Kwa Ripoti hii ya CAG, ni dhahiri Sukuma Gang imeshinda mapema mno!

Kwa Ripoti hii ya CAG, ni dhahiri Sukuma Gang imeshinda mapema mno!

Desprospero

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2023
Posts
1,015
Reaction score
2,493
Katika mchezo wa siasa unahitaji kuwa na akili nyingi sana kushinda "game". Lakini akili ya kwanza ni kumsoma, kumfahamu, kumwelewa aliyeketi kwenye kiti cha "executive" anawaza nini, nini hulka yake, ana uwezo gani wa kuona masafa marefu na tabia yake ikoje na ana uwezo gani wa kuadhibu au kusamehe jambo hata kama jambo hilo linaweza si tu kuangamiza Taifa lakini pia kumuangamiza yeye binafsi.

Katika utawala wa Rais John Pombe Magufuli (JPM) wateule wake walifanikiwa sana katika akili hiyo ya kwanza na kwa mantiki hiyo waliambizana na kukubaliana ni nyimbo zipi, mapambio yepi na kauli zipi zilimfurahisha "Mfalme" nao wakamwimbia, wakampambia na kumpa kauli zilizomfurahisha hata kama nyimbo hizo, mapambio hayo na kauli hizo ziliangamiza Taifa. Kazi ya wapambe (chawa) ni kuhakikisha wanapata mkate wao hata kama mwisho wa yote Mfalme atazama.

Kwa akili hiyo, wapambe wa JPM walijikuta wakisomba utajiri wa nchi hii kwa ubabe (si umame) bila hofu ya kuhojiwa. Waliomwabudu Magufuli kwa kicho wameshiba, wamenona kwa namna akaunti zao zilivyojaa noti hata za bandia na damu! Ama kweli, "kila zamu na kitabu chake" alijisemea Mzee Alli Hassan Mwinyi!

Alipoingia madarakani Mama Samia Suluhu Hassan "chawa" wake wakatumia akili ile ile ya kwanza. Wakati Samia Suluhu Hassan akiimba "Kazi Iendelee" wao kwa siri na usadi mkubwa wanaimba, "It's Our Time to Eat" (IOTE) kwa gharama ya wananchi wasakatonge na wadunda kazi. Genge lililoingia na Mama Samia wanawazomea "machawa" wa JPM na sasa wanashindana nani ana pesa nyingi katika akaunti ndani na nje ya nchi.

Mbinu waliyotumia na kufaulu kwa haraka ndani ya siku 720 tu ni kuwaimbisha Watanzania dhana ya Sukuma Gang ili waaminike kumbe ni wimbo sahaulishi ili waibe, wakwapue na kula bila hata kunawa! Hii ni aibu si kwa Taifa balj hata kwa wahisani walioamini kuwa utawala wa Samia Suluhu Hassan ungepambana na rushwa na ufisadi badala yake anaandika historia ya kukubuhu kwa ufisadi kuliko tawala ZOTE zilizotangulia kama kweli CAG Charles Kichere hakusema uongo.

Mabilioni (madudu) yaliyoibuliwa na CAG imeithibitishia Dunia na walimwengu kuwa Samia hana dhamira ya kweli kupambana na ufisadi, hawezi kupambana na ufisadi na mafisadi au naye ni sehemu ya mafisadi. Kwa maana kwamba mafisadi wamemteka nyara kwa kujua au bila kujua.

Kwamba tulipoimba Sukuma Gang wanafanya hiki na kile ililenga kumpumbaza Rais Samia Suluhu Hassan asijue wizi na unyang'anyi wa fedha za umma ulivyokuwa ukisukwa na kufanikishwa! Na katika kulifahamu hili, nani aliamini mkwara aliowachimba wateule wake kuhusu fedha za UVIKO-19 angetoke mwamba asiyeogopa rangi yake wala macho yake kukwapua fedha hizo? Kwani ukinitukana "stupid" hadharani napungukiwa nini ilhali mzigo ninao nakula na kunywa kwa raha zangu na mke/mume wangu?

Samia anaposema, "kula kwa urefu wa kamba yako" wao wanasema, "goli liko wazi ushindwe tu kufunga" huku wananchi masikini hawana hakika walau wa mlo mmoja kwa siku. Wapiga dili wana akili sana! Wamefanikiwa kupasuka nchi vipande viwili: matajiri kupindukia na masikini kupindukia. Tabaka la kati limefutika. Balaa linanyemelea Taifa soon!

Ni wakati wa kila mwananchi kuamka na kukataa aina hii ya uongozi wa kuwaonea haya na huruma mafisadi. Kila mtu aandamane chumbani kwake walau hata kila siku mara moja kumsema vibaya SSH. Mungu ana tabia ya kusikia na kufanyia kazi sauti ya mnyonge mmoja. Hata wasiosoma JF waambiwe kwamba kwa Ripoti hii ya CAG mwaka huu, Sukuma Gang wameibuka kidedea! Wajue kwamba Samia amezungukwa na wezi wenye akili kuliko waliomzunguka Dikteta Magufuli.

Naililia nchi yangu Tanzania!
 
SSH aliangukia pua baada tu ya kuanza kupachika mafisadi kwenye serikali yake, mara walamba asali ,wauza pembe za ndovu nk. Angekuwa na dhamira angetusikiliza ,sasa yako wapi. Sukuma gang haijawahi kukumbwa na hii aibu ya mchana kweupe ,
 
Walituaminisha kuwa wao ni malaika kumbe ndio wataalam wa upigaji.

Rais naye anawaogopa kwa kuogopa kukosa support yao dhidi ya dhana ya Sukuma gang.

