Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Wasalaam,
Sina uhakika kama taarifa hii imewahi kutolewa hapa. Nimewahi kupita ila sijawahi kuishi hapa.
Nchini Afrika ya Kusini kuna Condom ya kike imezinduliwa (muda kidogo umepita)ambayo inasaidia 'wakati wa kubakwa'. Nimesema hivyo kwa sababu aliyegundua anasema inazuia kubakwa lakini hapa kwetu sidhani kama inazuia. Kubaka kwa sheria zetu ni kitendo cha kumuingilia mwanamke bila ridhaa yake na kumuingilia ashakum si matusi ni kuingiza hata 'kichwa'. Hiyo ndiyo sheria.
Condom hiyo inayoitwa Rapex inavaliwa na mwanamke kila atokapo nyumbani na kuelekea maeneo hatarishi. Inachofanya ni mara baada ya mwanaume kuingiza 'anachoingiza' inabana na kumchoma huku ikisbabisha maumivu makali. Ili kuitoa ni lazima aende hospitali kutolewa na condom hiyo inauwezo wa kukusanya DNA ya mbakaji.
Kuna mambo yanayoweza kujitokea au maswali ya kujiuliza;
1. Je kina dada wengine hawatatumia kukomoa?
2. Je mbakaji hatapata hasira na kutenda kosa kubwa zaidi kama mauaji?
3. Condom hiyo inavaliwa kila mara hiyohiyo au inabidi kubadilishwa hata kama mtu hajabakwa?
4. Hapa kwetu itafaa? Lakini mbakaji akishaingiza kisheria si amebaka na aliyebakwa anakuwa ameshabakwa?
Kwa ninavyoona ni vizuri kwa wanaume ukamkinga mwenza wako kwa kumnunulia na kumshauri avae kila mara akienda ofisini kwa bosi wake, akienda kwenye party za wakora, akiwa anakunywa bila kipimo nk. Pia mwanao wa kike inaweza kumsaidia.
Maoni na mawazo tofauti yatasaidia.
Sina uhakika kama taarifa hii imewahi kutolewa hapa. Nimewahi kupita ila sijawahi kuishi hapa.
Nchini Afrika ya Kusini kuna Condom ya kike imezinduliwa (muda kidogo umepita)ambayo inasaidia 'wakati wa kubakwa'. Nimesema hivyo kwa sababu aliyegundua anasema inazuia kubakwa lakini hapa kwetu sidhani kama inazuia. Kubaka kwa sheria zetu ni kitendo cha kumuingilia mwanamke bila ridhaa yake na kumuingilia ashakum si matusi ni kuingiza hata 'kichwa'. Hiyo ndiyo sheria.
Condom hiyo inayoitwa Rapex inavaliwa na mwanamke kila atokapo nyumbani na kuelekea maeneo hatarishi. Inachofanya ni mara baada ya mwanaume kuingiza 'anachoingiza' inabana na kumchoma huku ikisbabisha maumivu makali. Ili kuitoa ni lazima aende hospitali kutolewa na condom hiyo inauwezo wa kukusanya DNA ya mbakaji.
Kuna mambo yanayoweza kujitokea au maswali ya kujiuliza;
1. Je kina dada wengine hawatatumia kukomoa?
2. Je mbakaji hatapata hasira na kutenda kosa kubwa zaidi kama mauaji?
3. Condom hiyo inavaliwa kila mara hiyohiyo au inabidi kubadilishwa hata kama mtu hajabakwa?
4. Hapa kwetu itafaa? Lakini mbakaji akishaingiza kisheria si amebaka na aliyebakwa anakuwa ameshabakwa?
Kwa ninavyoona ni vizuri kwa wanaume ukamkinga mwenza wako kwa kumnunulia na kumshauri avae kila mara akienda ofisini kwa bosi wake, akienda kwenye party za wakora, akiwa anakunywa bila kipimo nk. Pia mwanao wa kike inaweza kumsaidia.
Maoni na mawazo tofauti yatasaidia.