Kwa Rwakatare je hii ni halali?

Kwa Rwakatare je hii ni halali?

William Mshumbusi

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2012
Posts
1,761
Reaction score
2,391
Kukaa rumande kwa zaidi ya saa 24 bila kufunguliwa mashitaka.

Je huu si uteswaji wa wazi. Au ndio yuko kizuizini?

Tumpokee lini mtaani kama shujaa kwa mkutano
 
Kukaa rumande kwa zaidi ya saa 24 bila kufunguliwa mashitaka.

Je huu si uteswaji wa wazi. Au ndio yuko kizuizini?

Tumpokee lini mtaani kama shujaa kwa mkutano

Ni kinyume kabisa cha sheria. Polisi wanafanya kazi kwa upendeleo wa hali ya juu sana. Naamini pia wanafanya kazi kwa maelekezo. Yote haya mwisho. Naamini kabisa kuwa CCM na serikali yake wamepigwa upofu kabisa ili ukombozi wa nchi hii uweze kupatikana, vinginevyo madudu wanayofanya siyo ya kawaida!
 
Kukaa rumande kwa zaidi ya saa 24 bila kufunguliwa mashitaka.

Je huu si uteswaji wa wazi. Au ndio yuko kizuizini?

Tumpokee lini mtaani kama shujaa kwa mkutano
Masaa ishirini na nne kitu gani?Shk Ponda miezi mitano sasa yupo gerezani!Na ukiangalia uzito wa kosa la Lwakatare na la Ponda la Lwakatare ni kosa Kubwa mno.Kumuachia itahatarisha usalama wa wanahabari!
 
Pweru, sitaki kuzungumzia ponda nataka uniambia lwakatare hata kama ni yeye kwenye ile clip unamshtaki kwa kosa la kumdhuru nani? Ametajwa mwandishi wa mwananchi je yupo aliyedhurika, clip kwa mujibu wa aliyeileta inataka tuamini ni mpango wa mauaji je kuna namna yoyote imezungumzwa mtu afe? Nani ametajwa, kisheria polisi wana wakati mgumu, clip haijajitosheleza
 
Masaa ishirini na nne kitu gani?Shk Ponda miezi mitano sasa yupo gerezani!Na ukiangalia uzito wa kosa la Lwakatare na la Ponda la Lwakatare ni kosa Kubwa mno.Kumuachia itahatarisha usalama wa wanahabari!

Tumia akili wewe, Sheikh Ponda alishafikishwa mahakamani. Kama huna unalolijua ni bora kukaa kimya kuliko kuonyesha utupu wako upstairs...
 
Masaa ishirini na nne kitu gani?Shk Ponda miezi mitano sasa yupo gerezani!Na ukiangalia uzito wa kosa la Lwakatare na la Ponda la Lwakatare ni kosa Kubwa mno.Kumuachia itahatarisha usalama wa wanahabari!

>Nikweli sheik ponda yupo gerezani lakini kesi yake iko mahakamani, hii yaweza kuwa sawa kisheria.
>ndio mana mawakiri wa Lwakatare walidai kesi anayotuhumiwa ijulikane na mahakama.
>Kisheria si sawa kukaa lumande zaidi ya masaa 24 na kesi kutopelekwa mahakamani.
 
Polisi wenyewe Elimu ya kuunga unga tu asa kazi watafanyaje? Roma Mkatoliki alisema kimbilio la waliofeli ni upolisi na ......
 
Masaa ishirini na nne kitu gani?Shk Ponda miezi mitano sasa yupo gerezani!Na ukiangalia uzito wa kosa la Lwakatare na la Ponda la Lwakatare ni kosa Kubwa mno.Kumuachia itahatarisha usalama wa wanahabari!


Ponda ni gaidi period.
 
Masaa ishirini na nne kitu gani?Shk Ponda miezi mitano sasa yupo gerezani!Na ukiangalia uzito wa kosa la Lwakatare na la Ponda la Lwakatare ni kosa Kubwa mno.Kumuachia itahatarisha usalama wa wanahabari!

Toa udini wako hapa, umesikia Lwakatare ni kiongozi wa dini? Makosa wanayotuhumiwa nayo yana uhusiano gani? Jifunike basi.
 
>Nikweli sheik ponda yupo gerezani lakini kesi yake iko mahakamani, hii yaweza kuwa sawa kisheria.
>ndio mana mawakiri wa Lwakatare walidai kesi anayotuhumiwa ijulikane na mahakama.
>Kisheria si sawa kukaa lumande zaidi ya masaa 24 na kesi kutopelekwa mahakamani.

