Pre GE2025 Kwa Rais Samia kujifanya "Chura kiziwi" ni dharau kwa watanzania. Kwani yupo Ikulu kwa maslahi ya akina nani?

Pre GE2025 Kwa Rais Samia kujifanya "Chura kiziwi" ni dharau kwa watanzania. Kwani yupo Ikulu kwa maslahi ya akina nani?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

G4N

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2014
Posts
4,283
Reaction score
9,925
Rais Samia amekiri kusikia kelele na matusi ya watanzania juu ya sera zake na uongozi wake. Lakini amesema ameamua kujifanya kuwa kama "chura kiziwi" mpaka dhamira yake na lengo lake la litakapotimia.

Katika kauli yake hii nabaini mambo 2:-
1. Ni ule ugonjwa walionao viongozi wengi wa Afrika wa kudhani "cheo ni akili". Hivyo Samia kwa kuwa yeye ni Rais, basi anajiona yeye ndiyo mwenye akili kuliko watanzania wote. Ndiyo maana anapuuza maoni (yeye kayaita kelele) na ukosoaji (matusi) yao.

2. Watanzania wameporwa madaraka yao, hivyo Samia hayuko tena kwenye kiti cha urais ili kuwatumikia. Ndiyo maana kile wanachokitaka kinaitwa kelele na matusi. Kama Rais angekuwa yuko pale kwa kuwatumikia wananchi, basi angefanya kwa kadri wanavyopendekeza.

Siyo mara ya kwanza kwa Samia kutoa kauli ya aina hii. Hata wakati wa sakata la kupinga DP World, alijitokeza na kusema atakaa kimya na kamwe hatojibu chochote. Mwisho wa siku akausaini mkataba wa DP World uliokataliwa na watanzania.

Pia, soma
=>
Rais Samia: Wananitukana ili niwajibu, najigeuza chura siwajibu
 
Mamilioni ya watanzania wanamuunga mkono Mheshimiwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi.hawataki kuona Rais wetu akijibu uzushi ,utoto utoto na uongo wa kupikwa unaokuwa ukitolewa na wanasiasa uchwara waliofirisika na kuishiwa hoja. Wapinzani janja yenu mlitaka muwe mnazusha vitu vya uongo ili muwe mnajibiwa kuwaweka midomoni.

Sasa Rais hana muda huo mchafu wa kujibu uzushi na uongo .yupo Bize kuwatumikia watanzania na kuwaletea maendeleo,kazi ambayo ndio tuliyomkabidhi na kumpatia.hatumlipi mshahara kukaa ikulu kwa ajili ya kujibu uzushi wa wanasiasa uchwara wa CHADEMA
 
Mamilioni ya watanzania wanamuunga mkono Mheshimiwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi.hawataki kuona Rais wetu akijibu uzushi ,utoto utoto na uongo wa kupikwa unaokuwa ukitolewa na wanasiasa uchwara waliofirisika na kuishiwa hoja.
Hao mamilioni wapo wapi na umefanya utafiti gani na lini kuwabaini?!
 
Wewe ni mjinga kweli Urais ni ajira na ajira ni kwa maslahi ya Rais na familia yake siyo maslahi yako na famila yako tafuta ajira na wewe yenye maslahi kwako na familia yako,acha uninga jingeze
 
hivi dhamira yake na lengo lake nn?
Baadhi ni hizi hapa chini..

Inamaana we jamaa unataka kusema Samia hahusiki na haya mabati ya kila sehemu!?
We huoni maraisi wote wa zenji ni awamu hii pekee ndo ina maendeleo ya Kasi zaidi? Kama unabisha subiri Samia atolewe madarakani uone kama utaona Kasi hii iliyopo.

Barabara mpya ya 2020 eti inakwanguliwa na kujengwa tena upya we unafikiri hii ni jeuri ya nani kama si Samia?
 
Unapokuwa Rais ni lazima uwe na msimamo alichosema leo SSH Hakina tofauti na ile hotuba ya Mwalimu Nyerere ya kiongozi kutosikiliza maneno mengi kutoka kila
Upande, “ huyooo , huyooo” lakini Rais anabakia na msimamo ulioimara na usiotetereka.
Nyerere siyo msahafu, kwamba kila alichokifanya ama kutamka basi alikuwa yuko sahihi. Nyerere ni miongoni mwa viongozi wabaya kuwahi kutokea ktk nchi hii. Bahati yake ni kuwa alitawala enzi za giza.
 
Watu wanaomtukana hawafanyi hivyo kukosoa bali mitusi ya nguoni. Mfano mange anasema semia anasagana. Sasa unataka ajibu upuuzi wa mange na upuuzi wa lisu. Keep calm mama ni jibu la wapumbavu akina lisu
Siyo kweli mange ni kisingizio tu. Dp world waraka umesomwa kila kitongoji. Hata katikati ya tusi moja la mange kuna hoja kibao na ukosoaji mwingi ambao unajenga anatoa. Rais mwenye kujali utawala bora angetuliza mizuka na kuyafanyia kazi hayo yanayopigiwa kelele na watanzania.
 
Back
Top Bottom