Kwa sasa Katiba mpya ni hisani ya Rais, akitaka atatekeleza

Kwa sasa Katiba mpya ni hisani ya Rais, akitaka atatekeleza

safuher

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2019
Posts
11,837
Reaction score
17,412
Mama samia akiamua mchakato wa katiba mpya kwa sasa itakuwa kafanya hisani tu na wala isisemwe ni takwa la wananchi.

Ilani ya chama cha mapinduzi hawakuahidi katiba mpya hivyo haipo katika mambo ambayo wanatakiwa wayatekeleze.

Kama ambavyo watu wanawaponda wana CCM kwamba kuna mambo katika ilani yao hawajayatekeleza basi ndivyo wana CCM wanahaki ya kukataa kutekeleza kila ambacho hakimo katika ilani yao.

Laiti mama samia angeombwa kujenga mashule na barabara asingesema apewe muda ili akuze uchumi kisha atajenga kwasababu ni jambo ambalo wanatakiwa kulitekeleza katika ilani yao.
 
Mods naomba isomeke "akitaka kutekeleza"
 
Back
Top Bottom