Sheria hairuhusu mtu kushikiliwa na Polisi zaidi ya saa 24 lakini pia hairuhusu mtuhumiwa kunyimwa dhamana! Shehe Ponda kwanini ananyimwa dhamana? ameua? ni muhimu tuwe wakweli na wa wazi katika hili!
 
Toa udini wako hapa, umesikia Lwakatare ni kiongozi wa dini? Makosa wanayotuhumiwa nayo yana uhusiano gani? Jifunike basi.

Sheria za nchi hazibagui kuwa huyu ni Kiongozi wa dini au mwanasiasa!
 
Pweru, sitaki kuzungumzia
ponda nataka uniambia lwakatare hata kama ni yeye kwenye ile clip
unamshtaki kwa kosa la kumdhuru nani? Ametajwa mwandishi wa mwananchi
je yupo aliyedhurika, clip kwa mujibu wa aliyeileta inataka tuamini ni
mpango wa mauaji je kuna namna yoyote imezungumzwa mtu afe? Nani
ametajwa, kisheria polisi wana wakati mgumu, clip
haijajitosheleza

hayo ni masuala ya kuongelea mahakamani. rwakatare atashitakiwa kimazingira. kwanza ni kosa la jinai kwa mtu kupanga njama za kutaka kumdhuru mtu. adhabu yake ni sawa na kutekeleza tendo. mwache anyee debe kwanza ajifunze kuishi vizuri na watu. yule hatoki na kama akitoka waandishi wa habari watakula naye sahani moja. atang'olewa kucha zake na meno kavukavu
 
Tumia akili wewe,
Sheikh Ponda alishafikishwa mahakamani. Kama huna unalolijua ni bora
kukaa kimya kuliko kuonyesha utupu wako upstairs...

ilichukua muda gani kushitakiwa? na mbona anakosa haki ya dhamana wakati hajaua?
 
>Nikweli sheik ponda yupo gerezani lakini kesi yake iko mahakamani, hii yaweza kuwa sawa kisheria.
>ndio mana mawakiri wa Lwakatare walidai kesi anayotuhumiwa ijulikane na mahakama.
>Kisheria si sawa kukaa lumande zaidi ya masaa 24 na kesi kutopelekwa mahakamani.

polisi pia ina mamlaka ya kumweka mtu kizuizini kwa muda usiojulikana ikiwa kutoka kwake mtu huyo kutaathiri upelelezi.
 
Naona watu wanaanza kukosa ustaarabu ndani ya jamii forum mie napitatu!!
 
hayo ni masuala ya kuongelea mahakamani. rwakatare atashitakiwa kimazingira. kwanza ni kosa la jinai kwa mtu kupanga njama za kutaka kumdhuru mtu. adhabu yake ni sawa na kutekeleza tendo. mwache anyee debe kwanza ajifunze kuishi vizuri na watu. yule hatoki na kama akitoka waandishi wa habari watakula naye sahani moja. atang'olewa kucha zake na meno kavukavu
Atongwele we niambie mazingira yepi? Angekua amekutwa eneo la tukio ni sahihi, akifika mahakamani kama ushahidi wanategemea ile clip hakimu anaweza kumpiga mtu kibao, ukiita njama za kumdhuru mtu, yupi huyo mtu? Wao wamezungumzia mambo yao ndani ya nyumba yao pasipo kuwa na vielelezo vyovyote vya kuwa walijiandaa kufanya uhalifu, na ndo maana polisi wanashinda kwa lwakatare kutafuta chochote cha kuwasaidia kuwa kielelezo cha kumkamata, narudia kwa ile clip its 0+0=0
 
Ndugu hili swali hata ipite miaka mia hawawezi kujibu,kwao wao haki ni yao tu!ya wengine sio haki.
Haki yao kina nani, na wengine ni akina nani? Kinachozungumzwa hapa tunasema lwakatare anapaswa kupelekwa mahakamani sheria hairuhusu mtu kukaa selo zaidi ya saa 24 sasa tatizo liko wapi?
 
Haki yao kina nani, na wengine ni akina nani? Kinachozungumzwa hapa tunasema lwakatare anapaswa kupelekwa mahakamani sheria hairuhusu mtu kukaa selo zaidi ya saa 24 sasa tatizo liko wapi?

Ni haki kwa Lwakatare pekee?
 
Back
Top Bottom