Wamemuaminisha kuichukia kitu walichokiita sukuma gang na kumwaminisha kuwa ni wao pekee ndio wenye uwezo wa kupambana nao, nae kawaamini na ili kulinda kibarua chake analazimika kuendelea nao hata wakifanya madudu ili nao wamlinde hapo alipo.

Hapo inatumika tu kanuni ya skratch my back and i will skratch yours.

Wananchi tuendelee tu kuvumilia maana kwa utawala huu tusitegemee hatua yeyote ile kuchukuliwa dhidi ya wezi mafisadi.
 
Tatizo ni kwamba Samia ni mpenda Madaraka wa kupindukia,yeye hajali nini kinaibiwa wapi?

Yeye hajali nani na nani wanaiba!

Anachojali ni,nani na nani wako na mimi katika kuhakikisha ninabaki Ikulu mpaka 2030.

Na hapo ndio unyonge wake mkuu ulipo!

Hata anapokamatwa mwizi,akiambiwa tu, mama hizi tunatafuta za kampeni 2025 dhidi ya Sukuma Gang!

Macho yanalegea zaidi!

Anatumia nguvu nyingi kupambana na Legacy ya Magufuli,badala ya kupambana na upotevu wa mali za nchi hii.

Kwa hali hii,Usishangae huko tuendako tukaja kuwa na rais mstaafu akiishi Oman au Dubai.
 
SSH aliangukia pua baada tu ya kuanza kupachika mafisadi kwenye serikali yake, mara walamba asali ,wauza pembe za ndovu nk. Angekuwa na dhamira angetusikiliza ,sasa yako wapi. Sukuma gang haijawahi kukumbwa na hii aibu ya mchana kweupe ,
Hivi Asaad alitoa ripoti ya upotevu wa trilion ngapi alipofukuzwa?
Halafu ccm ni moja hakuna ccm mbili.
 
Katika mchezo wa siasa unahitaji kuwa na akili nyingi sana kushinda "game". Lakini akili ya kwanza ni kumsoma, kumfahamu, kumwelewa aliyeketi kwenye kiti cha "executive" anawaza nini...
Je wizi uliotokea awamu ya sita unafananaje kwanza na ile 1.5 trilion pekee?
 
Katika mchezo wa siasa unahitaji kuwa na akili nyingi sana kushinda "game". Lakini akili ya kwanza ni kumsoma, kumfahamu, kumwelewa aliyeketi kwenye kiti cha "executive" anawaza nini...
Magufuli hakuwa dictator na wala hatokuwa tena. Wewe ni walewale walamba asali wa Nchi hii. Tumikeni tu siku zitafika siku moja.
 
Katika mchezo wa siasa unahitaji kuwa na akili nyingi sana kushinda "game". Lakini akili ya kwanza ni kumsoma, kumfahamu, kumwelewa aliyeketi kwenye kiti cha "executive" anawaza nini...
Mfumo CCM ulipo ni hatari kwa nchi hii.
 
Katika mchezo wa siasa unahitaji kuwa na akili nyingi sana kushinda "game". Lakini akili ya kwanza ni kumsoma, kumfahamu, kumwelewa aliyeketi kwenye kiti cha "executive" anawaza nini...
samia ameshinda kwa mbali kuhusu ripoti za cag kwani kwa sasa kila kitu kinawekwa wazi hakuna kuogopa,enzi za jpm vitu vingi vilifichwa
 
Mi najua kimantiki Bimkubwa wanamparura Bure tu maana hahitaji kuwa na uchungu wa Mali za nchi maana hakuingia urais Kwa kupambana kwenye majukwaa vijijini na mijini kwenye mavumbi Wala hakuhangaika kutengeneza figisu za kuiba kura za wapinzani na kusambaza masanduku ya kura feki na sasa tayari kanogewa.

Ni muda wake kuusoma mchezo na price anayolipa ni majizi kushika hatamu!

Baba yenu akija nitamwambia makosa yenu nyie nyie nyie stupid ibeni tu hamtaenda nazo kaburini!!
 
"Wazuri hawafi..." Sasa hata ungekuwa wewe ungetaka uwe mtu mbaya ili ufe?
 
Anawaza nini,hulka yake,tabia yake,ana uwezo gani:hii point imenitafakarisha Sana🤔🤔🤔
 
Hivi Asaad alitoa ripoti ya upotevu wa trilion ngapi alipofukuzwa?
Halafu ccm ni moja hakuna ccm mbili.
Kwa mtindo wa bitozo sukuma gang ingekwapua nadhani siieiigiii angeanzia huko kwa namna zumaridi anavyopambana na legacy
 
Uwa tuna conclude kwa kusema anashauriwa vibaya, kukwepa kusema neno halisi lenye kumfaha
 
SSH aliangukia pua baada tu ya kuanza kupachika mafisadi kwenye serikali yake, mara walamba asali ,wauza pembe za ndovu nk. Angekuwa na dhamira angetusikiliza ,sasa yako wapi. Sukuma gang haijawahi kukumbwa na hii aibu ya mchana kweupe ,
SSH alionesha udhaifu sana pale alipokubali shinikizo la WACHINA kuwaachia wachina wote wahalifu waliokuwa kwenye jela zetu akiwemo yule mama QUEEN OF IVORY aliyeongoza genge la majangili waliosafisha tembo wetu huko mbugani!! Ingawa balozi Mbwelwa Kairuki alipinga kuwa hawakuachiwa ,ukweli ni kwamba yule mama hayuko gerezani bali amerudi China!!
 
Back
Top Bottom