TUUTOKOMEZE UMASKINI.

KWA PAMOJA TUUTOKOMEZE UMASKINI.

Passion hustler

New Member
Joined
Sep 17, 2021
Posts
1
Reaction score
1
Kwanza kabisa, ninapenda kuihasa jamii kuhusu suala la kufanya kazi (kujishughulisha), ili iweze kuondokana na Uzembe na Umaskini. Pia Wazazi au walezi, wanapaswa kuwafunza vijana wao namna ya kuweza kuyakabili Maisha wakiwa Shule au hata nje ya shule, ili hata wanapohitimu wawe tayari wanajitambua na wala wasiwe ni vijana wanaojihusisha na maadili mabovu,
Ni lazima kwa kila Mfanyakazi au Mfanyabiashara kulipa kodi ili kuiwezesha Serikali katika kuleta Mabadiliko chanya hasa katika Nyanja za kiuchumi na Miundombinu. Na inabidi kila Mfanyakazi au Mfanyabiashara aweze kuwa na Malengo chanya, kwake yeye na kwa Jamii ili faida irejee kwa wote, Asasi za kiuchumi zinapaswa kutoa Mafunzo kwa Wananchi kuhusu Suala la kujikimu kimaisha kwa kujishughulisha na masuala kama ; Ujasiriamali na Uwekezaji, Na Kwa kila Mfanyakazi aliyeajiriwa aweze kuwa mtunzaji na mtumiaji mzuri wa pato lake ili kukwepa hasara itakayoweza kumtupa kwenye Umaskini, pia kujituma katika mwenendo mzuri wa kimaadili kwa mfano: kuwahi kuamka asubuhi na mapema na pia kuwaheshimu watu wa rika zote ili hata anapotaka kufanya jambo fulani kuhusu biashara ya aina yoyote ile, hiyo jamii iweze kumuunga mkono katika mambo yake atakayotaka kuyafanya.
 
Kwanza kabisa, ninapenda kuihasa jamii kuhusu suala la kufanya kazi (kujishughulisha), ili iweze kuondokana na Uzembe na Umaskini. Pia Wazazi au walezi, wanapaswa kuwafunza vijana wao namna ya kuweza kuyakabili Maisha wakiwa Shule au hata nje ya shule, ili hata wanapohitimu wawe tayari wanajitambua na wala wasiwe ni vijana wanaojihusisha na maadili mabovu,
Ni lazima kwa kila Mfanyakazi au Mfanyabiashara kulipa kodi ili kuiwezesha Serikali katika kuleta Mabadiliko chanya hasa katika Nyanja za kiuchumi na Miundombinu. Na inabidi kila Mfanyakazi au Mfanyabiashara aweze kuwa na Malengo chanya, kwake yeye na kwa Jamii ili faida irejee kwa wote, Asasi za kiuchumi zinapaswa kutoa Mafunzo kwa Wananchi kuhusu Suala la kujikimu kimaisha kwa kujishughulisha na masuala kama ; Ujasiriamali na Uwekezaji, Na Kwa kila Mfanyakazi aliyeajiriwa aweze kuwa mtunzaji na mtumiaji mzuri wa pato lake ili kukwepa hasara itakayoweza kumtupa kwenye Umaskini, pia kujituma katika mwenendo mzuri wa kimaadili kwa mfano: kuwahi kuamka asubuhi na mapema na pia kuwaheshimu watu wa rika zote ili hata anapotaka kufanya jambo fulani kuhusu biashara ya aina yoyote ile, hiyo jamii iweze kumuunga mkono katika mambo yake atakayotaka kuyafanya.
Upo sawa kabisa
 
Naona ndugu" MAARIFA " umemsahau, wazungu na warabu walituchukua utumwani kwa sababu ni wachapa kazi wazuri tu. Waafrika hawana maarifa na si tabia ya kujituma.
Mpaka leo karne ya 21 mwafrika anainua jembe la mkono ili kuilima ardhi hizo nguvu za kumtoa kwenye umasikini atazipata wapi ?
Mchina anatumia skaveta kuinua mizigo mwafrika anatimia mwili wake.
Hamasisha watu wawe na maarifa, China wamefika mbali kwa kijifunza maarifa ya kisasa.
 
Back
Top Bottom